mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,136
- 275
- Thread starter
- #301
SIMULIZI: BALAA.
MWANDISHI: HALFANI SUDY
SIMU: 0757 633010
SEHEMU YA MIA NA TANO
Katika akili ya Dokta Kilumba alikuwa anajua yule mwanamke aliyeongea na kule baa, Alice baamedi, mwanamke aliyekubaliana nae kule katika baa ya Masoko by night ndiye alikuwa anagonga mlango muda ule. Dokta Kilumba aliusogelea ule mlango bila wasiwasi wowote. Akiwa amejifunga taulo jeupe safi kiunoni, huku juu akiwa kifua wazi.
Dokta Kilumba alipofungua tu mlango alikutana na Balaa! Alikutana na dhoruba kali sana. Alijikuta amesukumwa kwa nguvu na kifua cha kiume cha Dokta Yusha, msukumo ambao ulimrudisha ndani kwa kasi na kumdondosha chini moja kwa moja. Dokta Kilumba hakujiandaa kabisa na tukio lile, alitegemea kukutana na kukumbatiwa na kifua laini cha mrembo Alice, lakini kwa bahati mbaya kabisa alikutana na kitu tofauti, alikutana na kifua kigumu cha kiume, kifua cha Dokta Yusha.
Baada ya anguko lililotokana na msukumo wa kifua cha dokta Yusha. Kwa mwendo wa taratibu dokta Yusha alimfata Dokta Kilumba pale chini. Wakati Dokta Yusha akimfata Dokta Kilumba pale chini, Mwanasheria mlevi alibaki pale mlangoni, alikuwa anafunga mlango wa chumba kile cha kulala wageni kwa ndani. Mambo yote hayo yalifanyika kwa muda mfupi sana, na kwa umakini mkubwa pia.
Dokta Kilumba alibaki ametumbua macho pale chini, sakafuni. Kichwani mwake yalikuwa yanapita maswali mengi sana, bila ya kuwa na majibu. Ingawa Dokta Kilumba alikuwa anawafahamu vizuri watu wale wawili lakini Dokta Kilumba hakujua kabisa watu wale wametokea wapi baada ya kutoweka kwa mm muda mrefu, na wamekijua vipi chumba chake. Dokta Kilumba hakupata muda wa kutafakari zaidi, Kofi la nguvu la mkono wa kulia toka kwa Dokta Yusha lilitua katikati ya uso wa Dokta Kilumba. Dokta Kilumba aliona vimulimuli. Kilikuwa kitendo cha ghafla sana na Dokta Kilumba hakutegemea kabisa kufanyiwa vile na Dokta Yusha....
Dokta Kilumba kikaangoni...atatoka salama?
ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA
MWANDISHI: HALFANI SUDY
SIMU: 0757 633010
SEHEMU YA MIA NA TANO
Katika akili ya Dokta Kilumba alikuwa anajua yule mwanamke aliyeongea na kule baa, Alice baamedi, mwanamke aliyekubaliana nae kule katika baa ya Masoko by night ndiye alikuwa anagonga mlango muda ule. Dokta Kilumba aliusogelea ule mlango bila wasiwasi wowote. Akiwa amejifunga taulo jeupe safi kiunoni, huku juu akiwa kifua wazi.
Dokta Kilumba alipofungua tu mlango alikutana na Balaa! Alikutana na dhoruba kali sana. Alijikuta amesukumwa kwa nguvu na kifua cha kiume cha Dokta Yusha, msukumo ambao ulimrudisha ndani kwa kasi na kumdondosha chini moja kwa moja. Dokta Kilumba hakujiandaa kabisa na tukio lile, alitegemea kukutana na kukumbatiwa na kifua laini cha mrembo Alice, lakini kwa bahati mbaya kabisa alikutana na kitu tofauti, alikutana na kifua kigumu cha kiume, kifua cha Dokta Yusha.
Baada ya anguko lililotokana na msukumo wa kifua cha dokta Yusha. Kwa mwendo wa taratibu dokta Yusha alimfata Dokta Kilumba pale chini. Wakati Dokta Yusha akimfata Dokta Kilumba pale chini, Mwanasheria mlevi alibaki pale mlangoni, alikuwa anafunga mlango wa chumba kile cha kulala wageni kwa ndani. Mambo yote hayo yalifanyika kwa muda mfupi sana, na kwa umakini mkubwa pia.
Dokta Kilumba alibaki ametumbua macho pale chini, sakafuni. Kichwani mwake yalikuwa yanapita maswali mengi sana, bila ya kuwa na majibu. Ingawa Dokta Kilumba alikuwa anawafahamu vizuri watu wale wawili lakini Dokta Kilumba hakujua kabisa watu wale wametokea wapi baada ya kutoweka kwa mm muda mrefu, na wamekijua vipi chumba chake. Dokta Kilumba hakupata muda wa kutafakari zaidi, Kofi la nguvu la mkono wa kulia toka kwa Dokta Yusha lilitua katikati ya uso wa Dokta Kilumba. Dokta Kilumba aliona vimulimuli. Kilikuwa kitendo cha ghafla sana na Dokta Kilumba hakutegemea kabisa kufanyiwa vile na Dokta Yusha....
Dokta Kilumba kikaangoni...atatoka salama?
ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA