Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,447
- 7,823
Wale wana walioshinda kule Marekani TRA Tanzania inawasubiri kwa hamu, hela walizoshinda zitakatwa kodi ya 30%, yaani mtu ambae hajaruka sarakasi hata moja anakinga mkono apewe 30%. Akishaichukua wenyewe ndio wagawane 50% each kwenye kilichobaki.
600m-180m inabaki 420m, wakishapata hiyo wakigawana kila mmoja anaondoka na 210.. Yaani kila mmoja anakuwa amemzidi bwana TRA milioni 30 pekee. Wangekuwa watatu TRA angewapiga bao kwenye maokoto. Nafuu itatokea endapo watalipa kodi hela zilikotoka.
Aliyeunda mifumo ya kodi na tawala duniani alichemka kwenye kiwango wanachotakiwa kuchukua mifukoni mwetu. Vilio ni hivi hivi kwenye kodi ya biashara na slip za mishahara, gross inanona ila hapo kati wanakuja TRA na taasisi nyingine za Serikali wanaikausha kila mwezi, bado ukistaafu wanaleta mastori ya vikokotoo.
Ukimaliza yote hayo, njoo kwenye matumizi ya hizo kodi kwenye nchi zetu za dunia ya tatu
600m-180m inabaki 420m, wakishapata hiyo wakigawana kila mmoja anaondoka na 210.. Yaani kila mmoja anakuwa amemzidi bwana TRA milioni 30 pekee. Wangekuwa watatu TRA angewapiga bao kwenye maokoto. Nafuu itatokea endapo watalipa kodi hela zilikotoka.
Aliyeunda mifumo ya kodi na tawala duniani alichemka kwenye kiwango wanachotakiwa kuchukua mifukoni mwetu. Vilio ni hivi hivi kwenye kodi ya biashara na slip za mishahara, gross inanona ila hapo kati wanakuja TRA na taasisi nyingine za Serikali wanaikausha kila mwezi, bado ukistaafu wanaleta mastori ya vikokotoo.
Ukimaliza yote hayo, njoo kwenye matumizi ya hizo kodi kwenye nchi zetu za dunia ya tatu