Mlengo wa Kati
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 2,730
- 492
Ndugu wana JF ni wiki ya Tatu sasa tangu wabunge wetu waingiziwe kwenye akaunti zao kiasi cha Milioni 90,nimetaja wabunge hawa vijana watuambie hivi wanajisikiaje kupata kiasi hicho wakati wakijua hali ya maisha ya Watanzania kwa sasa? Ndugu zangu hivi tuige nini hasa tunapo ona wapiganaji wetu nao wanafanya makosa yaleyale ambayo ni sawa na Wabunge wa CCM! Dr slaa hivi umehoji kwa nini wabunge wako wamekubali kuingiziwa kiasi hicho bila kuangalia maisha yetu watanzania ambao wengi kwa sasa tuna weza kupata mlo mmoja kwa siku? Milioni 90 najua imetokana na jasho la walipa kodi! Nashauri kamati kuu ya Chadema ikae iliangalie suala hili lasivyo linatutia matope na kupoteza hata ile maana ya Chadema kuwa chama cha ukombozi kwa Watanzani! Mh Mnyika,Mh Zitto na Mh Mtema najua safari yenu bado ndefu kisiasa hivi kweli mumekubali kula hii hela haramu ya maskini wa kitanzania? Mh Regia Mtema hivi kweli Aluta Kontinua kwa namna hii! Mandela aliwahi kusema makaburu hawana uwezo wa kutuhonga kwa garama yeyote ile bali kilicho na thamani ni Maisha ya Watu wetu! Mmekubali kuhongwa kwa mkate kama askari wa kihindi! My take: ni mhimu tujipime kama chama cha ukombozi wa maskini wa watanzania walio wengi!