Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Tumeshaona mara nyingi mambo ya serikali yakishughulikiwa na familia ya Kikwete. Pamoja na kusemwa sana hadharani, ndio kwanza familia hii inaendelea na mtindo huo. Mfano mmoja ni huu:
...................................................................................................................................
JK atasuluhisha migogoro ya mipaka - Mama Salma
Na Lulu George
21st September 2010
Mama Salma Kikwete ambaye ni mke wa mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amesema chama hicho kikishinda katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, serikali yake itatatua migogoro ya mipaka.
Amesema migogoro ya mipaka ni miongoni mwa kero zinazowaathiri wananchi wengi, hivyo utatuzi wake utafanyika ndani ya miaka mitano ijayo.
Mama Salma aliyasema hayo jana mjini hapa, wakati akizungumza na wanachama wa CCM, kupitia Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa chama hicho (UWT) katika wilaya ya Tanga.
Alisema, serikali ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha inatatua kero zinazoikabili jamii likiwemo suala la migogoro ya mipaka.
Hata hivyo, Mama Salma alisema kero ya migogoro ya mipaka limeanza kushughulikiwa na serikali ya CCM kupitia ofisi ya Waziri Mkuu.
"Serikali ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha kwamba changamoto mbalimbali zinazowakabili zinatatuliwa, ikiwemo ile ya migogoro ya mipaka…suala hili lipo kwa Waziri Mkuu na tayari linashughulikiwa na punde utatuzi utapatikana,"alisema.
Pia Mama Salma alisema katika miaka mitano ijayo, serikali itaongeza mtaji kwa lengo la kuwawezesha wanawake kiuchumi.
Pia Mama Salma alisema serikali itatekeleza mpango wa ufufuaji na kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo, ili kuharakisha kasi ya maendeleo na ukuaji wa uchumi.
CHANZO: NIPASHE
...................................................................................................................................
JK atasuluhisha migogoro ya mipaka - Mama Salma
Na Lulu George
21st September 2010
Mama Salma Kikwete ambaye ni mke wa mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amesema chama hicho kikishinda katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, serikali yake itatatua migogoro ya mipaka.
Amesema migogoro ya mipaka ni miongoni mwa kero zinazowaathiri wananchi wengi, hivyo utatuzi wake utafanyika ndani ya miaka mitano ijayo.
Mama Salma aliyasema hayo jana mjini hapa, wakati akizungumza na wanachama wa CCM, kupitia Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa chama hicho (UWT) katika wilaya ya Tanga.
Alisema, serikali ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha inatatua kero zinazoikabili jamii likiwemo suala la migogoro ya mipaka.
Hata hivyo, Mama Salma alisema kero ya migogoro ya mipaka limeanza kushughulikiwa na serikali ya CCM kupitia ofisi ya Waziri Mkuu.
"Serikali ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha kwamba changamoto mbalimbali zinazowakabili zinatatuliwa, ikiwemo ile ya migogoro ya mipaka…suala hili lipo kwa Waziri Mkuu na tayari linashughulikiwa na punde utatuzi utapatikana,"alisema.
Pia Mama Salma alisema katika miaka mitano ijayo, serikali itaongeza mtaji kwa lengo la kuwawezesha wanawake kiuchumi.
Pia Mama Salma alisema serikali itatekeleza mpango wa ufufuaji na kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo, ili kuharakisha kasi ya maendeleo na ukuaji wa uchumi.
CHANZO: NIPASHE