Chachasteven
JF-Expert Member
- Jul 4, 2014
- 1,881
- 1,850
Mashindano ya taji la Miss Tanzania kwa mwaka 2020 yamefika tamati leo tarehe 5/12/2020 na Mshindi wake kutangazwa kutokana na maoni ya majaji na wapiga kura. Jina lake anaitwa Rose Manfere na namba yake ya ushiriki ilikuwa ni namba 14. Huyu ndiye ataiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Miss world huko Brazil. Kwenye historia ya mataji ya Miss Tanzania, Ukitoa lile la Miss Tanganyika aliloshinda mzungu mmoja wa kikoloni, huyu anakuwa ni Miss wa 24 tangu mwaka 1964. Baadhi ya picha zake.
Orodha ya Mamiss waliomtangulia huku ikiambatana na mwaka waliochukua mataji:
Video inayoonesha Rose akitangazwa ushindi wa Taji la Miss Tanzania 2020.
Orodha ya Mamiss waliomtangulia huku ikiambatana na mwaka waliochukua mataji:
Jina | Mwaka |
Theresa Shayo | 1967 |
Aina Maeda | 1994 |
Emily Adolf | 1995 |
Shose Sinare | 1996 |
Saida Kessy | 1997 |
Basila Mwanukuzi | 1998 |
Hoyce Temu | 1999 |
Jacqueline Ntuyabaliwe | 2000 |
Happiness Magese | 2001 |
Sylvia Bahame | 2003 |
Faraja Kotta | 2004 |
Nancy Sumari | 2005 |
Wema Sepetu | 2006 |
Richa Adhia | 2007 |
Nasrin Karim | 2009 |
Miriam Gerald | 2009 |
Genevieve Emmanuel | 2010 |
Salha Israel | 2011 |
Brigitee Alfred | 2012 |
Happiness Watimanywa | 2013 |
Lilian Kamazima | 2014 |
Diana Edward | 2016 |
Queen Elizabeth Makune | 2018 |
Rose Manfere | 2020 |
Video inayoonesha Rose akitangazwa ushindi wa Taji la Miss Tanzania 2020.