Benaya-
JF-Expert Member
- Jul 31, 2019
- 4,417
- 7,610
Mheshimiwa rais na amiri Jeshi mkuu Samia Suluhu shikamoo.
Ninaandika machache kuhusu udhalilishaji unaoendelea nchini kwa masikitiko makubwa sana.
Kwa wasomi wa Biblia wanafahamu vyema hadithi ya Binti wa Kiyahudi jina lake Ester.
Binti huyu hakuwa na wazazi bali alilelewa na mjomba/binamu yake aitwaye Modekai.
Ester alishawishiwa na Modekai ambaye alikuwa mmoja wa watumishi wa Mfalme Ahasuero kuwa ajitokeze kwenye tafrija ya mfalme ya kutafuta mwanamwali awe mkewe.
Ester alifanikiwa kuibuka mshindi na kuwa mke wa mfalme, jambo ambalo lilikuwa gumu sana kwa Myahudi kuibuka mshindi kwani yeye alikuwa ni mtoto wa mmoja wa watumwa wa mfalme Ahasuero.
Baada ya Ester kuwa mke wa mfalme kwa kiasi flani alijitenga na Wayahudi wenzake ambao waliendelea kuteswa kubaguliwa nk.
Lakini ulifika wakati mgumu wa Wayahufi wote kuuawa kwa amri ya mfalme.
Modekai mjomba wake alimwendea ali awatetee lakini Ester hakuonekana kujali sana.
Ndipo Modekai alipomwambia Ester.
IKIWA HUONI UMUHIMU WA KULITETEA TAIFA LAKO MUNGU ATATOKEZA MSAADA MWINGINE LAKINI WEWE NA NYUMBA YAKO UTATEKETEA.
Rais wangu, kumekuwa na udhalilishaji mkubwa sana wa wanawake nchini kwa neno maarfu KONEKSHENI.
Hii inafanywa sana na dada aitwaye Mange Kimambi, jambo hili limeleta hofu na mashaka kwa watu maarufu na wenye ushawishi katika jamii hasa wasanii.
Jambo hili lisipodhibitiwa mapema hakika litasababisha vifo vitokanavyo na msongo wa mawazo.
Mheshimiwa rais wewe ni mwanamke Mungu ameruhusu uwe rais sio kwasababu wewe ni bora kuliko wanawake wote Tanzania bali imempendeza akuchague wewe ili uvae viatu vya mateso ya wanawake wa Tanzania.
Mange anakusikiliza sana...ukimwagiza msaidizi wako Yunus akipiga simu moja tu wanawake watakuwa salama.
Mama kemea kemea hii kitu ni mbaya.
Ninatanguliza shukrani nikiamini utalifikiria jambo hili.
Ninaandika machache kuhusu udhalilishaji unaoendelea nchini kwa masikitiko makubwa sana.
Kwa wasomi wa Biblia wanafahamu vyema hadithi ya Binti wa Kiyahudi jina lake Ester.
Binti huyu hakuwa na wazazi bali alilelewa na mjomba/binamu yake aitwaye Modekai.
Ester alishawishiwa na Modekai ambaye alikuwa mmoja wa watumishi wa Mfalme Ahasuero kuwa ajitokeze kwenye tafrija ya mfalme ya kutafuta mwanamwali awe mkewe.
Ester alifanikiwa kuibuka mshindi na kuwa mke wa mfalme, jambo ambalo lilikuwa gumu sana kwa Myahudi kuibuka mshindi kwani yeye alikuwa ni mtoto wa mmoja wa watumwa wa mfalme Ahasuero.
Baada ya Ester kuwa mke wa mfalme kwa kiasi flani alijitenga na Wayahudi wenzake ambao waliendelea kuteswa kubaguliwa nk.
Lakini ulifika wakati mgumu wa Wayahufi wote kuuawa kwa amri ya mfalme.
Modekai mjomba wake alimwendea ali awatetee lakini Ester hakuonekana kujali sana.
Ndipo Modekai alipomwambia Ester.
IKIWA HUONI UMUHIMU WA KULITETEA TAIFA LAKO MUNGU ATATOKEZA MSAADA MWINGINE LAKINI WEWE NA NYUMBA YAKO UTATEKETEA.
Rais wangu, kumekuwa na udhalilishaji mkubwa sana wa wanawake nchini kwa neno maarfu KONEKSHENI.
Hii inafanywa sana na dada aitwaye Mange Kimambi, jambo hili limeleta hofu na mashaka kwa watu maarufu na wenye ushawishi katika jamii hasa wasanii.
Jambo hili lisipodhibitiwa mapema hakika litasababisha vifo vitokanavyo na msongo wa mawazo.
Mheshimiwa rais wewe ni mwanamke Mungu ameruhusu uwe rais sio kwasababu wewe ni bora kuliko wanawake wote Tanzania bali imempendeza akuchague wewe ili uvae viatu vya mateso ya wanawake wa Tanzania.
Mange anakusikiliza sana...ukimwagiza msaidizi wako Yunus akipiga simu moja tu wanawake watakuwa salama.
Mama kemea kemea hii kitu ni mbaya.
Ninatanguliza shukrani nikiamini utalifikiria jambo hili.