Riwaya: Mji tulivu ulionipa gonjwa la milele

Siku hizi watu hawasomi hivyo wana miss mambo mengi ya kufikirika........
wanataka kusomewa.......badala ya kupakata wanataka kupakatwa......
 
na nyie mnakuwaga na maneno matamu yaani mnasema nakupenda nyingi mtu mpaka anachanganyika kiasi ambacho ukikooa tu yeye anakusaidia kutema

Umenichekesha sana..
mzaramo wa vigwaza au..lete mambo basi...
 
Aagh..!

Ina maana hapo ndio mwisho au..?
kwani ukimaliza hicho kitabu kitakosa wateja au,?
 
SIMULIZI MARIDHAWA: MJI TULIVU ulionipa gonjwa la milele.

SEHEMU YA KUMI NA SABA.

ILIPOISHIA 16

Hatimaye Joshua ameweza kuonana tena na mama yake mzazi, ametoa kiasi cha dola za kimarekani ambacho ni sawa na milioni mia moja sabini za kitanzania. Sasa amerejea jijini Dar es salaam.
Anaingia katika nyumba yake ambapo alimuacha Nyambura na Mariam Sumra.
Anakutana na kisa kipya!
Mariam amejibwaka sakafuni kidevu chake kikiutawanya uso wake mezani!!

ENDELEA.

NUKUU
MKE/MUME ni kitu kingine. Awali unapoingia katika mahusiano ya kimapenzi mwenzi wako anakuwa kama mtu wa ziada kwako ambaye hata akikumbwa na jambo inakuwa mbali na wewe, baada ya muda mnaanza kufanana mitazamo, na hapo unajihisi huwezi kufanya lolote la maana bila yeye… unaamua kuingia katika ndoa. Damu zinakutana na mnakuwa mwili mmoja.
Mwenza wako anageuka kuwa ndugu yako wa karibu zaidi wa kila siku……
Ukifika wakati huu, waweza kufanya lolote kwa ajili yake.
Umewahi kusikia watu wanakuwa vichaa kwa sababu ya mapenzi? Umewahi kusikia wanaojinyonga kwa sababu ya mapenzi?
Haya yote hutokea wakati mwili wako umeungana na wa mwenza wako!
HII NI SEHEMU YA KUMI NA SABA….

Nilikimbia huku na kule kutafuta muafaka wa jambo nisilolijua kabisa. Nilishika simu nikaicha, mama naye alikuwa amechanganyikiwa akiulizia ni wapi Nyambura atakuwa ameenda. Sikuwa na jibu la kumpatia….
Kwa sababu yeye mwenyewe alifahamu fika kuwa tulikuwa wote Morogoro na sasa tupo jijini Dar es salaam.
Nilifahamu fika kuwa mimi nikionyesha kuchanganyikia na mama naye aonyeshe kuchanganyikiwa basi patakuwa hapakaliki pale ndani, nikatulia na kuchukua tena simu yangu nikajisahaulisha kama kuna lolote ambalo limetokea.
Sasa niliweza kupata mtu wa kumpigia.
Mume wa Mariam Sumra ambaye ni mwanasheria wangu!
Simu ilipokelewa upesi sana.
“Nilitaka kukupigia simu muda huu huu!” alianza kuzungumza bila salamu yoyote. Nikamsikiliza.
“Simpati Nyambura hewani, sijui kama upon aye?”
“Nyambura? Wa nini?” nikamrushia swali.
“Upon aye?” aliendelea kuuliza badala ya kujibu.
“Hapana! Kuna tatizo lolote?” nikarusha tena swali.
Hapohapo bila kutarajia chochote, ghafla mama akanipokonya ile simu.
“Mje mtusaidie tumekuta mtu ni mwanamke ndani ya nyumba yetu, hatujui kama amekufa ama ni mzima. Na mke wa mwanangu hayupo, nje mtusaidie jamaniii!” alizungumza upesi upesi mama akiwa amechanganyikiwa sana.
Ni tukio ambalo sikulitarajia kabisa na lilizua mshikemshike.
Alipomaliza akanipatia simu huku akinilaumu kuwa ninazunguka zunguka mbuyu badala niseme shida inayotukabili.
Sikumlaumu mama!
Niliporejea kumsikiliza mwanasheria alinisihi nimweleze ukweli nini kinatoke.
Nikamweleza hali kwa ufupi kama ilivyokuwa inaonekana machoni pangu. Lakini sikumgusia juu ya safari yangu ya Morogoro!
Akasema anakuja pale nyumbani.
Sisi tulibaki mbali kabisa na mwili wa Mariam Sumra, mama alikuwa ananionya kabisa nisiusogelee mpaka polisi wafike.
Yeye alijua niliyekuwa nazungumza naye anahusika na mambo ya kipolisi.

Baada tya dakika kumi na tano na ushee, pikipiki ilisimama mbele ya nyumba yangu. Geti lilikuwa wazi nikasikia vishindo vya mtu akija mbiombio.
Nikaufungua mlango na kumtazama kwa mbali mwanasheria wangu akitimua mbio.
Ama! Mapenzi ni kitu cha ajabu sana.
Usiombe yakakumeza na kukutupa katika mji unaoamini ni tulivu kupita yote.
Hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona mwanasheria huyu akiwa na hofu kubwa kiasi hiki.
Alipofika akanisalimia mimi ‘SHKAMOO’ kisha akamwambia mama yangu ‘HABARI ZA KAZI’
Nilijikuta nachekea mbavuni, baada ya muda mrefu kupita nikiwa sina hata tabasamu.
“Amekuwaje mke wangu eeh! Amekuwaje jamani?” alihoji.
“Kama nilivyokueleza katika simu mkuu. Hakuna ajuaye.. wote tumeingia muda huu.”
“Hata mama nawe haukuwepo?” alimtupia swali mama.
Mama hakujibu!
Mwenye mke akamsogelea mkewe.
Akamgusa hapa na pale….
“Anapumua!!” alisema….
“Nini kimemtokea jamani eeh!” sasa alikitoa kichwa pale mezani na kumnyoosha sakafuni.
Sasa hata mimi niliweza kuona akiwa anapumua.
Hapakuwa na muda wa kupoteza zaidi, tukakubaliana kumpeleka hospitali.
Nilijikaza na kuendesha gari kwa sababu mwanasheria alikuwa amepagawa zaidi.
Tukiwa katika gari alikuwa akirudia rudia maneno ambayo awali niliyachukulia kuwa ya kawaida sana lakini alipozidi kuyarudia nikaanza kupatwa na hasira.
Alikuwa akisema, ‘Joshua unajua mkeo ni shetani eeh! Shetani kabisa huyu mwanamke, sijui hata ulikosea nini ukaoa shetani.’
Anatulia kidogo ananikumbusha tena kuwa mke wangu ni shetani.
Hasira zikanikaba, lakini nikapambana nisije kufanya jambo lolote la kishenzi.
Hii hali ya kukasirika baada ya mke wangu kuitwa shetani ilinifanya nitambue kuwa licha ya haya yote yaliyotokea, alama za penzi zito la Nyambura zilikuwa katika sehemu kubwa tu ya moyo wangu licha ya hayo yote yaliyotokea.
Unaweza kunishangaa sana na kusema kuwa laiti kama ingelikuwa ni wewe usingelichukia kabisa.
Ni kweli kwa sababu si wewe uliyeshuhudia penzi zito na la dhati kabla ya mkasa huu!!
Tulifika hospitali, tukasaidia kumshusha Mariam Sumra!
Akapokelewa na wauguzi akaingizwa wodini.
Baada ya kutoa maelekezo na sisi kupewa maelekezo sasa tulibaki nje kusubiri kitakachojiri.
Mwanasheria akaanza tena kusema vibaya juu ya Nyambura.
Nikaona huyu bila kumwonyesha makucha sekunde si nyingi atanivuruga upya akili yangu.
“Brother! Achana na masuala ya Nyambura na ushetani wake, unapomzungumzia Nyambura kama shetani unamzungumzia mke wangu wa ndoa, mama wa mtoto wangu mmoja. Unaposema ni shetani ni kipi mkeo alifuata kwa Nyambura kama sio shetani kumfuata shetani mwenzake? Wote ni mashetani tu, shetani mmoja yupo wodini amepoteza fahamu, shetani mwenzake anazurura popote anapojua yeye. Acha kumsema Nyambura hivyo tafadhali….” Niliwaka!!
“Joshua acha baba…. Yaishe tupo matatizoni, na wewe baba mwingine acha kusema ushetani wa mtu usiyemjua…. Hivi mnajua Nyambura mnayemuita shetani alinitolea damu nyingi sana alipokuja kuniuguza kijijini, bila yeye ningeweza kufa. Hakutaka sifa zozote hajatangazia mtu… hebu mtunzie na haya mazuri yake basi…. Hata kama ni shetani basi tuyatunze katika mioyo yetu.” Mama alitusuluhisha.
Yakaishia pale.
Lakini sikutaka tena kuwa jirani na mwanasheria nikaketi mbali kiasi.
Nusu saa baadaye majibu yalitoka kuwa Mariam Sumra alilishwa madawa ya kuleta usingizi, hakuwa na tatizo lolote zaidi ya pale.
Huduma zikaendelea kutolewa hadi mjajira ya saa kumi jioni tukaondoka pale.
Niliendesha gari hadi nyumbani kwa mwanasheria, wakati huo maelezo ya Mariam Sumra hayakufaa kitu chochote.
Kwa sababu alidai kuwa Nyambura hakumweleza mpango wowote aliokuwanao.
Tulipowashusha, mwanasheria alinifikia na kunipigapiga begani kisha akajutia kauli zake.
Nikamwambia yamekwisha kabisa.
Tukaondoka na mama hadi nyumbani, tukiwa kimya kabisa katika gari.

Tulifika na kuikuta nyumba ipo kama vile tulivyoiacha. Hii ilimaanisha kuwa Nyambura hakuwa amerejea.
Niliufungua mlango na kuingia pale ndani….
Mara mama akapiga mayowe, nikaruka mbele kukwepa hatari yoyote ambayo ingejitokeza.
Nikageuka na kumtazama mama alikuwa anatazama chini…..
Damu!!
Palikuwa na alama za damu ambazo hazikuwepo hapo kabla.
Kutazama vizuri ulikuwa ni mchirizi wa damu…..
Sijui pale tulipouona ndo ulikuwa unaanzia ama ulikuwa unaishia…
Mchorizi ule ulikuwa unatokea chumbani ama kuelekea huko.
Mapigo ya moyo yakaanza kufukuzana tena……
Nini hiki?
Tulijiuliza, nikatimua mbio mpaka chumbani bila uoga wowote ule.
Matatizo yalikuwa lukuki sana sasa sikuwa naogopa lolote lile.
Niliingia na kuufuata mchirizi ule.
Nikainama uvunguni, mama naye akinifuata nyuma hapakuwa na mauaji wala hapakuwa na mtu yeyote yule.
Tulibaki kustaajabu.
“Bahasha hiyo ina damu..” mama aliona na kusema, nikageuka na kutazama upande alionionyesha.
Kweli kulikuwa na bahasha yenye damu.
“Mama wamemuua Agy wangu!!” nilianza kulia sasa.
“Agy! Umejuaje?” alinibambika swali lililokatisha kilio changu, kwa sababu nilikuwa nalilia kitu nisichokijua.
Nikaiokota ile bahasha huku nikitetemeka.
Nikaifungua na kukuta ndani kuna kipande cha barua.
Nikatoa huku nikiomba Mungu pasije kuwa na masharti ya kipesa kwa ajili ya kumkomboa mwanangu.
Sikuwa na pesa kabisa, hivyo mwanangu angeweza kuuwawa.
Safari hii sikuwaza sana juu ya Nyambura!
Kutazama ulikuwa ni mwandiko wa Nyambura, mwandiko niliouzoea pindi tulipokuwa ofisini.
Nikaisoma kwa sauti mama awe shuhuda kwa kusikia.

NYANBURA ANAANDIKA!!
Joshua, mume kipenzi kabisa.
Ndugu yangu pekee, na baba halali wa mtoto wetu!
Niligundua kuwa nakupenda sana lakini nilikuwa nimechelewa, tayari nilikuwa nimeharibu kwa kutunza kisasi kisokuwa na tija.
Kisasi cha kipuuzi!
Umeteseika nimeona kwa macho, nami ninateseka moyoni hakuna anayeweza kuona.
Nikiulizwa peponi nini maana ya pendo la dhati nitajibu Joshua, hata wakihitaji orodha ya wanaume wa uhakika niliowahi kukutana nao jibu litakuwa Joshua.
Yaliyopita yamepita! Wewe ni baba bora sana ambaye unastahili kupata mwanamke safi asekuwa na visasi katika nafsi yake.
Lakini ni mwanaume ambaye haustahili kutendewa haya yaliyotokea kwako.
Nimeona na kwa dakika za mwisho nimejaribu walau kupigania kidogo kilicho chako walichotaka kukupokonya,
Ulipishana nami katika hoteli Morogoro.
Usingeweza kunijua, nilikutazama na kuuona uso wako ulivyosononeka kwa haya yaliyotokea, niliona jinsi ulivyokonda kwa mawazo.
Nilimuona mama yetu alivyokuwa anakusikitikia.
Niliingia ulipokuwa na niliua!
Ndio niliua….
Kuhusu niliuaje na niliua wangapi? Haya hayana tija lakini kwa sababu walikiuka makubaliano yetu niliona hawa ndo wanafaa kuadhibu na sio wewe Joshua.
Mimi ni binti imara kabisa kutoka mkoani Mara, nimepitia suluba zote na pale mtu anapokiuka tulichokubaliana nipo radhi hata kuua.
Narudia tena niliua na nimeirejesha bahasha iole kwako. Sikutoa hata noti moja.
Halali yangu ipo katika akaunti yangu, ulinilipa mshahara mzuri sana unanitosha kuanza maisha mapya nikiwa namlea mtoto wako.
Kama nisipokamatwa mapema basi mwanao akifikisha miaka minne, nitamleta kwako.
Lakini kama ukisikia nimekamatwa mapema tafadhali usiache Agness akatua katika mikono ya watu wabaya.
Mchukue wewe uliyesota kumpata!
Mchirizi huo wa damu usikushangaze sana…
Nimejikata maksudi na kuiacha damu hii iishi nawe katika nyumba yako milele yote.
Nawapenda sana!
Nakusihi sana usiyafuatilie tena mambo haya kwa namna yoyote kwa sababu yatakuumiza kichwa.
Naomba msamaha mimi kwa niaba ya wote nilioshirikiana nao.
FUNUA GODORO MUDA HUU!!

Nyambura Joshua!!

Barua iliishia pale, nami upesi nikafunua godoro.
Macho yangu yakakutana na ile bahasha niliyoipeleka Morogoro.
Nilijikuta natokwa na kilio huku moyo wangu ukiuma sana, nilitamani Nyambura angerejea tena katika maisha yangu!!
Lakini Nyambura hakujulikana ni wapi alipo…..

_____

Baada ya muda nikaendelea na shughuli zangu katika kampuni yangu ambayo ilikuwa imeacha kufanya kazi kwa sababu wafanyakazi hawajalipwa mishahara yao.
Siku niliyoingia ofisini kwangu, nilijikuta natabasamu tu, nilikuwa nimewakumbuka wale matapeli waliodai kuagizwa na mizimu….
Nikatambua kuwa hata wao huko walipo kuzimu watakuwa wakikumbuka wananicheka sana.
Nikatulia katika kiti changu cha kuzunguka, nikaanza kuandika majina na madhara katika akili yangu.

NYAMBURA: Sitakaa niwaamini wanawake katika maisha yangu hasaha katika sekta ya mapenzi, sikuwaza kuoa tena. Mpaka hivi sasa sitaki ushauri!!

REVO: akili yangu haikuwa na nafasi tena kwa ajili ya rafiki wa dhati, hata mwanasheria aliyenisaidia bado sikutaka kumwamini sana. Ikiwa naye alimuita mke wangu shetani, ipo siku nami anaweza kuniita baradhuli.

MGANGA: Sitathubutu kwenda kwa waganga wa jadi tena, ni waongo na wanafiki wakubwa.

Majina haya yalinitosha sana kwa wakati ule.
Na niliapa kuwa hata wanasaikolojia wahamie nyumbani kwangu na wengine waje kuishi ofisini kwangu hawataweza kulitibu gonjwa langu la kihisia juu ya marafiki na mapenzi.
“Ama hakika Nyambura ulikuwa ni mji tulivu, mji bora kabisa niliowahi kuishi lakini gonjwa uliloniachia ni la milele nitadumu nalo….”

JIFUNZE:

KATIKA maisha kuna nyakati huja katika maisha ya watu wengine, nawe utaziona na kuishia kusema yamemtokea fulani. Lakini halahala litokealo kwa jirani yako hata nawe laweza kukutokea. Majaribu shida na mateso tumeumbiwa wanadamu!!!
Jifunze kupitia uyaonayo ili ujiandae kuyakabili yakija kwako…..

MWISHOO!!



 

Similar Discussions

Back
Top Bottom