Ruvuma: Ajali ya Fuso yaua Watu 13 na kujeruhi wawili Songea

Mrao keryo

JF-Expert Member
Aug 29, 2022
1,611
2,169
Watu 13 wamepoteza maisha na majeruhi kadhaa baada ya Fuso walilokuwa wanasafiria kutoka mnadani kutumbukia mtoni. Watu hao walitoka kijiji cha Nambendo wilaya ya Namtumbo kurudi Songea walikokwenda kuuza vitu mbalimbali jana siku ya Pasaka! Miili ya marehemu ipo hospitali ya mkoa wa Ruvuma. Pole kwa wote waliokumbwa na maafa hayo.

---------------- -------------
Singida 1.jpg

Singida 2.jpg


==================

Updates
Ajali hiyo imetokea wakati gari aina ya Mistubishi Fuso (T.800 BXB) lililokuwa limewabeba watu kutoka Ndongosi Mnadani kutumbukia mtoni wakati walipokuwa wakielekea Namatui, Aprili 9, 2023.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Marco Chilya amesema majeruhi wawili wamelazwa katika Kituo cha Afya Mpitimbi na miili ya marehemu ipo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.

Amesema uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha ajali ni ubovu wa barabara na utelezi kutokana na mvua.
 
Tatizo kubwa ni Kodi za magari kuwa kubwa watu wanaamua kuchukua Fuso tani nne na kuziongeza ziweze kubeba mzigo wa Tani kumi hizi fuso zote hazina tatizo la brake ila mfumo wa brake hawaubadilishi wanapoongeza mzigo sijajua kodi imefika ngapi kwa zile fuso za kubebea Mchanga Nchi ipo karibu na bandari magari huko nie yapo bei ya kutupwa mpaka leo watu wanasafiri kwenye maroli na Serikali inaona sawa inawapa kesi madereva wakati sio kweli...chanzo kikuu cha ajali ni kuwa na kodi kubwa kwa magari chakavu...
 
Watu 13 wamepoteza maisha na majeruhi kadhaa baada ya Fuso walilokuwa wanasafiria kutoka mnadani kutumbukia mtoni. Watu hao walitoka kijiji cha Nambendo wilaya ya Namtumbo kurudi Songea walikokwenda kuuza vitu mbalimbali jana siku ya Pasaka! Miili ya marehemu ipo hospitali ya mkoa wa Ruvuma. Pole kwa wote waliokumbwa na maafa hayo.

----------------
Watu 13 wamepoteza maisha na wengine wawili kujeruhiwa vibaya baada ya gari aina ya Fuso waliyokuwa wakisafiria kupoteza mwelekeo na kutumbukia mtoni majira ya saa 2: 30 usiku wa kuamkia leo.

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Wilman Ndile amesema gari hiyo ilikuwa imebeba wafanyabiashara waliokuwa wakitoka mnadani katika kijiji cha Ndongosi na walikuwa wakielekea kijiji jirani cha Namatuhi wilayani humo.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Songea na tayari ndugu wameitambua miili hiyo. DC Ndile amesema majeruhi wanaendelea na matibabu katika kituo cha Afya cha Namanditi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma Daktari Majura Magafu amethibitisha kupokelewa kwa miili 13 iliyotokana na ajali hiyo.

Kama kawaida sikiliza hadithi zile zile tokea polisi ... Hawana jipya na bila kuwaondoa hawa na kuwa na vyombo vilivyo elimika shida hii hadi nabii Issa kurudi mara ya pili.
 
Ndugu zangu,
Kuna taarifa kuwa Lori la mizigo (fuso) limepinduka huko songea na kusababisha vifo vya takribani watu 13,
Lori hilo lilibeba mizigo na wafanyabiashara ambao inasemekana walikuwa wanatoka mnadani.
IMG-20230410-WA0002.jpg
 
Kichwa Cha habari chajieleza watanzania 13 Leo wamekufa Kwa kupanda roli kutumbukia mtoni very shame aise.
 
Watu 13 wamepoteza maisha na majeruhi kadhaa baada ya Fuso walilokuwa wanasafiria kutoka mnadani kutumbukia mtoni. Watu hao walitoka kijiji cha Nambendo wilaya ya Namtumbo kurudi Songea walikokwenda kuuza vitu mbalimbali jana siku ya Pasaka! Miili ya marehemu ipo hospitali ya mkoa wa Ruvuma. Pole kwa wote waliokumbwa na maafa hayo.

---------------- -------------
View attachment 2583007
View attachment 2583008

==================

Updates
Ajali hiyo imetokea wakati gari aina ya Mistubishi Fuso (T.800 BXB) lililokuwa limewabeba watu kutoka Ndongosi Mnadani kutumbukia mtoni wakati walipokuwa wakielekea Namatui, Aprili 9, 2023.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Marco Chilya amesema majeruhi wawili wamelazwa katika Kituo cha Afya Mpitimbi na miili ya marehemu ipo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.

Amesema uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha ajali ni ubovu wa barabara na utelezi kutokana na mvua.
Hajari haina kinga lakini hii tabia ya polisi kuchukua rushwa wakawaruhusu wafanya biashara wa minada kuketi juu ya mizigo yao kwenye fusu ni hatari sana laki sasa nani wakiwazuia tarafiki wanaishi watakavyo hacha tukome na boda boda bajaji noah na mabasi
 
Back
Top Bottom