Kuna jamaa mmoja amezidi sana kuchakachua,sijui ana pepo la ngono au amechanjia!!!Hivi kweli ni halali kuchakachua watu watatu wa familia moja???Jamaa alianza kutembea na dada mmoja(rika lake)-baadae wakaachana.Baada ya muda akaanza kutoka na mdogo wa huyo dada(wa tumbo moja) baadae wakamwagana!sasa majuzi kashuhudiwa (nami miongoni mwao) anatembea na mama mzazi wa hao wadada wawili.Nina amini asilimia 80 mama anafahamu mwanae (mdada wa kwanza) alitembea na huyo kijana sasa sijui kwa nini nae kamkubali.Mama huyo ana kazi yake na alitengana na mumewe ila anaishi na hao mabinti kwenye nyumba yake.Hii ni nini laana au vipi??Tumsaidiaje huyu jamaa aache hiyo tabia.Kuna watu watadhani ni hadithi ya kutunga ila hii imetokea laivu.Kabla sijamvaa kumpa counselling naomba maoni yenu