Losambo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 2,612
- 864
Kwa wanajamvi kwa ujumla.
Natumanini wote mtakuwa mmesikia hukumu iliyovuta hisia za watu wengi ya jimbo la Segerea. Ni kilio na furaha kutegemeana na upande uliopo.
Lengo langu la leo si kujadili hukumu bali kumpa ushauri rais wangu Jakaya M. Kikwete kuwa asimchague au asimrudishe Mh. Makongoro Mahanga katika baraza jipya la mawaziri analotarajiwa kulitangaza muda wowote wiki hii.
Kwa nini nasema hivi?
Ni wazi ushindi wa Makongoro licha ya kuonekana na mawaa mengi machoni pa wananchi ambao ni wapiga kura lakini sheria haijamtia hatiani.
Kutokana na hilo la ushindi wa Makongoro kuwa na mawaa, sikiliza kilio cha wapiga kura indirect kwa kutomrudisha Makongoro katika baraza jipya atakuchafua.
Ukifanya hivyo utakuwa umetibu makovu ya wengi ambao wanaamini kabisa Mahanga kapendelewa na kurudisha imani kwa wananchi katika hukumu ile hakukuwa na mkono wako ili umrudishe barazani licha ya kesi kuonekana kumkalia kooni.
Endapo ukimrudisha wakatokea wajanja na kupitisha maneno katika media au vyovyote vile utakuwa na wakati mgumu wa kujitetea japokuwa naamini huwajibiki kujitetea kwa yoyote yule.
Ni kweli lakini uchungu wa wananchi ambao wangependa kusikia sauti yako kupitia baraza la mawaziri kwa kutoiona sura ya Mahanga inaweza kuwa mbaya sana 2015 kwa utakayempa kijiti akupokee endapo atarudi tena.
Kwanza utendaji wake ni wa kawaida sana na safu yako bado ina watu wengi ambao wanaweza kuwa mbadala kwa huyo mtu mmoja ambaye aaweza kukuchafua pasipo sababu.
Naomba ulione hili kwa uzito wake.
Karibuni kwa mjadala huu.
Losambo.
Natumanini wote mtakuwa mmesikia hukumu iliyovuta hisia za watu wengi ya jimbo la Segerea. Ni kilio na furaha kutegemeana na upande uliopo.
Lengo langu la leo si kujadili hukumu bali kumpa ushauri rais wangu Jakaya M. Kikwete kuwa asimchague au asimrudishe Mh. Makongoro Mahanga katika baraza jipya la mawaziri analotarajiwa kulitangaza muda wowote wiki hii.
Kwa nini nasema hivi?
Ni wazi ushindi wa Makongoro licha ya kuonekana na mawaa mengi machoni pa wananchi ambao ni wapiga kura lakini sheria haijamtia hatiani.
Kutokana na hilo la ushindi wa Makongoro kuwa na mawaa, sikiliza kilio cha wapiga kura indirect kwa kutomrudisha Makongoro katika baraza jipya atakuchafua.
Ukifanya hivyo utakuwa umetibu makovu ya wengi ambao wanaamini kabisa Mahanga kapendelewa na kurudisha imani kwa wananchi katika hukumu ile hakukuwa na mkono wako ili umrudishe barazani licha ya kesi kuonekana kumkalia kooni.
Endapo ukimrudisha wakatokea wajanja na kupitisha maneno katika media au vyovyote vile utakuwa na wakati mgumu wa kujitetea japokuwa naamini huwajibiki kujitetea kwa yoyote yule.
Ni kweli lakini uchungu wa wananchi ambao wangependa kusikia sauti yako kupitia baraza la mawaziri kwa kutoiona sura ya Mahanga inaweza kuwa mbaya sana 2015 kwa utakayempa kijiti akupokee endapo atarudi tena.
Kwanza utendaji wake ni wa kawaida sana na safu yako bado ina watu wengi ambao wanaweza kuwa mbadala kwa huyo mtu mmoja ambaye aaweza kukuchafua pasipo sababu.
Naomba ulione hili kwa uzito wake.
Karibuni kwa mjadala huu.
Losambo.