GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,647
- 109,036
RC MAKALA: HAKUNA TENA MGAO WA MAJI DAR
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amosi Makala amesema kuwa mgao wa maji uliokuwa unaendelea katika Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani hautakwepo tena kufuatia kuongezeka kwa maji kwenye chanzo cha Mto Ruvu ikiwa ni matokeo ya mvua zinazoendelea kunyesha kwenye mikoa mbalimbali.
Chanzo: dawasatz
Halafu kuna sehemu katika Maelezo yako nimeona umemshukuru Rais Samia. Je, ina maana kumbe hizi mvua zinazoujaza sasa Mto Ruvu yeye (Rais) ndiyo alikuwa kazifungia na sasa kaamua kuziachia baada ya wananchi (wakazi) wa Dar es Salaam kumlilia kutokana na mgawo wa maji?
Na nijuavyo mimi (na hata Kijiografia) ni kwamba kujaa kwa mto Ruvu kunatokana na mvua za mkoani Morogoro (hasa kule milmani) inayopelekea mito kujaa na kuja kumwaga Mto Ruvu. Sasa RC Makalla huko Morogoro mvua kubwa zimenyesha lini hadi kujaza Mto Ruvu na kumaliza rasmi mgao wa maji mkoani Dar es Salaam?
Kwani mkisema tu kuwa mgao wa maji uliokuwepo ulikuwa ni mkakati maalum wa kuhakikisha mashamba makubwa ya matajiri unakopita mto yaweze kumwagiliwa kisha mabwawa ya kuhifadhia maji ya akiba huko mashambani yajazwe na miradi ya uchimbwaji wa visima jijini Dar es Salaam ikubaliwe na serikali ili watu (wajanja) wapige pesa kiulaini mtapungukiwa nini?
Ni matumaini yangu makubwa wodi za Hospitali za Milembe (Dodoma) na Lutindi (Tanga) mmeshamuandalia kitanda chake huyu RC ili awahi kuanza tiba, kwani wakati akitudanganya wenye akili kubwa kumzidi kuwa hakuna tena mgao wa maji mkoani kwake (Dar es Salaam) kumbe bado mpaka muda huu (saa 8 na dakika 27 usiku mkubwa) maeneo mengi ya mkoa wa Dar es Salaam watu hawana maji).
Hovyo kabisa.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amosi Makala amesema kuwa mgao wa maji uliokuwa unaendelea katika Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani hautakwepo tena kufuatia kuongezeka kwa maji kwenye chanzo cha Mto Ruvu ikiwa ni matokeo ya mvua zinazoendelea kunyesha kwenye mikoa mbalimbali.
Chanzo: dawasatz
Halafu kuna sehemu katika Maelezo yako nimeona umemshukuru Rais Samia. Je, ina maana kumbe hizi mvua zinazoujaza sasa Mto Ruvu yeye (Rais) ndiyo alikuwa kazifungia na sasa kaamua kuziachia baada ya wananchi (wakazi) wa Dar es Salaam kumlilia kutokana na mgawo wa maji?
Na nijuavyo mimi (na hata Kijiografia) ni kwamba kujaa kwa mto Ruvu kunatokana na mvua za mkoani Morogoro (hasa kule milmani) inayopelekea mito kujaa na kuja kumwaga Mto Ruvu. Sasa RC Makalla huko Morogoro mvua kubwa zimenyesha lini hadi kujaza Mto Ruvu na kumaliza rasmi mgao wa maji mkoani Dar es Salaam?
Kwani mkisema tu kuwa mgao wa maji uliokuwepo ulikuwa ni mkakati maalum wa kuhakikisha mashamba makubwa ya matajiri unakopita mto yaweze kumwagiliwa kisha mabwawa ya kuhifadhia maji ya akiba huko mashambani yajazwe na miradi ya uchimbwaji wa visima jijini Dar es Salaam ikubaliwe na serikali ili watu (wajanja) wapige pesa kiulaini mtapungukiwa nini?
Ni matumaini yangu makubwa wodi za Hospitali za Milembe (Dodoma) na Lutindi (Tanga) mmeshamuandalia kitanda chake huyu RC ili awahi kuanza tiba, kwani wakati akitudanganya wenye akili kubwa kumzidi kuwa hakuna tena mgao wa maji mkoani kwake (Dar es Salaam) kumbe bado mpaka muda huu (saa 8 na dakika 27 usiku mkubwa) maeneo mengi ya mkoa wa Dar es Salaam watu hawana maji).
Hovyo kabisa.