Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Hapa Mgambo akimfukuza mpiga picha bia kujua kuwa wapiga picha walikuwa wawili mwingine alijificha , halafu mgambo ni hakika hajui mambo ya kuzoom
Picha liliendelea kwa askari huyu wa Jiji la Dar es Salaam alipomkuta mama huyu amesimama pembezoni mwa jengo la IPS jijini Dar na kuanza kumfokea pindo alipomuomba kidogo dogo ili asimfikishe ofisini kwao.
... Baada ya kumalizia mazungumzo alichukua kidogo dogo kwa staili ambayo si rahisi mtu kujua alichokuwa akifanya. Mambo kama haya ndiyo wanayoyafanya askari hawa wa jiji la Dar kwa kunyanyasa wananchi hasa akina mama pindi wanapowakuta wamepaki vibaya magari yao. Lakini jambo la kushangaza kwa nini magari hasa ya viongozi/serikali yakipaki hayasumbuliwi
baada ya kuwa amekula kidogo dogo kutoka kwa mwanamama na kumuachia akaondoka, zilipita dakika 3 tu ndipo lilipokuja gari lililokuwa limeandikwa Wizara ya Kazi na Ajira (W KA), na kupaki ila hawakulifanya lolote