Revealed: Jumuia ya Madaktari waliotharika na mgomo ndio hii

Jackbauer

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
6,038
2,199
najaribu kuwaletea kipande kwa kipande juu ya wanaojiita jumuiya ya madaktari walioathiriwa na mgomo ambao jana walisikika wakiomba msamaha.hii ni kwa mujibu wa vyanzo vya social media za madaktari.
This is a highly classified information

Dr. Sakala akiwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo cha BUGANDO alifikia hatua kukigeuza Chuo kama Tawi la CCM kwa kuwashawishi wanafunzi wenzake kujiunga na CCM pamoja na kusambaza kadi, Dr. Nuru Mwambola, ambaye amejibadilisha jina na kujiita Nuru light alituhumiwa kuhujumu wenzake akiwa Makamu wa Rais pale Kairuki mpaka kufikia kupigiwa kura ya kutokuwa imani nae, Ni Nuru ambaye amekuwa Mwanachama mtiifu kwa CCM alikuwa akitumika kushawishi wanafunzi wenzake kujiunga na CCM.

Ni kwa kutumia nafasi hiyo, walikwenda kwa mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kinondoni Wakili Makene tar 21.08.2012 na kumuomba awakutanishe na Stephen Wassira ili waweze kuonana na Rais. Wakili Makene aliwajibu kuwa Wassira yupo nje ya Dar ila ametoa maelekezo kuwa Rais yupo tayari kuwaona ila waombe msamaha kwanza kwa rais, serikali na wananchi.

Baada ya agizo hilo ndipo wakaendelea na mchakato wa kukusanya majina ya interns, na kwa taarifa zilizopo ni kwamba ni inters 150 tu kati ya 319 ndio waliotuma majina yao. Baada ya kutekeleza agizo la kuomba msamaha hapo jana, baadhi ya wajumbe wa kamati ya Madaktari wa CCM walikwenda wizarani ili kupata mrejesho, na Naibu Waziri aliwajibu kuwa Mwizi akikiri ameiba kinachofuata ni hukumu. Huko ndiko shinikizo la Msamaha lilikoanzia.
check na hii hapa chini

WAKATI WA MGOMO WA MADAKTARI "DR PAUL SWAKALA" alizungumza maneno haya…

'Nasikitika kuona kwa jinsi gani ambavyo tunataka kukata tamaa, ambacho nataka kusema ni kitu kimoja, moja kati ya kada ambazo unasoma course unit nyingi kuliko kada yoyote ni udaktari, nasikitika kuona kwamba tunataka kuwa desperate na kuamini kwamba bila kutibu, bila kukutana na mgonjwa, bila kuajiriwa na serikali, there is no life, hiyo sio kweli kabisa, kama mlango mmoja utafungwa ninaamini kuna mlango mwingine utafunguliwa, nina uhakika kwa mtu ambaye amesoma degree iliyokamilika huwezi kukosa kibarua cha kukuweka mjini, nab ado maisha yataendelea kuwepo, na bado unaweza ukaishi vizuri hata kuliko utakapoingia kwenye kada hii ya kutibu…..huyu ni daktari Intern alokuwa akiwakilisha Mwananyamala kwenye mikutano ya …MAT'''

…Leo hii anazungumza hivi tena:
"Tunatumia fursa hii kupitia kwenu waandishi wa habari kuwaomba radhi watanzania wote na kwa serikali kutokana na madhara yaliyosababishwa na migomo ile ambayo ushiriki wetu ulikuwa hauepukiki.Tunajua wapo watu walioathirika na mgomo ule,hivyo tunaomba radhi watanzania wote walioathirika na mgomo,pia kwa usumbufu uliojitokeza…"

(MTANZANIA JUMANNE, SEPTEMBER 18,2012)

angalia sms ya bwana huyu(Dr sakwala) alivyokua jasiri .....
"Damu yangu iliyomwagika na iwe chachu ya kutuimarisha na kuendelea kudai maslahi ya madaktari" Maneno ya Dr Ulimboka wakati mamia wakimuaga akielekea nje ya nchi. Mimi( yaani yeye Dr. Sakala) hata kama nitabaki peke yangu sitamsaliti na kurudi nyuma, wewe je?

Ni Sakala huyu aliyekuwa akibandika matangazo na kutuma sms za kuhamasisha wenzake wa Mwananyamala, leo anadai ameshawishiwa? Yani unagoma mara 3 kwa miezi 7 unasema umeshinikizwa?

pia kuna hili linakuja...
Stay tuned, ntaendelea kutiririka mpaka donge aliloahidiwa
 
Tatizo la Wasomi wengi wa Nchi hii ni waoga na wanafiki wakubwa...kisikia kunguru anakimbia nae anakimbia kuelekea asikokujua...Madaktari walisema huduma za afya ni mbovu hilo halina shaka wala huhitaji kuwa na PHD kulijua hilo...sasa ghafla hao hao jitu lingne linasema tunaomba msamaha tutatibu..sasa je vifaa tiba mlivyolalamikia vimeletwa?!! je wagonjwa sasa wanalalal mmoja kitandan au 4!! kama sivyo basi nyie ni wasomi njaa milikua mnacopy assignment za wenzenu mnafaulu kichwani peupeeee..ovyo kabisa,

swali la kujiuliza ni watu wangapi wanapata Tiba stahiki hapa Tz?!! wakubwa na mafisadi wao waaenda nje huduma ziko safi na bora nyie mnakalia kupiga mayowe tukasema labda mtakazia mafisadi wanunue vifaa wote tutibiwe hapa kwa uzuri kumbe nyie nao hovyo kabisaaa...yaani wanafiki kama nyie mbingu mtaisikia tu..
 
Ukijiulizzza Ulmboka yuko wapi?!! alipigwa nusra auwawe, taja sasa kilichotokea na kama kweli ile No ya simu unaijua naye kakaa kimyaa sasa hiyo akili matope..wakati huo watu walimchangia akaenda kutibiwa nje kisa hapa huduma hakuna!!!
 
CCM ikiendelea kudumu zaidi ya miaka mitatu ya kikatiba madarakani....Tanzania itakuwa historia tu kwani tumechoshwa na uzalimu wake.
Ukienda muhimbili leo dawa hakuna na wagonjwa hawahudumiwi ipasavyo na madaktari.Kama msamaha umeombwa kwa dhati ningeshangilia sana ila wale wachache wametapeliwa na wanyama wa ccm na pia si wazalendo kwani hata historia zao zina mashaka
 
Tatizo la Wasomi wengi wa Nchi hii ni waoga na wanafiki wakubwa...kisikia kunguru anakimbia nae anakimbia kuelekea asikokujua...Madaktari walisema huduma za afya ni mbovu hilo halina shaka wala huhitaji kuwa na PHD kulijua hilo...sasa ghafla hao hao jitu lingne linasema tunaomba msamaha tutatibu..sasa je vifaa tiba mlivyolalamikia vimeletwa?!! je wagonjwa sasa wanalalal mmoja kitandan au 4!! kama sivyo basi nyie ni wasomi njaa milikua mnacopy assignment za wenzenu mnafaulu kichwani peupeeee..ovyo kabisa,

swali la kujiuliza ni watu wangapi wanapata Tiba stahiki hapa Tz?!! wakubwa na mafisadi wao waaenda nje huduma ziko safi na bora nyie mnakalia kupiga mayowe tukasema labda mtakazia mafisadi wanunue vifaa wote tutibiwe hapa kwa uzuri kumbe nyie nao hovyo kabisaaa...yaani wanafiki kama nyie mbingu mtaisikia tu..

Ni uamuzi wa busara. Mnaowachachoea kugoma nyie mmekaa na vibarua vyenu na mnaendelea na maisha yenu kama kawaida. Ni nani kati ya wana JF ameshafuatilia au hata kutoa msaada kwa hawa vijana wa vijana wa interns tangu wagome na kufukuzwa vibarua. Wote ni wanafiki mnasubiri kuja kuchangia JF kuwashinikiza waendelee na msimamo wao huku nyie mnaendelea na vibarua vyenu. Tunawapongeza wameliona hili na kuchukua hatua stahiki. Nani humu ndani alishawatafuta na kuwapa hata senti kama kweli tunawajali?
 
Hao ni wa Mwanza tuwekee na wa Dar es Salaam na maeneo mengine.
Kwahiyo sasa inaonekana hata Ccm huyu bwana haijui na yeye anataka kutuambia hata waliompiga ulimboka atakua anawafahamu na alifurahishwa na hicho kitendo maana viongozi wote wa serikali na ccm ikiwa ni pamoja na wabuge wao walishangilia sana mfano mzuri ni stell manyanya mabovu na lisura lake kama mzibua vyoo alishadadia sana kupigwa dr.ulimboka....Lawama zangu kwa ulimboka maana ukimya wako na jinsi taifa lilivyopiga keelele ili haki yako yako ipatikane ikiwa ni pamoja na kuwaadabisha wahusika ambao tunajua wanatoka ikulu umetuvunja nguvu na kibaya zaidi mtakungutwa zaidi na sasa umeonesha kwamba hata kama mtanyanyaswa kiasi gani hamstahili huruma wala msaada toka kwa watz na nasikitika nilichanga zaidi ya 70,000 ili upone na kuendeleza mapambano lkn umenikatisha tamaa sana wapoti!!!!Siwaamini na siwapendi tene madr.Liwalo na liwe
 
Safi sana wanazidi kuumbuka kumbe ni ccm bhana!

Nilitaka nishangae ccm kutotoa maagizo ya kuomba msamaha.
 
Ni uamuzi wa busara. Mnaowachachoea kugoma nyie mmekaa na vibarua vyenu na mnaendelea na maisha yenu kama kawaida. Ni nani kati ya wana JF ameshafuatilia au hata kutoa msaada kwa hawa vijana wa vijana wa interns tangu wagome na kufukuzwa vibarua. Wote ni wanafiki mnasubiri kuja kuchangia JF kuwashinikiza waendelee na msimamo wao huku nyie mnaendelea na vibarua vyenu. Tunawapongeza wameliona hili na kuchukua hatua stahiki. Nani humu ndani alishawatafuta na kuwapa hata senti kama kweli tunawajali?


Uwezo wako wa kufikiri mdogo sana...uamuzi wa busara ni kugoma kama unasababu ya msingi ya kugomea kama huna gloves, huna nyembe na wagonjwa wamejaa hadi chini ww unatibu vipi hao wtu,kibarua sio kila mtu ameajiriwa, mwanaume husifiwi kwa kuajiriwa unapiga kazi sio kusubiria uletewe...ovyooo
 
Ni uamuzi wa busara. Mnaowachachoea kugoma nyie mmekaa na vibarua vyenu na mnaendelea na maisha yenu kama kawaida. Ni nani kati ya wana JF ameshafuatilia au hata kutoa msaada kwa hawa vijana wa vijana wa interns tangu wagome na kufukuzwa vibarua. Wote ni wanafiki mnasubiri kuja kuchangia
  • A%20S-devil1.gif

JF kuwashinikiza waendelee na msimamo wao huku nyie mnaendelea na vibarua vyenu. Tunawapongeza wameliona hili na kuchukua hatua stahiki. Nani humu ndani alishawatafuta na kuwapa hata senti kama kweli tunawajali?
hakuchochewa mtu bali walikaa chini na kuafikiana na mmoja wa wahamasishaji wa mgomo mwananyamala ni huyu aneyeomba msamaha leo.
au ndio tuseme alitumwa kuchochea mgomo ili baadae auzime na kutoa credit kwa watawala??
 
langei Kila kitu kina mwisho wake. Nadhani wamechambua faida na hasara ya uamuzi wao na kubaini kuwa kuomba msaada ndiyo njia mwafaka ya kuendelea na maisha. Hao kina Slaa wenyewe waliowachachoea hawajawasidia hata senti. Hata mashabiki wa migomo hapa JF hawana msaada wowote kwao. Kumbuka hawa vijana nawao wana malengo na ndoto zao. Wameamua kuweka siasa chini na kuamua kukubalina na hali halisi. Na huo ndiyo uungwana. Tunaojidai kuwalaumu tujiulize sisi binafsi tumewasaidiaje tangu wapoteze ajira zao zaidi ya kushinda tunapost hapa JF tu.
 
Last edited by a moderator:
Ni uamuzi wa busara. Mnaowachachoea kugoma nyie mmekaa na vibarua vyenu na mnaendelea na maisha yenu kama kawaida. Ni nani kati ya wana JF ameshafuatilia au hata kutoa msaada kwa hawa vijana wa vijana wa interns tangu wagome na kufukuzwa vibarua. Wote ni wanafiki mnasubiri kuja kuchangia JF kuwashinikiza waendelee na msimamo wao huku nyie mnaendelea na vibarua vyenu. Tunawapongeza wameliona hili na kuchukua hatua stahiki. Nani humu ndani alishawatafuta na kuwapa hata senti kama kweli tunawajali?

Well said mkuu!
 
Kila kitu kina mwisho wake. Nadhani wamechambua faida na hasara ya uamuzi wao na kubaini kuwa kuomba msaada ndiyo njia mwafaka ya kuendelea na maisha. Hao kina Slaa wenyewe waliowachachoea hawajawasidia hata senti. Hata mashabiki wa migomo hapa JF hawana msaada wowote kwao. Kumbuka hawa vijana nawao wana malengo na ndoto zao. Wameamua kuweka siasa chini na kuamua kukubalina na hali halisi. Na huo ndiyo uungwana. Tunaojidai kuwalaumu tujiulize sisi binafsi tumewasaidiaje tangu wapoteze ajira zao zaidi ya kushinda tunapost hapa JF tu.
Kwa hoja zako si tu naona uhafifu wa kufikiri bali hata nadhani hujawahi kufikiria maisha yako yote.
 
Back
Top Bottom