Sababu za kutomwamini Prof.Lipumba

mmaroroi

JF-Expert Member
May 8, 2008
2,960
544
1. Anawaponda wapinzani wenzake.
2. Amechuja kwa kugombea mara ya nne.
3. Alishatumika na Serikali bila mafanikio.
4. Chama chake(CUF) kina makubaliano na CCM huko Zanzibar,wakati CCM kinakumbatia ufisadi/mafisadi.
5. Haamini kuchuka kwa bei ya bidhaa za ujenzi wakati malighafi inapatikana Tanzania.
NDIVYO NINAVYOONA WEWE JE ?
 
Huyu Lipumba ana chuki kwa sana kwa akili yake anafikiri PHD zake ndizo zinaweza kuongoza nchi. Ebu fikiria hajawahi kuwa hata mbunge wala baba wa familia je ni nchi ataweza kuongoza.
 
Mimi naona yafuatayo,

1. Kuhusu kuponda vyama vingine. kweli hapa Prof alichemsha. Alipaswa kutumia muda zaidi kwenye kunadi sera za chama chake na sio kukosoa sera za vyama vingine. Suala la kukosoa vyama ni la mpiga kura sio la mgombea. Mpiga kura ndio anapaswa kuamua nani zaidi. Watanzania wanataka kujua atawafanyia nini na kwa njia gani na sio porojo.

2. Kuhusu kugombea mara nne, kama wanachama wa CUF wameridhia Prof. kugombania mara ya nne kwangu hapa sioni tatizo. Kila chama kina taratibu zake za kupata mgombea wa chama chake.

3. Hoja ya "Alishatumika na Serikali bila mafanikio." inaitaji ushaidi makini. Navyojua Prof. ajawahi kutumika kama na serikali kama mtu mwenye maamuzi ya mwisho. Alikuwa anafanyakazi ya ushauri zaidi. Swali, una ushahidi gani kama alipotoa ushauri bosi wake aliupuuza pengine kwa maslahi binafis hata kama ushauri huo ulikuwa mzuri?

4. Kuhusu makubaliano ya CUF na CCM Zanzibar sitii neno.

5. Haamini kushuka kwa bei ya bidhaa za ujenzi: Kiuchumi kushuka kwa bei za bidhaa mbalimbali kunawezekana, nadhani Lipumba akiwa kama mchumi analielewa hili vizuri sema tuu labda alipitiwa au alikuwa na maana ya tofauti au alikosa muda wa kulielezea kwa kinagaubaga. Kama amesahau naomba ni mkumbushe baadhi ya topic kwenye uchumi ambazo zinaweza kumpa mwananchi nafuu kwenye bei. Baadhi ya topic hizo ni price discrimination(bei ndogo kwa watu wa kipato kidogo na kubwa kwa watu wa kipato kikubwa), government interventionist, subsidies (serikali inauweza kumlipia mwananchi asilimia fulani ya bei), Supply theories (ongezeko la makampuni ya watoa huduma hushusha bei ya huduma) etc. Hivyo hapa Prof. Lipumba kama alimaanisha alichosema basi alikosea kwani kiuchumi bei kushuka inawezekana.



1. Anawaponda wapinzani wenzake.
2. Amechuja kwa kugombea mara ya nne.
3. Alishatumika na Serikali bila mafanikio.
4. Chama chake(CUF) kina makubaliano na CCM huko Zanzibar,wakati CCM kinakumbatia ufisadi/mafisadi.
5. Haamini kuchuka kwa bei ya bidhaa za ujenzi wakati malighafi inapatikana Tanzania.
NDIVYO NINAVYOONA WEWE JE ?
 
mimi naona yafuatayo,

1. Kuhusu kuponda vyama vingine. Kweli hapa prof alichemsha. Alipaswa kutumia muda zaidi kwenye kunadi sera za chama chake na sio kukosoa sera za vyama vingine. Suala la kukosoa vyama ni la mpiga kura sio la mgombea. Mpiga kura ndio anapaswa kuamua nani zaidi. Watanzania wanataka kujua atawafanyia nini na kwa njia gani na sio porojo.

2. Kuhusu kugombea mara nne, kama wanachama wa cuf wameridhia prof. Kugombania mara ya nne kwangu hapa sioni tatizo. Kila chama kina taratibu zake za kupata mgombea wa chama chake.

3. Hoja ya "alishatumika na serikali bila mafanikio." inaitaji ushaidi makini. Navyojua prof. Ajawahi kutumika kama na serikali kama mtu mwenye maamuzi ya mwisho. Alikuwa anafanyakazi ya ushauri zaidi. Swali, una ushahidi gani kama alipotoa ushauri bosi wake aliupuuza pengine kwa maslahi binafis hata kama ushauri huo ulikuwa mzuri?

4. Kuhusu makubaliano ya cuf na ccm zanzibar sitii neno.

5. Haamini kushuka kwa bei ya bidhaa za ujenzi: Kiuchumi kushuka kwa bei za bidhaa mbalimbali kunawezekana, nadhani lipumba akiwa kama mchumi analielewa hili vizuri sema tuu labda alipitiwa au alikuwa na maana ya tofauti au alikosa muda wa kulielezea kwa kinagaubaga. Kama amesahau naomba ni mkumbushe baadhi ya topic kwenye uchumi ambazo zinaweza kumpa mwananchi nafuu kwenye bei. Baadhi ya topic hizo ni price discrimination(bei ndogo kwa watu wa kipato kidogo na kubwa kwa watu wa kipato kikubwa), government interventionist, subsidies (serikali inauweza kumlipia mwananchi asilimia fulani ya bei), supply theories (ongezeko la makampuni ya watoa huduma hushusha bei ya huduma) etc. Hivyo hapa prof. Lipumba kama alimaanisha alichosema basi alikosea kwani kiuchumi bei kushuka inawezekana.


u r truly great thinker nakupa tano........
 
u r truly great thinker nakupa tano........

Na jana kalifunika jiji,mpaka ccm na chadema wameogopa,pale jangwani ule umma haujawahi kutokea ktk kampeni za mwaka huu..

Halafu anamwaga sera si mchezo,anajua jinsi ya kuongea, mpaka niliongea na mfuasi mmoja wa chama kimoja anasema sisi kwenye mikutano yetu ni matusi tu kwenda mbele,lkn ukimsikiliza Lipumba raha tupu,huyu ndie Rais. anasema huyo mfuasi. uzuri wake kaenda shule,na akienda kwenye kampeni hatokei bar..
 
ni kibaraka wa ccm. Jukumu alilopewa na mwajiri wake ccm ni kugawa kura za upinzani, cuf na ccm ni damu damu na hata kwenye nyaraka za shura ya maimamu iko hivyo.
 
Siku zimekwisha yamtu ya nini, tuseme ya ya nchi, yao ni yakwao tu, ninavyofikiri mimi, lipumba anachuki za ainafulani kwakuwa chama chake kimeshuka sn chati hapa TZ bara, naona kama anachukuliwa kura zake za 19kweuzi wakati Ukombozi nikuafundisha mafisadi juu ya yote waliyoyafanya ilikuikomboa TZ huru bila sisem, amesahau kuwa adui wa dini zote ni shetani ibilisi, wakati adui wa wapinzani wote ni sisiem, imempasa kutokkutia neno kwa wapinzani wenzake, pia aachekuonyesha kama redet walivyojifanya wanajua zaidi kwakuwa wako UD, kuwa watakachosema ni kweli hata kama ni uongo watu wasiofika UD au waliopitia mahalipengine au wanafunzi wao watawakubali.
Usijambe mbele yawatoto ukamsingizia mmoja wao watajua tu ni wewe, na siyo mwezao japo ni watoto, Lipumba see a new era, you have to make amargamation to fight for the people from sisiem domination upon the poor TZs.
ndiyo nionayo mimi.
 
Na jana kalifunika jiji,mpaka ccm na chadema wameogopa,pale jangwani ule umma haujawahi kutokea ktk kampeni za mwaka huu..

Halafu anamwaga sera si mchezo,anajua jinsi ya kuongea, mpaka niliongea na mfuasi mmoja wa chama kimoja anasema sisi kwenye mikutano yetu ni matusi tu kwenda mbele,lkn ukimsikiliza Lipumba raha tupu,huyu ndie Rais. anasema huyo mfuasi. uzuri wake kaenda shule,na akienda kwenye kampeni hatokei bar..

Nimependa style yao ya kampeni nakiri umati ule ulikuwa mkubwa sana na kampeni zao wamefanyia kwa kutumia usafiri wa barabara na wameweza kutembea mikoa yote isipokuwa singida tu. Wamelala vijijini wamepita kwenye barabara wanazopita wananchi wa kawaida kwahiyo wanajua adha ya wananchi nina muda wa kuwafikiria pengine nitatia kura yangu kwao.

Tunataka watu wenye analitiko data sio wanaofokafoka na kutokwa na povu la mdomo, tunataka viongozi wastaarabu sio wenye harufu ya kuleta machafuko. Tutumie busara kufanya maamuzi.
 
Mimi naona yafuatayo,

1. Kuhusu kuponda vyama vingine. kweli hapa Prof alichemsha. Alipaswa kutumia muda zaidi kwenye kunadi sera za chama chake na sio kukosoa sera za vyama vingine. Suala la kukosoa vyama ni la mpiga kura sio la mgombea. Mpiga kura ndio anapaswa kuamua nani zaidi. Watanzania wanataka kujua atawafanyia nini na kwa njia gani na sio porojo.

2. Kuhusu kugombea mara nne, kama wanachama wa CUF wameridhia Prof. kugombania mara ya nne kwangu hapa sioni tatizo. Kila chama kina taratibu zake za kupata mgombea wa chama chake.

3. Hoja ya "Alishatumika na Serikali bila mafanikio." inaitaji ushaidi makini. Navyojua Prof. ajawahi kutumika kama na serikali kama mtu mwenye maamuzi ya mwisho. Alikuwa anafanyakazi ya ushauri zaidi. Swali, una ushahidi gani kama alipotoa ushauri bosi wake aliupuuza pengine kwa maslahi binafis hata kama ushauri huo ulikuwa mzuri?

4. Kuhusu makubaliano ya CUF na CCM Zanzibar sitii neno.

5. Haamini kushuka kwa bei ya bidhaa za ujenzi: Kiuchumi kushuka kwa bei za bidhaa mbalimbali kunawezekana, nadhani Lipumba akiwa kama mchumi analielewa hili vizuri sema tuu labda alipitiwa au alikuwa na maana ya tofauti au alikosa muda wa kulielezea kwa kinagaubaga. Kama amesahau naomba ni mkumbushe baadhi ya topic kwenye uchumi ambazo zinaweza kumpa mwananchi nafuu kwenye bei. Baadhi ya topic hizo ni price discrimination(bei ndogo kwa watu wa kipato kidogo na kubwa kwa watu wa kipato kikubwa), government interventionist, subsidies (serikali inauweza kumlipia mwananchi asilimia fulani ya bei), Supply theories (ongezeko la makampuni ya watoa huduma hushusha bei ya huduma) etc. Hivyo hapa Prof. Lipumba kama alimaanisha alichosema basi alikosea kwani kiuchumi bei kushuka inawezekana.
No.2 Kwa kugombea mara nyingi angejua kuwa hafai hivyo angejaribu Ubunge au angerudi Chuo kikuu kufundisha.
No.3 Kwa kutumika na serikali hajawahi kujiuzulu kwa kutosikilizwa ushauri wake.
No.4 Sema usikwepe,inakuwaje chama kiwe na misimamo tofauti bara na visiwani,yaani visiwani muafaka,bara usiwepo?
No.5 Umedhihirisha mwenyewe bingwa wa uchumi anavyoshindwa kuchanganua mambo ya uchumi sasa chuo kikukuu alikuwa anafundisha nini? Mpiga kura moja kichwani.
 
Nimependa style yao ya kampeni nakiri umati ule ulikuwa mkubwa sana na kampeni zao wamefanyia kwa kutumia usafiri wa barabara na wameweza kutembea mikoa yote isipokuwa singida tu. Wamelala vijijini wamepita kwenye barabara wanazopita wananchi wa kawaida kwahiyo wanajua adha ya wananchi nina muda wa kuwafikiria pengine nitatia kura yangu kwao.

Tunataka watu wenye analitiko data sio wanaofokafoka na kutokwa na povu la mdomo, tunataka viongozi wastaarabu sio wenye harufu ya kuleta machafuko. Tutumie busara kufanya maamuzi.

Sasambona chama chenyewe kinazidi kupwaya kwa kukimbiwa na watu makini kama akina Lwakatare.Halafu mbona kinahubiriwa misikitini?Hebu tueleze.
 
Sasambona chama chenyewe kinazidi kupwaya kwa kukimbiwa na watu makini kama akina Lwakatare.Halafu mbona kinahubiriwa misikitini?Hebu tueleze.

Hilo silijui kama una ushahidi weka link msikiti gani ili tuone kwenye video.
 
ni kibaraka wa ccm. Jukumu alilopewa na mwajiri wake ccm ni kugawa kura za upinzani, cuf na ccm ni damu damu na hata kwenye nyaraka za shura ya maimamu iko hivyo.

Hapo umenena kwani visiwani ni maridhiano/muafaka na bara kazi maalum ya kupunguza kura za wapinzani.Mpiga kura kazi kwako kwa ukombozi.
 
Hilo silijui kama una ushahidi weka link msikiti gani ili tuone kwenye video.

Leo ni ijumaa nenda kwenye misikiti wakati wa ibada au uliza waliosikia watakuambia kwani hawanong'oni wanatumia vipasa sauti.
 
Leo ni ijumaa nenda kwenye misikiti wakati wa ibada au uliza waliosikia watakuambia kwani hawanong'oni wanatumia vipasa sauti.

kakobe aliposema maisha binafsi ya padre hayana maana kumkosesha kura alikuwa anampigia kampeni bila kipaza sauti? udini ni uislamu tu?
 
1. Anawaponda wapinzani wenzake.
2. Amechuja kwa kugombea mara ya nne.
3. Alishatumika na Serikali bila mafanikio.
4. Chama chake(CUF) kina makubaliano na CCM huko Zanzibar,wakati CCM kinakumbatia ufisadi/mafisadi.
5. Haamini kuchuka kwa bei ya bidhaa za ujenzi wakati malighafi inapatikana Tanzania.
NDIVYO NINAVYOONA WEWE JE ?

Hata siku moja hajaibua mafisadi hadharini. Hivyo, hajiamini.
 
CUF imekaa kidini zaidi, hata Prof. mwenyewe kwenye mahojiano ITV alikubali kwamba chama chake kimekita kampeni zake zaidi kwenye maeneo yenye waislam wengi (Tanga, Pwani, Dar, Lindi, Mtwara, Tunduru, Tabora). Pia anashabikia dhana potofu kwamba Waislamu wanakandamizwa hasa katika kupewa elimu hivyo kunadi ajenda ya Haki Sawa inayoendeleza chuki kati ya dini mbili kubwa hapa nchini. Anachangia mgawanyiko zaidi kuliko kuleta umoja wa kitaifa anaouhubiri.
 
Back
Top Bottom