Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amejisalimisha kwa Polisi ili kuanza kutumikia kifungo cha miezi 15 jela

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,516
9,317
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma amejisalimisha kwa polisi ili kuanza kutumikia kifungo cha miezi 15 jela.

Wakfu wa Zuma Foundation uliandika katika mtandao wake wa Twitter kuwa kiongozi huyo ameamua kuheshimu agizo la korti na kwamba alikuwa njiani kuelekea katika kituo cha polisi cha wilaya ya Kwa Zulu-Natal.

Msemaji wa polisi Lirandzu Themba amethibitisha kuwa Zuma yuko chini ya ulinzi wa polisi baada ya kujisalimisha.

Dakika chache tu kabla ya muda wa mwisho aliyopewa na korti kujisalimisha kwa hiari kabla ya polisi kumkamata, Zuma aliondoka nyumbani kwake Nkandla akisindikizwa na msafara wa magari.
 
Wapo watu walikua wanadanganyana kuwa eti Zuma watamlinda jana police imetoa Tangazo siku ikiisha bila kujisalimisha atakamtwa kwa nguvu wahuni wote wamerudi nyuma ambao walisema damu itamwagika Zuma hawawezi kukamatwa...
Hujui usemalo. Kuna majadiliano yamefanyika makali sana kati ya Zuma na police minister Bheki Cele. Damu ingemwagika kama Zuma angekataa kujisalimisha. Kilichofanyika ni kwamba Zuma ameshauriwa akubali kujisalimisha ili kuepusha "mgogoro wa kikatiba" maana alikuwa na uwezo wote wa kutokujisalimisha na police wangenywea kumkamata, na kama wangethubutu kumkamata machafuko makubwa sana yangetokea. Kwa hiyo busara imetumika ili kuwaaminisha wasouth africa kuwa no one is above the law. Na kaondoka kwenye kasri lake na msafara wa magari kibao kuelekeo polisi akiwa na wapambe kibao nyuma yake.
 
Hujui usemalo. Kuna majadiliano yamefanyika makali sana kati ya Zuma na police minister Bheki Cele. Damu ingemwagika kama Zuma angekataa kujisalimisha. Kilichofanyika ni kwamba Zuma ameshauriwa akubali kujisalimisha ili kuepusha "mgogoro wa kikatiba" maana alikuwa na uwezo wote wa kutokujisalimisha na police wangenywea kumkamata, na kama wangethubutu kumkamata machafuko makubwa sana yangetokea. Kwa hiyo busara imetumika ili kuwaaminisha wasouth africa kuwa no one is above the law. Na kaondoka kwenye kasri lake na msafara wa magari kibao kuelekeo polisi akiwa na wapambe kibao nyuma yake.
Hakuna cha damu kumwagika Wala nini,ye atulie akasafishwe mtaro.
 
Back
Top Bottom