Rais Samia Suluhu Hassan, sambaratisha Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu

KooZito

JF-Expert Member
Dec 14, 2020
396
1,377
Wanabodi Shaloom!

Ninakuomba kama itakupendeza futilia mbali Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ili fedha za umma zinazoteketea kuligharamia zitumike kwingine. Ni kitengo cha upigaji.

Nikukumbushe: mwaka 2005 baada ya Jakaya kuingia madarakani ndipo kitengo hiki kiliundwa mahsusi kumpa Salvatory Rweyemamu ulaji kwa kazi kubwa aliyoifanya kumpamba Jakaya na kuwachafua wapinzani wake kupitia gazeti la RAI Nguvu ya Hoja.

Nafasi za Ubunge, Uwaziri, U-DC au RC hazikuonekana "kumtosha" Salva ndipo alipopendekeza kuwepo na Kurugenzi hiyo ili asafiri na Rais popote duniani na posho ya dola 6700 kwa siku kwa kila safari nje ya nchi.

Rais Magufuli alipoingia naye akaridhi kitengo hiki cha upigaji hela za umma akimweka Gerson Msigwa ambaye naye akawaalika "washikaji" wake kujazana hapo bila kazi maalum zaidi ya kupiga hela. Ofisi ina watu 13 lakini uliza kazi ya kila mmoja ni nini?

Magufuli alisambaratisha kitengo cha Jikoni-Ikulu iliyokuwa na watu zaidi ya 100 akisema, "nitapikiwa na mke wangu". Kilikuwa cha upigaji sawa na hii Kurugenzi.

Unajiuliza Rais anaye Katibu wake, Mwandishi wake wa Habari, Mpigapicha, nini kazi ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu? Hivi kuandika barua za teuzi na tenguzi ni za kuajiri Mkurugenzi na Idara hewa chini yake? Nini kazi ya Msemaji Mkuu wa Serikali?

Sasa tunaona Msigwa ndiye Msemaji wa Serikali na wakati huo ndiye Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu (Serikali). Huku ni kuchanganya Mawasiliano ndio maana tulishuhudia JPM akikana uwepo wa Covid-19 na Dk. Abbas akikiri kuwepo Corona. Ikulu vs Idara ya Habari MAELEZO.

Fedha za kugharamia Kurugenzi hii zielekezwe kwenye matumizi mengine. Nawasilisha!

#FreedomIsBack
 
Huo ni wivu na majungu. Mkurugenzi hiyo ina majukumu mazito ndomaana kikaanzishwa na tunaona uwajibikaji katika utoaji habari, uendeshaji hafla na shughuli zingine za ikulu.

Tumeona juzi Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiteua wasaidizi kadhaa ktk masuala mbalimbali. Ikulu ni taasisi hivyo inapaswa kuwa na Mkurugenzi.

Yawezekana nawe ni miongoni mwa waliopunguzwa Ktk Jiko LA Ikulu hivyo unaoenda mkose wote.

Kwamba Msigwa kajaza washkaji wake, sio jambo LA kweli, Ikulu hawawezi kuwa kama N. G.O, kutoa ajira kiholera namna hiyo.

Acha Msigwa apige kazi, kijana hodari sana na mchapa kazi. Kazi Iendeleee.
 
Mimi Wala Sina Shida ni nani awepo wapi wakati huu ila ili Mama afanye kazi yake vizuri tumpe muda ajipange..

Hii kazi na style aliyochukua nchi ni tofauti sana..Akianza kufukuza wote mara moja wakati ndio anajipanga anaweza kuharibu zaidi...

Kazi ya Urais ni ngumu sana ...sio rahisi sana kama mnavyowaza..Mpeni Muda ajitulize kwenye kiti kile.
 
Huo ni wivu na majungu. Mkurugenzi hiyo ina majukumu mazito ndomaana kikaanzishwa na tunaona uwajibikaji katika utoaji habari, uendeshaji hafla na shughuli zingine za ikulu.

Tumeona juzi Mheshimiwa SSH, akiteua wasaidizi kadhaa ktk masuala mbalimbali. Ikulu ni taasisi hivyo inapaswa kuwa na Mkurugenzi.

Yawezekana nawe ni miongoni mwa waliopunguzwa Ktk Jiko LA Ikulu hivyo unaoenda mkose wote.

Kwamba Msigwa kajaza washkaji wake, sio jambo LA kweli, Ikulu haoawezi kuwa kama N. G.O, kutoa ajira kiholera namna hiyo.

Acha Msigwa apige kazi, kijana hodari sana na mchapa kazi. Kazi Iendeleee.
Uko sahihi mkuu. Jamaa yuko vizuri. Mengine haya ni majungu tuu.
 
Kwa siku posho $6700 = TShs 15,443,500/=

Kuna baadhi ya watu wanaifaidi hii nnchi aisee

😅😅😅
hiyo ni ya kusafiri nje ya nchi, sasa uliza ya ndani ya nchi lazima itakiwa zaidi ya m 2 kwa siku wakati watumishi wengine ni 100,000 mpaka 150,000 kwa siku. kinachotakiwa ni kutafuta connection na wewe ubunje mahela hayo.
 
Huo ni wivu na majungu. Mkurugenzi hiyo ina majukumu mazito ndomaana kikaanzishwa na tunaona uwajibikaji katika utoaji habari, uendeshaji hafla na shughuli zingine za ikulu.

Tumeona juzi Mheshimiwa SSH, akiteua wasaidizi kadhaa ktk masuala mbalimbali. Ikulu ni taasisi hivyo inapaswa kuwa na Mkurugenzi.

Yawezekana nawe ni miongoni mwa waliopunguzwa Ktk Jiko LA Ikulu hivyo unaoenda mkose wote.

Kwamba Msigwa kajaza washkaji wake, sio jambo LA kweli, Ikulu hawawezi kuwa kama N. G.O, kutoa ajira kiholera namna hiyo.

Acha Msigwa apige kazi, kijana hodari sana na mchapa kazi. Kazi Iendeleee.
Wizi mtupu huo na wewe hakuna mtu wa kuamini maneno yako maana mataga kazi yenu ni kutetea wizi na ufisadi.
 
Huo ni wivu na majungu. Mkurugenzi hiyo ina majukumu mazito ndomaana kikaanzishwa na tunaona uwajibikaji katika utoaji habari, uendeshaji hafla na shughuli zingine za ikulu.

Tumeona juzi Mheshimiwa SSH, akiteua wasaidizi kadhaa ktk masuala mbalimbali. Ikulu ni taasisi hivyo inapaswa kuwa na Mkurugenzi.

Yawezekana nawe ni miongoni mwa waliopunguzwa Ktk Jiko LA Ikulu hivyo unaoenda mkose wote.

Kwamba Msigwa kajaza washkaji wake, sio jambo LA kweli, Ikulu hawawezi kuwa kama N. G.O, kutoa ajira kiholera namna hiyo.

Acha Msigwa apige kazi, kijana hodari sana na mchapa kazi. Kazi Iendeleee.
Majambazi wa rasilimali za watanzania
 
Back
Top Bottom