Ripoti ya PAC kuhusu Escrow Kusomwa Jioni Bungeni

Kwahiyo badala yake asubuhi ya leo kitafanyika kitu gani na haya maswali yanayoendelea yalikuwepo toka mwanzo ama yameingizwa ili kumisuse mda wa ripoti ya PAP?
 
Mahakama ilishindwa kuzuia BMK lisiendelee sababu ya Maoni ya Wananchi kupuuzwa,sintoshangaa Mahakama hii leo ikizuia ripoti ya PAC isisomwe Bungeni,BACK TANGANYIKA.
 
Escrow ni kokoro.

Jamani JF huwa haina longolongo. Kuna mtu aliandika humu kwamba Marando na Myele wameenda kuping mahakamani Report ya Escrow isisomwe, watu wakapinga na kukanusha. Sasa hati ya mahakama inaonyesha Mnyele ambay ni partner wa Marando katika kampuni ya uwakili ya Marando & Mnyele Advocates ndiye wakili kinara katika shauri hili akiiwakilisha PAP/IPTL.

Mnyele atakuwa anatumiwa na mzee Pinda ni mfipa mwenzake tena ni shushushu wa kutupwa ana nifahamu na nina mfahamu huyu mnyele alimuua mkewe kwa kipigo hata hakufungwa
 
Pinda lazima aondoke na serikali yao dhaifu..

Ivi Prof Jik yuko wapi awasafishe watu wake?
 
Kitendo cha kuahirisha mpaka jioni ni hatari.TBC taifa wanasema itawasilishwa muda mfupi ujao hivyo tusiondoke!!!
Tuendelee kusikiliza taarifa
 
Kwani zile busara za majaji tunazoambiwa wanazitumia kwenye issues nyeti zimeenda wapi??????????? au mgawo umewafumba macho na wao?????????????????? Hovyo, hakuna chombo kinachoamini ka nchi hii
 
Jamani kama hao mawaziri na wabunge na wote waliohusika na hii kesi hawakuchota hizo hela kwanini kuwe na malumbano yote hayo??? Na wazuie hiyo report isisomwe bungune. Dhahiri kabisa inaonyesha kua wamezichota. Infact ni mengi tu yaliochotwa ambayo ni mali ya umma mbali ya hii ESCROW. sasa kwa wale wenye akili zao timamu na wenye chungu na mali zao hata kama hataki vyama vya upinzani ni bora wakae manyumbani kwao badala ya kuwapa kura zao kwa CCM. Au iwe kura hewa. Hii nikashfa na aibu kubwa sana kwa nchi.
 
kwa mujibu wa maelezo ya mwanasheria wa standard Advocates leo asubuhi kwenye redio uhuru FM mahakama hawako sahihi wameliingilia bunge.hivyo bunge lipo sahihi.
Yani kuanzia sasa ni utawala wa majambazi kwa raha zao; mtu ataenda kule Loliondo atauawa wamasai wote kisha akimbilie mahakamani kuzuia bunge lisiunde kamati ya kuchunguza. Sasa kuna haja gani tena kuwa na bunge? si mahakama zinatosha? hata raisi atazuiwa kumuondoa waziri madarakani yani ni shiiiiiida; mimi sijapata kuona mtoto akamuoa mama yake. Bunge linatunga sheria ili mahakama zitumie leo mahakama zinasimama kuliambia bunge msitunge sheria hii na hii yani serikali ikishawekwa mfukoni ni majanja. Stahili ya majambazi haya ingekuwa muda huu yako ndani kwa uhujumu uchumi na sio mahakamani kupeleka maombi ya kufukuza bunge kazi.
 
si mahakama ipo pale. Tanesco nayo ipo pale na bunge lipo Dom . sasa ni wakati wa wanchi kuondoa fikra za uwoga liwe na liwe tufanye kama ya Bokinafaso
 
Back
Top Bottom