wana jf, salaamKufuatia wimbi la mageuzi ya kisiasa kushika kasi hapa nchini, baadhi ya wachambuzi wa mambo ya siasa wamesikika kwa nyakati tofauti wakisema kuwa eti CCM imepungua mvuto mbele ya jamii. lakini mimi napingana vikali na mtazamo huu kwani naamini kuwa CCM haijawahi kuwa na mvuto wowote kwa jamii. CCM ni ileile haikuwahi kuwa na lolote na sasa haina lolote. kinachotokea sasa ni matokeo ya mwamko wa wananchi juu ya mambo mbalimbali yahusuyo mustakbali wa maisha yao na maendeleo kwa ujumla.