Uchaguzi 2020 Sakata la Sheikh Ponda na "masheikh rasmi"

Madaraja ni sehemu ya maisha na hayakuja kuondoka ili watu wote tulingane,Cha msingi pambania maisha yako achana na siasa uchwara.Hata hao unaowapigania waingie madarakani nao wanatembelea VX na wana maisha mazuri,Ila Shida yao ni wanafiki.

Sawa kabisa, ila tunataka wanaotembelea VX sasa na kuharibu biashara zetu, na wao waje mtaani wafaidi kazi ya mikono yao.
 
Sasa Mzee wangu, ikitokea Wakatoliki au walutheri au wakristo wote kwa ujumla wakatangaza kura ni kwa flani(upande tofauti na aliochagua sheikh wako) kama alivyofanya Sheikh Ponda unadhani nini kitatokea baada ya matokeo!?
Hao wote mbona inajulikana wapo CCM ndugu au wewe upo Nchi gani ??
 
..mimi kitendo cha kusalimia "Bwana Yesu Asifiwe" na " Asalaam Aleykum" ktk shughuli za kiserikali naona tayari ni UDINI.

..Na jambo hili lilianza kidogo-kidogo awamu ya Mzee Kikwete, lakini likashika kasi kubwa kabisa ktk awamu ya Raisi Magufuli.

..Magufuli alianza kualika viongozi wa Dini ktk kila shughuli za Kiserikali, kitu ambacho huko nyuma hakikuwa kikifanyika.

..Sasa kama Magufuli amekuwa akijihalalisha kupitia viongozi wa dini, basi lazima wapinzani wake nao watajaribu kupita humohumo alikopita yeye.

..Kama kila shughuli au tukio la kiserikali iliyoko madarakani linahusisha viongozi wa dini, kwanini walioko nje na wanaotaka kuunda serikali nao wasihusishe viongozi wa dini ktk harakati zao?

..Lakini kibaya walichokuwa wakifanya viongozi wa dini waliokuwa wako karibu na Magufuli ni kuleta element za kiimani ktk maamuzi ya serikali. Yaani walikuwa wanahubiri kwamba anayoyafanya Magufuli na serikali yake yanaongozwa au yanahalalishwa na maandiko matakatifu ktk misahafu.

..Aliyetufikisha hapa ni Magufuli, na tatizo lake ni kwamba hana kipaji cha kuongoza, na kujenga hoja zenye ushawishi kwa wananchi. Hali hiyo ndiyo inayomsababisha awatumie viongozi wa dini kama "bakora" ya kusimama, vinginevyo atadondoka kisiasa.
 
Ni vizuri umetambua hilo.
Sio nimetambua bali nimeonesha tatizo,kwa sababu bila ccm huyo Magufuli asingekuwa hapo alipo na watu wameanza kulalamikia ccm kabla ya Magufuli,sasa nashangaa sasa hivi watu hasira zote zimeamishiwa kwa Magufuli tu wakati wanajua tatizo ni ccm.

Hata suala la masheikh wa uamsho walikamatwa na serikali hii ya ccm chini ya JK ila lawama anabebeshwa Magufuli.
 
Sheikh Ponda angekuwa anatueleza waislamu ni faida zipi ambazo tutazipata sie kama waislamu kwa kumpigia kura TunduALissu.
 
Sio nimetambua bali nimeonesha tatizo,kwa sababu bila ccm huyo Magufuli asingekuwa hapo alipo na watu wameanza kulalamikia ccm kabla ya Magufuli,sasa nashangaa sasa hivi watu hasira zote zimeamishiwa kwa Magufuli tu wakati wanajua tatizo ni ccm.

Hata suala la masheikh wa uamsho walikamatwa na serikali hii ya ccm chini ya JK ila lawama anabebeshwa Magufuli.
Sasa unamtenganisha vipi Magufuy na ccm? Mbona mazuri yote anasema ni yeye ndio amefanya na amevunja rekodi?

Iweje kwenye mabaya hasiusike yeye? Au yeye ni wa mazuri tu mabaya ya kina Mbowe?
 
Mkuu nichangie kidogo. Bakwata wao watangaze hadharani na mufti wao eti mitano tena. Akija huyu akisema mitano kwanza ndio nongwa. Nahisi wanaogopa km Tundu Lissu akichukua nchi wao na familia zao watakua hawana vibarua wachumia tumbo hawa.

Mwisho kabisa wewe ni verified member na kuna wachangiaji naona km wanakujua wengine wanakuita mzee. Waweza weka picha yako nikuone? Asante na samahani lkn.
Kwa kukusaidia, nenda Facebook search Mohamed Said utamkuta huko utapata maarifa makubwa na ufahamu kupitia kalamu yake.
 
SAKATA LA SHEIKH PONDA: MASIKINI "MASHEIKH RASMI" HAWAJUI KUWA HAWANA WAISLAM WANAOWAONGOZA, WAKO PEKE YAO

Awali ya yote mimi sitajiingiza katika propaganda za uchaguzi bali nitajaribu kueleza hali ya Waislam ilivyo.

Kwanza ni kuwa Waislam toka ilipovunjwa EAMWS na serikali mwaka wa 1968 na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir kukamatwa na kufukuzwa nchini na serikali kuwaundia Waislam BAKWATA, Waislam wameishi na kinyongo miaka yote sasa inafika nusu karne.

Ndiyo unasikia lugha za "sheikh wa BAKWATA," Waislam wakijiweka mbali na BAKWATA.

Na ukweli ni kuwa BAKWATA haijaweza kukubalika na sababu ni ndogo kuwa si taasisi iliyoundwa na Waislam wenyewe.

Matokeo yake ni kuwa katika hii jamii kubwa ya Kiislam Waislam wana viongozi wao wanaowakubali, kuwaamini, kuwapenda na kuwasikiliza wanachowaambia.

Sheikh Ponda ni mmoja wa masheikh hawa.

Sheikh Ponda amewaeleza Waislam nani adui ya Waislam wa Tanzania na akasimama kupambana na adui huyu huku akiungwa mkono na Waislam wengi sana.

Katika juhudi hizi Sheikh Ponda kakutwa na shida nyingi.

Kalipa kwa ajili ya Allah kwa machozi na damu.

Kwa damu yake na machozi ya nduguze Waislam.

Nimeweka hapa FB makala fupi ya maisha ya Sheikh Ponda katika kuwatumikia Waislam sasa mtafute sheikh yeyote wa BAKWATA ambae amepata kusimama na Waislam katika dhiki na shida zao.

Hakuna.

Katika hali kama hii ni tabu sana kujaribu kumchafua sheikh kwa propaganda hizi za uchaguzi kwa kuwa Waislam wanamjua Ponda ni nani.

Ponda anawakilisha sauti ya Waislam wengi, wengi, wengi sana.

Wako waliotambua hili na wamejua nini wafanye waweze kupata kura za Waislam.

Hawa ni watu wenye kufikiri na kukubali ukweli kuwa Waislam wanaishi na kinyongo dhidi ya utawala kwa miaka mingi.

Hawa wametumia fursa hii kwa kuhaidi kutoka haki na fursa sawa kwa wote.

Ndiyo maana hujasikia Waislam wamefanya maandamano kumpinga Sheikh Ponda.

Wanaompinga Sheikh Ponda si masheikh bali ni "masheikh wa BAKWATA."

Chunguza.

Picha: Kulia ni Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir (1880 - 1979) na kushoto ni Sheikh Issa Ponda.
na hapo wamekosa la kusema coz shekhe Ponda anamtetea mkristu ingekuwa muislam ndo wangemzushia kedekede,hakika awamu hii yamewakuta
 
1) Mzee Said unataka kusema kwamba waislamu wakimchagua Lissu mgombea alienadiwa na Ponda ndio matatizo ya waislamu yataisha, au huyo mgombea atakuwa sababu ya waislamu kuingia peponi?

2) Kwa mwendo huu wa Ponda kuwaambia waislamu wamchague Lissu akitokea kiongozi anaekubalika na wakristo wengi nae akasema wakristo wamchague JPM, huoni kwamba tunaelekea kuligawa taifa kidini?

Natanguliza shukran zangu kwako Mzee wetu Said wa jukwaa la history.
kwanza hakuna kiongozi wa kikristo anayekubalika na wakrsto halafu akasema eti mchague magufuli
 
SAKATA LA SHEIKH PONDA: MASIKINI "MASHEIKH RASMI" HAWAJUI KUWA HAWANA WAISLAM WANAOWAONGOZA, WAKO PEKE YAO

Awali ya yote mimi sitajiingiza katika propaganda za uchaguzi bali nitajaribu kueleza hali ya Waislam ilivyo.

Kwanza ni kuwa Waislam toka ilipovunjwa EAMWS na serikali mwaka wa 1968 na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir kukamatwa na kufukuzwa nchini na serikali kuwaundia Waislam BAKWATA, Waislam wameishi na kinyongo miaka yote sasa inafika nusu karne.

Ndiyo unasikia lugha za "sheikh wa BAKWATA," Waislam wakijiweka mbali na BAKWATA.

Na ukweli ni kuwa BAKWATA haijaweza kukubalika na sababu ni ndogo kuwa si taasisi iliyoundwa na Waislam wenyewe.

Matokeo yake ni kuwa katika hii jamii kubwa ya Kiislam Waislam wana viongozi wao wanaowakubali, kuwaamini, kuwapenda na kuwasikiliza wanachowaambia.

Sheikh Ponda ni mmoja wa masheikh hawa.

Sheikh Ponda amewaeleza Waislam nani adui ya Waislam wa Tanzania na akasimama kupambana na adui huyu huku akiungwa mkono na Waislam wengi sana.

Katika juhudi hizi Sheikh Ponda kakutwa na shida nyingi.

Kalipa kwa ajili ya Allah kwa machozi na damu.

Kwa damu yake na machozi ya nduguze Waislam.

Nimeweka hapa FB makala fupi ya maisha ya Sheikh Ponda katika kuwatumikia Waislam sasa mtafute sheikh yeyote wa BAKWATA ambae amepata kusimama na Waislam katika dhiki na shida zao.

Hakuna.

Katika hali kama hii ni tabu sana kujaribu kumchafua sheikh kwa propaganda hizi za uchaguzi kwa kuwa Waislam wanamjua Ponda ni nani.

Ponda anawakilisha sauti ya Waislam wengi, wengi, wengi sana.

Wako waliotambua hili na wamejua nini wafanye waweze kupata kura za Waislam.

Hawa ni watu wenye kufikiri na kukubali ukweli kuwa Waislam wanaishi na kinyongo dhidi ya utawala kwa miaka mingi.

Hawa wametumia fursa hii kwa kuhaidi kutoka haki na fursa sawa kwa wote.

Ndiyo maana hujasikia Waislam wamefanya maandamano kumpinga Sheikh Ponda.

Wanaompinga Sheikh Ponda si masheikh bali ni "masheikh wa BAKWATA."

Chunguza.

Picha: Kulia ni Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir (1880 - 1979) na kushoto ni Sheikh Issa Ponda.
Hayo unayoeleza yamepitwa na wakati. Yoote yalishaelezwa enzi za Mkapa na Kikwete na wakati huo yaliigawa nchi (hasa mitandaoni) katika makundi ya chuki. Kubenea na yule mwalimu wa chuo kikuu cha Dar Es Salaam na wewe pia walikuwa wakuu kupenyeza hizi chuki kwa Watanzania. Sasa naona na wewe unaanza kupenyeza hizi chuki za kuwagawa Watanzania. Ebu tueleza Ponda kafanikisha kipi ambacho Wailslam hawakuwa nacho kama sio kula hela ya kikundi cha Kiislam cha Saudi Arabia kinachoitwa Wahhabi. Tunajuwa kikundi hicho na mrengo wake wa Wahhabism kina pesa nyingi za kuwapa wake na Ponda kwa ajili ya destabilzation siyo wasiyowaislamu tuu, bali hata kwa Waislamu wenzao. Ponda na kundi lake hupata nguvu za kipesa kutoka huko kueneza chuki kati ya Waislamu na Waislamu na pia kati ya Waislamu na wasio waislamu na naona ndiyo wimbo unaimba wewew sasa hivi. Achana na fikra za kuwagawa Watanzania. UKITAKA HAMIA SAUDI ARABIA UJIUNGE NA WAHHABBI, LAKINI NASIKIA HWAMKARIBISHI JITU JEUSI KAMA WEWE.
 
na hapo wamekosa la kusema coz shekhe Ponda anamtetea mkristu ingekuwa muislam ndo wangemzushia kedekede,hakika awamu hii yamewakuta
Hamtetei mkristu wala Muislamu, anatetea umbo lake. Anajaribu kuonyesha pesa ya Wahhabbui haijapotea inatumika vizuri.
 
Hao wakatoliki na walutheri ni wa Tanzania hii au nchi nyingine.Hivi Katika Tanzania kuna mtu au jamii ambayo haijapitia chungu ya shubiri ya Huyu mungu wa chato?
Mimi sijapitia na sijaiona
 
Kwa kukusaidia, nenda Facebook search Mohamed Said utamkuta huko utapata maarifa makubwa na ufahamu kupitia kalamu yake.
Poa poa

Aaah nimeenda Mohamed Said wako kibao. Who is who God knows.
 
Kama ni upande unaotoa haki hakuna shida ila kama sio haki Wakristo wote wanajua watampa LISSU mtetezi wa haki hao hawana cha kuambiwa. Tatizo ni waislamu wamekandamizwa miaka 10 sasa na bado wamelala tu.

We umesikia padre gani kawekwa mahabusu hata siku moja tu eti ni gaidi au kamsema vibaya serikali. Waislamu amkeni mmelemazwa Sana na BAKWATA. Sisi Wakatoliki Magufuli tukimuita tu anakuja fasta.
That is very true

Nyie wenzetu mnaweza kuisema serikali na kuikosoa sisi tunatakiwa kuisifia kila siku na hili halikubaliki.
 
Hujui lolote, mzee ponda ni mnufaika wa mali za waislam, aliponyang’anywa (tena waliosimamia arejeshe hizo mali na waislam wenzie waliokuwa wanamtuhumu), sasa kabaki kutumia udhaifu wenu kupandikiza chuki, na magaidi wote wanatumia hiyo mbinu, si unakumbuka mlivyokuwa mnaunga mkono ugaidi?
Jambo moja tu mimi ninalolielewa Waislam awamu hii wanakwenda na Lissu full stop!
 
Waislamu tunajua ni nani mtetezi wetu, nani wa kumwamini na ni nani msanii; sijui kwa nini mashekh wote wa Tz wamepanic again Sheikh Ponda.
 
Sasa Mzee wangu, ikitokea Wakatoliki au walutheri au wakristo wote kwa ujumla wakatangaza kura ni kwa flani(upande tofauti na aliochagua sheikh wako) kama alivyofanya Sheikh Ponda unadhani nini kitatokea baada ya matokeo!?
Kwani nani alikwambia kuna mtu kwenye dini ana influence kura zetu.

Hivyo wewe anayekuambia cha kufanya ni mchungaji, sheikh au padri?!

Hata Pope akipanda jukwaani aseme asemacho kura ni kwa Lisu na chadema tu.

HAKI utangulia kabla ya amani.
 
Back
Top Bottom