Ni nini lakini kilitokea?
Kutokana na sababu nilizozitaja hapo juu, CHADEMA iliamua kujipanga kama jeshi la myamvuli. Ikaingia vitani ikiwa imedhamiria kuibana CCM kila kona. Iliweka mpango wa kufika Igunga mara tu baada ya kusikia habari kwamba Rostam Aziz alikuwa amejivua gamba; likatoka na ngozi na hatimaye kuvuja damu ya ubunge mpaka ikaisha.
Walipeleka timu ambayo imeishi ndani ya jimbo la Igunga siku 47 kabla ya kampeni za ubunge kuanza. Wakiwa Igunga wameweza kuweka mtandao wa chama ndani ya kata zote 26 na vijiji vyote 98.
Kinachotambulishwa kama jeshi la magaidi lililoingizwa na CHADEMA kutoka nje ya Igunga ni uwongo mtupu! Nimefuatilia jimbo zima nikagundua kwamba baada ya chama kukubalika mpaka ngazi ya vijiji, CHADEMA waliwahamasisha wanavijiji wote kujiundia kamati zao za ulinzi na usalama. Kwa hiyo katika kila kijiji na kitongoji, wananchi wa eneo hilo ndio walinzi na wana usalama wa CHADEMA. Hawaruhusu upuuzi wowote kwenye eneo lao.
Ni bahati mbaya kwamba CCM ilichukua vijana watanowatano kutoka kila kijiji ikawapeleka kwenye makambi ya kuwafundisha ugaidi ili waje wawashambulie wana CHADEMA na kung'oa mabango ya mgombea wao na bendera za chama hicho. Pia waliandaliwa kutumika kwa kushirikiana na vijana waliotoka nje ya jimbo hili kuwatisha wananchi wote wanaoiunga mkono CHADEMA na kuwalisha mkong'oto wale wote wanaokataa amri zao.
Lakini kwa kuwa CHADEMA inatumia wananchi wenyewe wa eneo husika kama walinzi, ina maana wanawafahamu vijana hao wote wanaotumiwa na CCM kigaidi. Vijana hao wanakabiliwa na nguvu ya umma ya kijiji mpaka wanashindwa kufanya lolote. Lakini pia inakuwa rahisi kuwakamata watu wote wanaojihusisha na kuihujumu CHADEMA. Mkuu wa wilaya aliyeamua kuisaidia CCM alinaswa vivyo hivyo na wananchi ambao walimripoti kwa viongozi wa chama. Mabalozi waliokuwa wanaandikisha kadi za kupiga kura walikamatwa kwa intelijensia ya nguvu ya umma kijijini.
Kwa ujumla CCM wamebanwa kila kona. CHADEMA wamekaba mpaka penalti na sasa CCM imekubali kuwa chama cha upinzani kwa kulalamika kila siku.
Kwa herini CCM!
Ahsante kwa majibu yako na tumekuelewa! kwani wewe uko Igunga? Na kama uko Igunga hebu basi tueleze wananchi wa Igunga wanalizukaka nilikuwa busy na kutafuta mlo wa kila siku ...............................mimi siyo mwandishi wa makala hii nimetoa ufafanuzi wa hili katika post mojawapo
habari zinatabanaisha kuwa igunga ina wapiga kura 170,586 waliopiga kura uchaguzi uliopita ni chini ya asilimia hamsini,sasa wale ndugu zetu wa CUF wakitoa kile wanachoita mtaji wao wa wapiga kura 10,000 ingawa ni imani yangu idadi hii inaweza kupungua zinabaki 160,586.Hapa kuna la kujiuliza
je kwa nini idadi ndogo ilipiga kura?
je ni wangapi watapiga kura?
je kama ambao hawakupiga kura kura hawakuona umuhimu wa kupigia CCM kwa kukosa imani nao ja watapigia CUF ambao hawakuwapigia mwanzo?
Je wale waliopigia CUF au CCM kwasababu walikosa mbadala watapigia wapi?
Nimetazama vyama zaidi kuliko mgombea hapa tena kuna la kujiuliza CUF ni mgombea yule yule ila CCM na CDM ni wagombea tofauti?