Sababu kubwa ya vijana wa Mbeya kuwazidi nguvu polisi.

Ozzie

JF-Expert Member
Oct 9, 2007
3,217
1,259
Bila shaka ni tukio la kwanza na la aina yake, kwamba polisi walishindwa kuwathibiti vijana wa jiji la Mbeya ambao walikuwa wakipambana nao kwa zaidi ya masaa ishirini. Kila sehemu ilisikika milio ya risasi na mabovu ya kutoa machozi. Hofu ya risasi ilisababisha kijana Mushi mkazi wa Uyole ayumbeyumbe akiwa pembezoni mwa barabara kuu na kusababisha agongwe na gari, na mpaka sasa kakatwa mguu wa kulia. Tukio hili lilihitaji msaada zaidi wa polisi toka wilaya za mkoa wa Mbeya, pia toka mkoa wa Sumbawanga, Iringa na Dar es Salaam.
Kwa hakika vijana hawa ambao wamevikwa jina la wamachinga (japo ukweli wamachinga walikuwa wachache sana; na wengi wa vijana hawa ni wale waliozaliwa kipindi cha miaka ya mwishoni mwa themanini na mwanzo wa miaka ya tisini) wamekatishwa tamaa ya maisha na utawala ulioko madarakani.
Ghasia zilianza maeneo ya Mwanjelwa wakati wakiwa na harakati za kujadiliana kuhusu kutimizwa kwa ahadi yao ya kupatiwa eneo la kufanyia biashara toka mamlaka za jiji na mkoa. Askari kadhaa wa jiji hawakufurahishwa na kusanyiko la vijana hawa kwa kuwa lilifanyika eneo ambalo wao walikuwa wameweka doria na pia lilipigwa marufuku kufanyia biashara za kimachinga. Hili likaleta majibizano yaliyosababisha vipigo vilivyoishia kuleta FFU na tukaishia kupata hadithi iliyopo mpaka sasa.
Walianza kwa kufunga barabara kwa njia nyingi ikiwa ni pamoja na kutumia mawe, kuchoma matairi n.k. Eneo la mama John ndio kulikuwa na pingamizi kubwa kwa kuwa waliweza kung’oa miti mikubwa iliyopo kandokando ya barabara kama tembo vile na kufunga njia.
Vijana hawa walipata nguvu kubwa pale Jeshi la Wananchi walipokuwa wakipita maeneo ya Soweto na Mama John walipoomba wafunguliwe njia kwa muda ili waweze kupita kwa kuwa wao ugomvi huo ulikuwa hauwahusu. Wanajeshi hao walikuwa wanapita barabara kuu iendayo Iringa, ambapo mwanzoni walikuwa wakipita kwenye service road mpaka walipofika sehemu ambayo iliwalazimu watumie njia kubwa ambayo ni kiunganishi cha eneo wanalokwenda. Hii ikawa sababu kubwa ya vijana wa Mbeya kupata nguvu. Ingawa kuna matukio yaliyoripotiwa kwa wanajeshi kutumia nguvu kwa baadhi ya watu, lakini haikuwa sana vile.
Vijana hawa walikuwa na ushirikiano wa kustaajabisha na wakaweza kupambana na polisi. Madereva taksi wa Soweto wanasimulia kwamba kwenye kituo cha daladala cha Soweto, ambako kuna container la taka kama la tani kumi hivi, liliwezwa kuwekwa barabarani baada ya majaribio mawili ya vijana hawa kushindwa. Baadaye, waliamua kuvunja mabango ya mahoteli mashuhuri, pamoja na kituo cha mafuta Oilcom Soweto ili watumie machuma yake kubebea hili container ambalo ndani yake lilikuwa lina moto wa kuteketeza taka.
Tunashukuru mapambano yameisha, tunawapa pole majeruhi na ndugu wa marehemu Kelvin Mwalongo. Bila shaka kila mtu ataona kuwa raia wamekuwa washindi dhidi ya polisi na serikali kwani serikali inazidi kupata ujumbe ya kwamba kutumia mabavu si njia sahihi. Na kwamba watu wameshawachoka, hivyo waanze kuwasikiliza wananchi na hasa vijana. Hili ni somo kubwa kwa watawala!!!!
 
Pamoja na uzuri wa mada yako hujasema ni nini kimewatuliza vijana na kufikia muafaka japo wa muda.Nakushauri fanya editing kidogo.
 
badala wagombane na wazazi wao walio warithisha umaskini wakati wengine wanawarithisha utajiri
 
Nadhani hata hao polisi nao walikuwa upande wa wamachinga
katika bango hili kuna ukweli ndani yake
386523_241433489251932_100001558489297_681046_1251734107_n[1].jpg
 
Bila shaka ni tukio la kwanza na la aina yake, kwamba polisi walishindwa kuwathibiti vijana wa jiji la Mbeya ambao walikuwa wakipambana nao kwa zaidi ya masaa ishirini. Kila sehemu ilisikika milio ya risasi na mabovu ya kutoa machozi. Hofu ya risasi ilisababisha kijana Mushi mkazi wa Uyole ayumbeyumbe akiwa pembezoni mwa barabara kuu na kusababisha agongwe na gari, na mpaka sasa kakatwa mguu wa kulia. Tukio hili lilihitaji msaada zaidi wa polisi toka wilaya za mkoa wa Mbeya, pia toka mkoa wa Sumbawanga, Iringa na Dar es Salaam.
Kwa hakika vijana hawa ambao wamevikwa jina la wamachinga (japo ukweli wamachinga walikuwa wachache sana; na wengi wa vijana hawa ni wale waliozaliwa kipindi cha miaka ya mwishoni mwa themanini na mwanzo wa miaka ya tisini) wamekatishwa tamaa ya maisha na utawala ulioko madarakani.
Ghasia zilianza maeneo ya Mwanjelwa wakati wakiwa na harakati za kujadiliana kuhusu kutimizwa kwa ahadi yao ya kupatiwa eneo la kufanyia biashara toka mamlaka za jiji na mkoa. Askari kadhaa wa jiji hawakufurahishwa na kusanyiko la vijana hawa kwa kuwa lilifanyika eneo ambalo wao walikuwa wameweka doria na pia lilipigwa marufuku kufanyia biashara za kimachinga. Hili likaleta majibizano yaliyosababisha vipigo vilivyoishia kuleta FFU na tukaishia kupata hadithi iliyopo mpaka sasa.
Walianza kwa kufunga barabara kwa njia nyingi ikiwa ni pamoja na kutumia mawe, kuchoma matairi n.k. Eneo la mama John ndio kulikuwa na pingamizi kubwa kwa kuwa waliweza kung’oa miti mikubwa iliyopo kandokando ya barabara kama tembo vile na kufunga njia.
Vijana hawa walipata nguvu kubwa pale Jeshi la Wananchi walipokuwa wakipita maeneo ya Soweto na Mama John walipoomba wafunguliwe njia kwa muda ili waweze kupita kwa kuwa wao ugomvi huo ulikuwa hauwahusu. Wanajeshi hao walikuwa wanapita barabara kuu iendayo Iringa, ambapo mwanzoni walikuwa wakipita kwenye service road mpaka walipofika sehemu ambayo iliwalazimu watumie njia kubwa ambayo ni kiunganishi cha eneo wanalokwenda. Hii ikawa sababu kubwa ya vijana wa Mbeya kupata nguvu. Ingawa kuna matukio yaliyoripotiwa kwa wanajeshi kutumia nguvu kwa baadhi ya watu, lakini haikuwa sana vile.
Vijana hawa walikuwa na ushirikiano wa kustaajabisha na wakaweza kupambana na polisi. Madereva taksi wa Soweto wanasimulia kwamba kwenye kituo cha daladala cha Soweto, ambako kuna container la taka kama la tani kumi hivi, liliwezwa kuwekwa barabarani baada ya majaribio mawili ya vijana hawa kushindwa. Baadaye, waliamua kuvunja mabango ya mahoteli mashuhuri, pamoja na kituo cha mafuta Oilcom Soweto ili watumie machuma yake kubebea hili container ambalo ndani yake lilikuwa lina moto wa kuteketeza taka.
Tunashukuru mapambano yameisha, tunawapa pole majeruhi na ndugu wa marehemu Kelvin Mwalongo. Bila shaka kila mtu ataona kuwa raia wamekuwa washindi dhidi ya polisi na serikali kwani serikali inazidi kupata ujumbe ya kwamba kutumia mabavu si njia sahihi. Na kwamba watu wameshawachoka, hivyo waanze kuwasikiliza wananchi na hasa vijana. Hili ni somo kubwa kwa watawala!!!!

Hivi kweli unaona kuna dalili ya watawala wetu kusikiliza kwa nia ya dhati kilio cha wananchi?

Hawa watawala wana macho ila hawaoni; wana masikio lakini hawasikii!
 
Asante kwa taarifa. Bila shaka welevu wataanza kufanyia kazi hali inayosababisha machafuko ya namna hii.
 
Back
Top Bottom