Rais wa Tanzania Samia aagiza majeruhi wote waliotokana na ajali iliyoua watu 25 mkoani Arusha watibiwe bure

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,304
Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel amesema Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameagiza majeruhi wote waliotokana na ajali iliyoua watu 25 mkoani Arusha watibiwe bure

Dkt Godwin Mollel amesema hayo leo Februari, 25, 2024 alipowajulia hali majeruhi wa ajali hiyo iliyohusisha magari manne eneo la Ngaramtoni, Mkoani Arusha waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mount Meru.

Dkt. Mollel amesema majeruhi wote wanaendelea vizuri na mmoja ndo kapewa Rufaa ya kwenda hospitali ya Rufaa ya Kanda KCMC Mkoani Moshi.

"Rais Samia Suluhu Hassan ametuelekeza majeruhi wote wa ajali hii kupatiwa matibabu bila kulipa gharama zozote"

Dkt. Mollel ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na watanzania kwa ujumla kuwa watulivu wakati wakiendelea kuwatibia majeruhi na kwa wale waliopoteza ndugu zao utaratibu wakupatiwa miili unaandaliwa na wataalamu.

Ajali hiyo imesababisha vifo vya watu 25 na majeruhi 21.

Credit - EastAfricaTV
 
Rais Samia aboreshe huduma za bima za afya Kwa wananchi. Hizi siasa cheap aachane nazo. Aagize wote waliopo mahospitalini mwezi huu nchi nzima watibiwe bure.
Taja rais aliyeboresha huduma za afya kwa muda mfupi sana kumzidi Samia nikuwekee ushahidi hapa.
 
Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel amesema Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameagiza majeruhi wote waliotokana na ajali iliyoua watu 25 mkoani Arusha watibiwe bure

Dkt Godwin Mollel amesema hayo leo Februari, 25, 2024 alipowajulia hali majeruhi wa ajali hiyo iliyohusisha magari manne eneo la Ngaramtoni, Mkoani Arusha waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mount Meru.

Dkt. Mollel amesema majeruhi wote wanaendelea vizuri na mmoja ndo kapewa Rufaa ya kwenda hospitali ya Rufaa ya Kanda KCMC Mkoani Moshi.

"Rais Samia Suluhu Hassan ametuelekeza majeruhi wote wa ajali hii kupatiwa matibabu bila kulipa gharama zozote"

Dkt. Mollel ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na watanzania kwa ujumla kuwa watulivu wakati wakiendelea kuwatibia majeruhi na kwa wale waliopoteza ndugu zao utaratibu wakupatiwa miili unaandaliwa na wataalamu.

Ajali hiyo imesababisha vifo vya watu 25 na majeruhi 21.

Credit - EastAfricaTV

Suluhisho ni kutibiwa wagonjwa wote kuhudumiwa kwa usawa. Kwanini hawa tu?
 
Wamefika 25?

Mwenye kisa kuhusu hii habari naomba,
Ninachosoma ni kwamba lori lilifakamia magari mengine,

Issue ni brake? Dereva? Na lilikua limebeba nini? maana kwa impact hio inaonesha Momentum(P=MV) ilikua kubwa sana.
 
Wamefika 25?

Mwenye kisa kuhusu hii habari naomba,
Ninachosoma ni kwamba lori lilifakamia magari mengine,

Issue ni brake? Dereva? Na lilikua limebeba nini? maana kwa impact hio inaonesha Momentum(P=MV) ilikua kubwa sana.
Inasemekana lori lilikuwa limebeba caterpillar; brakes zilipofeli likiwa out of control almost umbali wa 2km hadi lilipoparamia magari na kuuwa.

Wachambuzi wanahoji kwa umbali ule lililoserereka the driver could do something better badala ya kuwasha hazard na kupiga makelele. Anyway ndio hivyo imeshakuwa historia.
 
Wamefika 25?

Mwenye kisa kuhusu hii habari naomba,
Ninachosoma ni kwamba lori lilifakamia magari mengine,

Issue ni brake? Dereva? Na lilikua limebeba nini? maana kwa impact hio inaonesha Momentum(P=MV) ilikua kubwa sana.
Scania ilikuwa imebeba scaveter/buldozer (sjui kama inaandikwa hv) yale ya kutengeneza barabara.. kwa hiyo uzito wa scania ulikuwa mkubwa sana.labda nayo imechangia madhara kuwa makubwa.
 
Back
Top Bottom