Mlengo wa Kati
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 2,730
- 492
Yericko rose kamili ukiacha fungu la hela lakini pia kakutwa na shahada zaidi ya 137 za wapiga kura! Shahada kazitoa wapi na zanini?
nngu007
===>Prapaganda za Magamba,sina uhakika na hiki,ngoja tusubiri maelezo
kutoka Tumaini Makene
Kurugenzi ya Habari.
Huu uzi ulifutwa mara ya kwanza sijui kwa nini wakati picha inaongea.Rose kamili mikonöni mwa polisi.
Chagadema na rushwa damu damu
...
Mbunge wa Viti Maalum, Rose Kamili alikuwa akifanya kikao cha ndani Kijiji cha Kitawaya, Kata ya Luhota, ghafla yeye pamoja name makamanda wengine wanawake aliokuwa nao pamoja wakazingirwa na kikosi cha Green Guard vijana wa CCM.
Wakaanza kumpiga na kumdhalilisha vibaya kisha wakampeleka ofisi za CCM Mkoa wa Iringa kwa maelekezo ya viongozi wao kitaifa na mkoa waliokuwa kwenye mkutano wao was kufunga uliofanyika eneo la Kidamali.
Sasa baadae wakagundua kuwa suala hilo litakuwa gumu kwao ndiyo ikatungwa hiyo propaganda ya kwamba wamemkata kwa rushwa il I wajenge uhalali wa kumpiga na udhalilishaji waliomfanyia.
Polisi walienda kumchukua Mama Kammili akiwa ofisi ya CCM Mkoa ambako walikuwa wakiendelea kumdhalilisha.
Tunafuatilia kwa makini na kina suala hili na tutaendelea kuwapatia taarifa.
CCM iko kwenye wakati mgumu sana wa kukabiliana na ukweli wa kushindwa uchaguzi was Kalenga na kukataliwa na wananchi mchana name usiku.
Ni sawa na mtu anayetapatapa kufa maji.
Taarifa ya a wali...
Source : Kurugenzi ya Habari
Tupia mkuu.Kunapicha akiwa na Fuko la Feza naipandisha Muda si Mrefu Ngoja nifike kwenye PC yangu hapa Natumia Simu.Achana na Picha akiwa na Polisi ninayo Nyingine
Hivi sasa ameshafikishwa Polisi,Picha nazipandisha Muda huuu hapa.
Ni aibu ya kutupwa CHADEMA Baada ya Kushindwa kwa Kila Mbinu wameamua Kuingiza Fuko la Fedha Kalenga kuhonga Wapiga kura,Kununua Shahada za Kupigia Kura.
Mbaya zaidi wameingiza Genge la Wauaji na Wamwagiaji Tindikali kama Walivyomfanya Dreva wa Mwigulu
Cd yako ya neno uharo imeshazoeleka tafuta neno lingine