Roho inaniuma sana, mabati niliyoezekea nyumba yangu yamepauka sana

Sawa mkuu au kwa mama wahenga nako nasikia ipo
Sina uhakika na uaminifu wake,maana pana watu wao uangalia pesa ya leo na sio kujenga uaminifu.Kwann.Kwa dar bora uende kiwandani Alaf unapeleka vipimo vyake wanakukatia kulingana na vipimo vya mchoro wa nyumba yako hii inaepusha mambo ya kukata hovyo bati
 
Sawa mkuu nitakutafuta nikihitaji

Chief pole sana hiyo kampuni ya Sunshire nilinunua hapo Bati 2021 January lkn leo bati hazifahi hiyo ni kampuni ya hovyo sana
IMG_1622.jpg
 
Mkuu bati ambazo hazipauki hazijawahi kuwepo relax usiishii kwa mashindano na kujifananisha kila kitu, iliyopauka ni rangi siyo bati ..

Rangi za bati zako kupauka kusipoteze Furaha ya Nyumba yako. Tusiumie kwa tulivyopoteza na kusahau tulivyobaki navyoo.
Kuna bati za migongo mipana zimeezekwa madarasa pale same secondary lile darasa limejengwa mwaka 1970 uko hadi leo bado kama limepigwa jana...haya mabati nadhani yanagrades zake na nna uhakika wengi hatuwezi kumudu bei kwa Mali safi...tunapenda vitu ambavyo havina ubora just bcoz zinafanana na vyenye ubora
 
Kuna bati za migongo mipana zimeezekwa madarasa pale same secondary lile darasa limejengwa mwaka 1970 uko hadi leo bado kama limepigwa jana...haya mabati nadhani yanagrades zake na nna uhakika wengi hatuwezi kumudu bei kwa Mali safi...tunapenda vitu ambavyo havina ubora just bcoz zinafanana na vyenye ubora
Sio kila kitu chenye bei kubwa ni kizuri au kila kitu chenye bei ndogo ni hafifu.
Kuna watu wametumia Alaf Original kutoka kiwandani bati zimepauka.
 
Sio kila kitu chenye bei kubwa ni kizuri au kila kitu chenye bei ndogo ni hafifu.
Kuna watu wametumia Alaf Original kutoka kiwandani bati zimepauka.
Kwahyo unaona alaf pekee ndio bati bora?watu wanaagiza mabati nje na vifaa vingine ya ujenzi .ni pesa yako tu
 
Yaani nimefanikiwa kujenga nyumba tena kubwa ila sijahamia bado vitu vichache nihamie, lakini kinachoniuma kipindi napaua (kupiga bati)niliaminishwa kuwa bati za kampuni fulani (hapa siitaji jina) ni nzuri na nikaonyeshwa nyumba ya jirani yenye hizo bati kuwa hazipauki.

Nilikubali baada ya kukagua na nikajiridhisha kila kitu, nikaenda nunua hizo bati pale Tazara nikapaua nyumba vizuri tu, sasa ni miaka 4 tangu nipaue sijahamia lakini zile bati kwa kweli zinatia kinyaa zimepauka hadi sina hamu ya kuhamia tena huko.

Hapa kinachoniuma zaidi nyumba ya jirani zake rangi iko vile vile na ni yeye aliniagizia alikonunua hadi bei ni hiyo hiyo, na hata jirani na ofisini kuna bati kama hizo hizo zimezungushiwa kama fensi sehemu wanakojenga hazijapauka kila siku naona ni mpya na nashindwa elewa hapa kuna siri gani kwenye hiyo kampuni nyingine zipauke nyingine zisipauke!

Hapa nawaza je! Ninunue bati zingine au ninunue rangi ya bati nikapake upya kwa mkono?

Ushauri wenu naombeni.
Umepigwa maturu
 
Kuna siku nilinunua Bati- baada yakufika site Fundi alipokuja alinipigia Simu kuwa zile bati sio za ALAF ni fake. Bahati nna Jamaa angu anafanya kazi ALAF nilipompigia akanielekeza namna ya kutambuwa ALAF original na Fake!

Niliporudi Dukani Mmoja ya alieniuzia (walikuwa wawili) akaanza maneno ya shombo. Mimi nikawaambia wanibadilishie zile Bati wanipe Original au wanipe pesa yangu! Vinginevyo Kesi nawausisha ALAF Ili wawasaidie kuwaonyesha Walipozipata hizo fake ALAF mwenzake aliposikia hivyo akanipa tena Bati 50 zingine.

Akalipia usafiri wa kupeleka original Bati site na kusomba zile fake kurudisha dukani. Ni Zaidi ya Mwaka Bati zote zipo na same color.Pole sana ila kama una risiti ya Hizo Bati washirikishe ALAF mwende Dukani mkakomae nao
Hivi ni kitu gani huwa kinawafanya watu wawe wavivu kwenda Kiwandani ukapewa mzigo wako wenye kueleweka! Unapenda buguruni/tazara unategemea kupata bati original kweli? Pale ni full fake.
 
Yaani nimefanikiwa kujenga nyumba tena kubwa ila sijahamia bado vitu vichache nihamie, lakini kinachoniuma kipindi napaua (kupiga bati)niliaminishwa kuwa bati za kampuni fulani (hapa siitaji jina) ni nzuri na nikaonyeshwa nyumba ya jirani yenye hizo bati kuwa hazipauki.

Nilikubali baada ya kukagua na nikajiridhisha kila kitu, nikaenda nunua hizo bati pale Tazara nikapaua nyumba vizuri tu, sasa ni miaka 4 tangu nipaue sijahamia lakini zile bati kwa kweli zinatia kinyaa zimepauka hadi sina hamu ya kuhamia tena huko.

Hapa kinachoniuma zaidi nyumba ya jirani zake rangi iko vile vile na ni yeye aliniagizia alikonunua hadi bei ni hiyo hiyo, na hata jirani na ofisini kuna bati kama hizo hizo zimezungushiwa kama fensi sehemu wanakojenga hazijapauka kila siku naona ni mpya na nashindwa elewa hapa kuna siri gani kwenye hiyo kampuni nyingine zipauke nyingine zisipauke!

Hapa nawaza je! Ninunue bati zingine au ninunue rangi ya bati nikapake upya kwa mkono?

Ushauri wenu naombeni.
Mkuu kupaka rangi upya utaongeza stres hazishiki rangi
 
Zinakuwa zimeandikwa ALAF hapo
Unaiona kwa nyuma na kwa mbele
Halafu zinakuwa na code nyuma ya bati sema sikupiga picha nilivyonunua
Ila kiuhakika zaidi bora ukachukue kiwandani au store kubwa ambayo haiuzi vitu fakeView attachment 2324970View attachment 2324971
Hii ndio bati ya ALAF original....alama zake katikati ya mgongo moja na mwingne kuna njia tatu namaaisha migongo midogo mitatu.....hakuna kampuni yeyote ipo hvyo...kingine muhuri wa moto nyuma ya bati kingine muhuri wa kugonga ambao umeandikwa ALAF
 
Relax bro hiyo ipo kwa wote
Niliezeka bati upande umepauka na upande mwingine zipo vile vile,nyumba ipo kama ina aina 2 za bati,ila nilinunua sehemu moja,duka moja bei moja...ila ukiangalia kwa jirani bati zipo poa tu
Ilimradi sinyeshewi haina shida
Na wewe.walikuchanhanyia na feki
 
Mimi nilienda kiwandani pale ALAF....nilipo fika wakanishauri kuwa kiwandani tunapokea oda then ndio wanatengenea kwa mteja....pia mpaka kuja kupata zitachelewa pia bei ya kiwandani pale ALAF ni kubwa kuliko kwa mawakala wao....wakaniambia ukitaka kusubir subir lipia oda lakini kama unataka nenda kwa mawakala wetu....wakanitajia mawakala wao...na namba zao za simu....pia wakanipa namna ya kutambua bati ya ALAF....na wakaniambia kama ikipauka njoo kiwandani utoe taarifa....
Nikauliza kwanini bei ya kiwandani ni kubwa kuliko kwa wakala wenu...wakanijibu kuwa wakala wanampa punguzo la 10% ya kila bati kama bati kiwandani sh 39900 bhas wakala ananunua kwa 39900-10%=35910....kwa hyo wakala ndio anajipangia bei yake wengine watauza 38000 na 37500....hyo ndio taarifa....kwa hyo kwa bati ya Alaf bora ununue kwa wakala utapata bei rahisi....nenda kwa wakala ambaye ni legit(halali)..au nenda kiwandani kuchukua namba tu na kupata elimu ya utambuzi
 
Back
Top Bottom