Arnold Kalikawe
Senior Member
- Sep 28, 2016
- 145
- 335
Mahakama ya Juu ya nchi hiyo, katika uamuzi wa kihistoria wa Jumatano, ilitangaza Kifungu cha 250 cha Kanuni ya Jinai ya Mauritius, ambayo ilianza mwaka 1898, kuwa kinyume na katiba ya nchi.
Sheria hii iliyofutwa hapo awali iliwatia hatiani watu binafsi na kuhukumiwa kifungo cha hadi miaka mitano kwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Uamuzi wa Mahakama ya Juu ulisisitiza kuwa sheria hii haikuafikiana na maadili halisi ya watu asilia wa Mauritius bali ni masalia tu ya sheria na historia ya ukoloni wa taifa hilo kutoka Uingereza.
Safari ya kuelekea ubatilishaji huu wa kihistoria ilianza Oktoba 2019 wakati vijana wanne wa Mauritius, wanachama wa kundi la haki za Young Queer Alliance, waliwasilisha pingamizi la kisheria dhidi ya sheria ya kupinga ushoga, wakitaja ukiukaji wake wa haki zao za kimsingi na uhuru.
Uamuzi huu umepokea sifa kutoka kwenye Umoja wa Mataifa na mashirika mengi ya haki za binadamu. UNAids, katika taarifa waliyoichaoisha, iliikaribisha Mauritius katika orodha inayozidi kuongezeka ya nchi za Kiafrika ambazo zinakumbatia haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na zile za LGBTQI+ na Mambo ya ushoga.
Kwa hakika, Mauritius sasa inaungana na mataifa mengine ya Kiafrika kama vile Afrika Kusini, Angola, Botswana, Ushelisheli na Msumbiji katika kuhalalisha uhusiano wa watu wa jinsia.
Sheria hii iliyofutwa hapo awali iliwatia hatiani watu binafsi na kuhukumiwa kifungo cha hadi miaka mitano kwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Uamuzi wa Mahakama ya Juu ulisisitiza kuwa sheria hii haikuafikiana na maadili halisi ya watu asilia wa Mauritius bali ni masalia tu ya sheria na historia ya ukoloni wa taifa hilo kutoka Uingereza.
Safari ya kuelekea ubatilishaji huu wa kihistoria ilianza Oktoba 2019 wakati vijana wanne wa Mauritius, wanachama wa kundi la haki za Young Queer Alliance, waliwasilisha pingamizi la kisheria dhidi ya sheria ya kupinga ushoga, wakitaja ukiukaji wake wa haki zao za kimsingi na uhuru.
Uamuzi huu umepokea sifa kutoka kwenye Umoja wa Mataifa na mashirika mengi ya haki za binadamu. UNAids, katika taarifa waliyoichaoisha, iliikaribisha Mauritius katika orodha inayozidi kuongezeka ya nchi za Kiafrika ambazo zinakumbatia haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na zile za LGBTQI+ na Mambo ya ushoga.
Kwa hakika, Mauritius sasa inaungana na mataifa mengine ya Kiafrika kama vile Afrika Kusini, Angola, Botswana, Ushelisheli na Msumbiji katika kuhalalisha uhusiano wa watu wa jinsia.