Rais Tshisekedi siku zake zinahesabika

Akilihuru

JF-Expert Member
May 20, 2022
1,447
2,838
Wakuu inakuaje? sasa twende kazi.

Siku mbili tatu hizi kumekuwa na hali ya sintofahamu kati ya serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na ile ya Rwanda, kila mmoja akimtupia lawama mwenzake na kutishia kuvunjilia mbali uhusiano wao wa kidiplomasia nk.

Kwa upande wa Congo ndio wanaonekana kuwa wamechukia zaidi hadi kupelekea serikali yao kumfukuza nchini kwao balozi wa Rwanda, na pia kumwata balozi wao aliekuwa nchini Rwanda.

Kwa upande wa Rwanda yenyewe haioneshi kupanic wala kuchukizwa kivile, inaonekana ime relax ikisubiria kuona kingine kitachojiri kutoka katika serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Sasa basi... Rwanda ina uwezo wa kuichakaza na kuisambaratisha Congo kijeshi kwa njia zote, iwe kwa angani, majini au ardhini tena kwa muda mfupi sana.

Congo inaweza kuishinda Rwanda kwa maneno tu, maana wakongomani ni waimba miziki na wachezaji wakubwa, ila linapokuja swala la mapambano ya kijeshi na weupe sana wanashindwa hata na Burundi.

Kwanza toka Congo ilipopata uhuru jeshi lake halikuwahi kushinda vita yoyote ile. Wakati wa Mobutu jeshi la Congo lilichakazwa vibaya na waasi waliokuwa wanaongozwa na hayati Desire Kabila (father) na baadae jeshi hilo limeendelea kuchakazwa na makundi mbali mbali ya waasi wengi wao ni kutoka nchi jirani.

Sasa jiulize ikiwa nchi yenye raia zaidi ya milioni 1 inachakazwa na waasi wasiozidi elfu 5, huku waasi hao wakiwa na silaha za kuunga unga na mazoezi ya msituni yasiokuwa rasmi. Je watakapoingia kwenye vita na nchi yenyewe si ndo yatakuja kutokea yale ya Mobutu na Idi Amini!!

Hivi kweli Tshisekedi anaamini kuwa nchi yake inaweza kuipiga Rwanda au ndo kifo kinamwita, au wazee wa kazi (Kabila's team) wanamshauri ujinga ili akipigwa akikimbia Kabila arudi kuongoza Congo?

Maana katika hali ya kawaida haiwezekani nchi inayoshindwa vita na waasi elfu 3, ijidanganye kuwa inaweza kupambana na nchi yenye wanajeshi zaidi ya laki, wenye ueledi mkubwa wa kivita, silaha za kisasa na wanajeshi wa kutosha.

Katika EAC nzima, nchi ambazo Rwanda inaweza kuhofia kwa namna fulani kupambana nazo ni Tanzania na Kenya tu ambazo majeshi yao yameshafanya mambo makubwa ndani na nje ya mipaka yao Tanzania ikiwa inaongoza kwa kufanikiwa oparation mbali mbali katika nchi za Msumbiji, Zimbabwe, Angola, Namibia, Comoros nk. Ila hizo zingine Rwanda inaziona kama vile ni nchi zinazolindwa na makundi ya sungu sungu tu na sio wanajeshi kamili.

So chonde chonde Tshisekedi watu bado wanakuhitaji uendelee kuwa raisi wao. Usije kuingia kwenye mtego ambao utashindwa kujinasua. Kagame alimhofia Kikwete tu mjeshi mwenzake na anajua watu wa kicheka cheka kama JK maamuzi yao yanakuwaga na athari kubwa kwa wengine. Lakini nyinyi wengine anawaona vikaragosi wake.

Tena kwa Congo ndo kabisa hawezi kutuma jeshi lake kupoteza muda wao. Sana sana ataajiri vijana kutoka katika makampuni mbali mbali ya ulinzi waje kumaliza kazi.

Pichani juu ni jeshi la Rwanda na picha ya chini ni jeshi la Congo.
images (37).jpeg

images (40).jpeg

Siku njema kwa wasomaji na wachangiaji wote. Asanteni.
 
Tshisekedi awe na ulinzi usiohusisha wakongoman.... My opinion, Jamaa hakawii kanunua walinzi kwa mamilion ya dollar!
Ni ngumu sana, Congo ina walinzi royal sana mfano bodyguards wa Rais Mobutu ukitazama mahojiano yao utaelewa, wale jamaa walipewa kiapo cha kufa kwa ajili ya Rais na walikuwa hawaogopi kifo

Kabila mkubwa alijichanganya akaweka vilinzi vitoto visivyo na mafunzo yoyote ndicho kilimuangusha
 
Binafsi kwa utashi wangu Rwanda ni choko sana, anatafuta nini Congo..?

Si atulize makalio nchini nwake...!? Yeye deilee kumsakama Congo ili amwibie madini yake na magogo, aitajirishe Rwanda.

Muda huo Congo hali ni tete. Makundi ya M23 nina imani ni ya Rwanda yana leta choko choko ili waendelee kupiga mali za Congo.

Cha msingi hapo ni Congo kujilipua/kuamua kuhakikisha wana wafyekelea mbali hao wasenge wabaki kwao Rwanda.

Kila mtu awe na maisha yake, ili Congo iweze kupiga hatua na yenyewe, mambo ya kuwa mtumwa wa Ufaransa na mbelgiji, bado na Rwanda akutawale khaaa ni ujinga na kukubali utumwa mpya nchini mwako.

Congo jilipueni hakikisheni mna fyeka hao jamaa ili muweze ku survive kwa amani nchini kwenu, haiwezekani nchi ina utajiri wa kila madini ardhi yenye rutuba, misitu mikubwa, mto mkubwa africa, lakini nchi haina maendeleo hata bara bara za mikoani ni vumbi tupu, umeme shida utafikiri ndio mmepata uhuru juzi 2020 badilikeni wa congo amueni jitoeni.
 
Binafsi kwa utashi wangu Rwanda ni choko sana, anatafuta nini Congo..? Si atulize matako nchini nwake yeye deilee kumsakama Congo ili amwibie madini yake na magogo, aitajirishe Rwanda muda ho Congo hali tete hata hayo makundi ya M23 nina imani ni ya Rwanda yana leta choko choko ili waendelee kupiga mali za Congo cha msingi hapo ni Congo kujilipua tu kuhakikisha wana wafyekelea mbali hao wasenge wabaki kwao kila mtu awe na maisha yake ili Congo iweze kupiga hatua nayo sio mambo ya kuwa mtumwa wa Ufaransa na mbelgiji bado na Rwanda akutawale khaaa
Namna ya kusavaivu
 
Ukiniuliza mimi kwenye vita kamili isiyo ya kujificha kati ya Rwanda na DRC nani anashinda nasema ni DRC endapo hakuna external influence baina ya pande zote mbili.

Congo ukitaka kuipima kwa kuangalia eneo lake la Mashariki utapotea, itazame nchi nzima hadi kule Magharibi. Mashariki ni kama imepotezewa na ina waasi wengi wanaojificha na kusumbua kila wakijisikia. Wakipigwa wanavaa kiraia wanalima, wakipata support wanaanza mapigano. Ukija kwenye vita ya nchi na nchi hapo hujifichi, madaraja tunajua yalipo, kambi zilipo, airbase ilipo, HQ, defensive lines na mambo mengine.

Congo sio wazembe kuliko nchi nyingi za Kiafrika, tatizo lao wana rasilimali nyingi na bahati mbaya ya kunyonywa na mataifa ya nje, ila nchi nyingi za Afrika hazina unafuu kijeshi kuwazidi. Hakuna nchi ina makundi ya waasi hadi 10 kama Congo ilivyo, logistics za kuipiga Congo kuanzia mpakani kwa Rwanda mpaka katikati ya nchi kule ni gharama kwa Rwanda. Rwanda kuipiga Congo sio rahisi hata kidogo
 
Back
Top Bottom