Mwandishi Wetu, Morogoro
TATIZO la rushwa katika chaguzi za Chama Cha Mapinduzi (CCM), linaonekana kuzidi kukua baada ya uchaguzi wa viongozi wa chipukizi taifa kukumbwa na matukio ya utoaji takrima kwa wajumbe wa mkutano huo.
Habari zilizopatikana kutoka katika mkutano huo uliofanyika mjini Morogoro, Desemba 29 mwaka jana, zinaeleza baadhi ya wapambe wa wagombea waligawa pesa hadharani na wengine kukutana nao usiku wa manane.
Utoaji wa rushwa kwa wajumbe ulianza siku moja kabla ya uchaguzi huo ambapo wapambe wa wagombea hao watoto wadogo wa miaka kumi, walipita kwa wajumbe wakiomba kura na kutoa takrima mbalimbali zikiwamo pesa.
Katika uchaguzi huo ambao watoto wa vigogo ndani ya chama hicho waliibuka washindi, unaelezwa kuwa ni ishara mbaya kwa CCM kwa vile sasa hata watoto wadogo wa miaka 10, wanafundishwa kutoa na kupokea rushwa.
Wajumbe wa mkutano huo ni wenyeviti wote wa Chipukizi wilaya ambao ni watoto wa miaka 10 hadi 13, na makatibu wa Chipukizi na uhamasishaji wa wilaya ambao huwa ni vijana wakubwa.
Pia uchunguzi huo umebaini kuwa makatibu wa mikoa wa UVCCM ndio waliotumiwa na vigogo ndani ya CCM kupanga mkakati wa kuwawezesha watoto wao, kushinda katika uchaguzi huo.
"Hilo si siri kweli tuliitwa na baadhi ya watu ambao walijitambulisha walitumwa na kigogo na kupewa msimamo wa kuhakikisha kijana anashinda, tusimwangushe," alisema mjumbe mmoja wa mkutano huo.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Morogoro, Jonas Nkya alikanusha hayo akisema uchaguzi ulifanyika vizuri na yeye binafsi alishuhudia hakukuwepo vitendo vyovyote vya rushwa. Kigezo kingine ambacho Nkya alikichukulia kama sehemu ya uchaguzi kwenda vizuri ni kutokuwepo na malalamiko.
"Hadi sasa hakuna kiongozi wala mgombea ambaye amewasilisha malalamiko kuulalamikia," alisema Nkya huku akitoa wito wa yeyote ambaye hakuridhika na uchaguzi huo kutosita kuwasilisha malalamiko yake.
Baadhi ya wajumbe wengine wa mkutano huo, waliiambia Mwananchi Jumapili kwa masharti ya kutotajwa majina kuwa uchaguzi huo uligubikwa na rushwa kuchafuana majina miongoni mwa kambi hali iliyosababisha watoto wa vigogo kuibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi huo.
Walisema pamoja na kuweka msimamo wao mwanzo wa kuhakikisha hawawachagui watoto wa vigogo, msimamo huo ulishindikana kutokana na shinikizo la viongozi wa juu na kulainishwa kwa rushwa.
"Kwa kweli sisi wajumbe tulishaweka msimamo wetu baada ya kuona nafasi nyeti zote katika umoja wetu zinachukuliwa na watoto wa wakubwa na hivyo, kupendekeza tuwachague walalahoi wenzetu," alisema mmoja wa wajumbe wa mkutano huo kutoka Kanda ya Ziwa.
Baadhi ya wajumbe hao walidai msimamo huo uliwashtua baadhi ya viongozi wa juu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) taifa waliokuwepo mkoani hapa na kuamua kumshauri mmoja wa wagombea wa uchaguzi huo, Halfan Kikwete asitokee katika uchaguzi huo kwa kukwepa aibu ya kushindwa.
Waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Gabriel Makala ambaye ni mtoto wa Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM Taifa, Amos Makala kuwa Mwenyekiti mpya wa chipukizi taifa baada ya kupata kura 300 kati ya kura 357 zilizopigwa na hivyo kuwashinda wagombea wenzake saba waliojitokeza kuwania nafasi hiyo.
Mbali na Makala pia mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Halfan Kikwete alichaguliwa kuwa mjumbe wa baraza kuu kutoka Tanzania bara kwa kura 301 bila kuwako ukumbini hali mbayo iliwashangaza wafuatiliaji wengi wa uchaguzi huo.
Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na Mwananchi Jumapili katika uchaguzi huo, uliohudhuriwa na Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Emanuel Nchimbi, mshauri wa rais January Makamba, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM taifa, Amos Makala pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Issa Machibya ulibaini kulikuwepo na mazingira ya rushwa.
Mwandishi wa habari hii aliyekuwepo katika chuo cha ualimu Kigurunyembe siku moja kabla ya uchaguzi huo saa 7:00 usiku, alishuhudia vigogo mbalimbali wakiwaamsha wajumbe katika vyumba vyao na kugawa fedha kuwashawishi wawapigie kura wagombea wao.
Hata hivyo, habari zingine zimedai kuwa makatibu wa Chipukizi na Uhamasishaji waliitisha mgomo siku moja kabla ya uchaguzi huo wakidai posho waliyopewa ni ndogo na hivyo hata wakipiga kura hawatawachagua watoto wa vigogo.
Hatua hiyo ilimfanya kiongozi mmoja wa CCM kunusuru jahazi kwa kuwapa sh 30,000 kila mmoja na hivyo uchaguzi ukafanyika.
Source: Mwananchi Jumapili
TATIZO la rushwa katika chaguzi za Chama Cha Mapinduzi (CCM), linaonekana kuzidi kukua baada ya uchaguzi wa viongozi wa chipukizi taifa kukumbwa na matukio ya utoaji takrima kwa wajumbe wa mkutano huo.
Habari zilizopatikana kutoka katika mkutano huo uliofanyika mjini Morogoro, Desemba 29 mwaka jana, zinaeleza baadhi ya wapambe wa wagombea waligawa pesa hadharani na wengine kukutana nao usiku wa manane.
Utoaji wa rushwa kwa wajumbe ulianza siku moja kabla ya uchaguzi huo ambapo wapambe wa wagombea hao watoto wadogo wa miaka kumi, walipita kwa wajumbe wakiomba kura na kutoa takrima mbalimbali zikiwamo pesa.
Katika uchaguzi huo ambao watoto wa vigogo ndani ya chama hicho waliibuka washindi, unaelezwa kuwa ni ishara mbaya kwa CCM kwa vile sasa hata watoto wadogo wa miaka 10, wanafundishwa kutoa na kupokea rushwa.
Wajumbe wa mkutano huo ni wenyeviti wote wa Chipukizi wilaya ambao ni watoto wa miaka 10 hadi 13, na makatibu wa Chipukizi na uhamasishaji wa wilaya ambao huwa ni vijana wakubwa.
Pia uchunguzi huo umebaini kuwa makatibu wa mikoa wa UVCCM ndio waliotumiwa na vigogo ndani ya CCM kupanga mkakati wa kuwawezesha watoto wao, kushinda katika uchaguzi huo.
"Hilo si siri kweli tuliitwa na baadhi ya watu ambao walijitambulisha walitumwa na kigogo na kupewa msimamo wa kuhakikisha kijana anashinda, tusimwangushe," alisema mjumbe mmoja wa mkutano huo.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Morogoro, Jonas Nkya alikanusha hayo akisema uchaguzi ulifanyika vizuri na yeye binafsi alishuhudia hakukuwepo vitendo vyovyote vya rushwa. Kigezo kingine ambacho Nkya alikichukulia kama sehemu ya uchaguzi kwenda vizuri ni kutokuwepo na malalamiko.
"Hadi sasa hakuna kiongozi wala mgombea ambaye amewasilisha malalamiko kuulalamikia," alisema Nkya huku akitoa wito wa yeyote ambaye hakuridhika na uchaguzi huo kutosita kuwasilisha malalamiko yake.
Baadhi ya wajumbe wengine wa mkutano huo, waliiambia Mwananchi Jumapili kwa masharti ya kutotajwa majina kuwa uchaguzi huo uligubikwa na rushwa kuchafuana majina miongoni mwa kambi hali iliyosababisha watoto wa vigogo kuibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi huo.
Walisema pamoja na kuweka msimamo wao mwanzo wa kuhakikisha hawawachagui watoto wa vigogo, msimamo huo ulishindikana kutokana na shinikizo la viongozi wa juu na kulainishwa kwa rushwa.
"Kwa kweli sisi wajumbe tulishaweka msimamo wetu baada ya kuona nafasi nyeti zote katika umoja wetu zinachukuliwa na watoto wa wakubwa na hivyo, kupendekeza tuwachague walalahoi wenzetu," alisema mmoja wa wajumbe wa mkutano huo kutoka Kanda ya Ziwa.
Baadhi ya wajumbe hao walidai msimamo huo uliwashtua baadhi ya viongozi wa juu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) taifa waliokuwepo mkoani hapa na kuamua kumshauri mmoja wa wagombea wa uchaguzi huo, Halfan Kikwete asitokee katika uchaguzi huo kwa kukwepa aibu ya kushindwa.
Waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Gabriel Makala ambaye ni mtoto wa Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM Taifa, Amos Makala kuwa Mwenyekiti mpya wa chipukizi taifa baada ya kupata kura 300 kati ya kura 357 zilizopigwa na hivyo kuwashinda wagombea wenzake saba waliojitokeza kuwania nafasi hiyo.
Mbali na Makala pia mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Halfan Kikwete alichaguliwa kuwa mjumbe wa baraza kuu kutoka Tanzania bara kwa kura 301 bila kuwako ukumbini hali mbayo iliwashangaza wafuatiliaji wengi wa uchaguzi huo.
Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na Mwananchi Jumapili katika uchaguzi huo, uliohudhuriwa na Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Emanuel Nchimbi, mshauri wa rais January Makamba, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM taifa, Amos Makala pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Issa Machibya ulibaini kulikuwepo na mazingira ya rushwa.
Mwandishi wa habari hii aliyekuwepo katika chuo cha ualimu Kigurunyembe siku moja kabla ya uchaguzi huo saa 7:00 usiku, alishuhudia vigogo mbalimbali wakiwaamsha wajumbe katika vyumba vyao na kugawa fedha kuwashawishi wawapigie kura wagombea wao.
Hata hivyo, habari zingine zimedai kuwa makatibu wa Chipukizi na Uhamasishaji waliitisha mgomo siku moja kabla ya uchaguzi huo wakidai posho waliyopewa ni ndogo na hivyo hata wakipiga kura hawatawachagua watoto wa vigogo.
Hatua hiyo ilimfanya kiongozi mmoja wa CCM kunusuru jahazi kwa kuwapa sh 30,000 kila mmoja na hivyo uchaguzi ukafanyika.
Source: Mwananchi Jumapili