Troll JF
JF-Expert Member
- Feb 6, 2015
- 7,804
- 12,224
SHAKA AUNGURUMA
Maneno yaliosemwa na bavicha yanatakiwa kupuuzwa na watanzania werevu wenye kuitakia mema nchi yetu"
Vikra na mitazamo ya BAVICHA inapaswa kulaumiwa kwani wameonyesha utovu wa nidhamu kwa Serikali"
"Tukio la Lissu si la kuleta siasa, si la kuanza kuchochea vurugu"
"Umoja wa Vijana wa chama cha mapinduzi unawakanya Bavicha waache kiherehere.
"UVCCM inawakanya BAVICHA kuacha kiherehere wakati huu ambao vyombo vya dola inatimiza wajibu wao"
"UVCCM inaunga mkono kwa mara ya kwanza kauli ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ambae alitaka tusinyoosheane kidole"
"UVCCM inaomba Mwenyezi Mungu amponye Mhe. Tundu Lissu arudi kwenye majukumu yake kama kawaida"- Shaka
"Matamshi ya BAVICHA yana nia na lengo la kupalilia chuki na hasama kwan yamethubutu kuingilia medani za kintelejinsia na upelelezi" - Shaka
"Kuishutumu Serikali na na kudai eti inaendeshwa kwa mfumo kandamizi si tu kama ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa adabu" - Shaka
Tukio la kushambuliwa Mhe. Lissu na watu wasiojulikana si jambo dogo na jepesi kama inavyochukuliwa na BAVICHA na viongozi wake" - Shaka
"Yapo matukio mengi huko nyuma yamewahi kutokea. Mengine yamepoteza maisha ya viongozi wa juu wa Serikali kabla hili la Mhe. Lissu" - Shaka
"BAVICHA wamekwepa kutaja kiini cha kifo cha kushangaza cha Marehemu Chacha Zakayo Wangwe." - Shaka
"Mbowe ametamka matamshi yaliopevuka kifikra na kisiasa tofauti na povu lilivyowatoka vijana wake na kuonyesha uchanga katika siasa" - Shaka
"UVCCM tulitegemea kuona ujasiri wao wanaojigamba na kuwapa kiburi, wangehoji mazingira tata ya vifo vya Malima na Ditopile" - Shaka
"UVCCM tunaendelea kushauri ni vema kwa wakati huu tukaongozwa na busara kuliko pupa na ushabiki" - Shaka
"UVCCM tunamuomba Mwenyezi Mungu amponye Mhe. Lisu aje kushirikiana na Watanzania wenzake kujenga na kuliendeleza taifa letu." - Shaka