Rais Samia: Huwa napitia JamiiForums naangalia maoni yenu

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,447
7,830
Rais Samia: Hakuna kisichowezekana kwenye mazungumzo, tumeshuhudia nchi kadhaa zimeingia kwenye vita hawakupata suluhu, suluhu imepatikana kwenye mazungumzo kwahiyo tuendelee kuzungumza. Najua si rahisi kabisa watu kuja na utamaduni huu mpya ukakubalika mara moja, si rahisi, kwenuu kuna vikwazo kwangu kuna vikwazo.

Huwa napitia Jamiiforums naangalia maoni yenu kule ndani, nasoma nnacheka, nasema lakini huu ni utamaduni mpya, si rahisi kukubalika kwa ghafla, kwahiyo pande zote Tanzania nzima si rahisi kukubali utamaduni huu mpya kwa haraka.


======

Samia bawacha.jpeg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wanawake wa CHADEMA, viongozi mbalimbali wa Baraza la Wanawake CHADEMA (BAWACHA) pamoja na Wanachama wa Chama hicho kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Moshi Mkoani Kilimanjaro tarehe 08 Machi, 2023.

Rais Samia alihudhuria kongamano hilo akiwa mgeni rasmi aliyealikwa na wanachama hao, Rais Samia amesema utamaduni wa mazungumzo ni mgeni kwa nchi yetu na unaletewa vikwazo kwenye pande zote mbili
yaani mamlaka pamoja na CHADEMA, lakini amesisitiza ndio njia salama ya kufikia makubaliano katika kutatua changamoto na kuahidi kuendelea na mazungumzo ili kufikia maridhiano.

Katika kongamano hilo Rais Samia amewaambia wanachama hao kuwa amekuwa akipita katika mtandao wa Jamiiforums.com na kusoma maoni yao huko ndani na kisha anacheka. Kauli hiyo imeamsha ari ya wanachama na watanzania wengi na kuwaongezea motisha katika kutumia mtandao wa Jamiiforums kwa kuona kuwa ni sehemu salaa na ya uhakika ambayo wanawasilisha mawazo na maoni yao moja kwa moja na kusomwa na Rais na viongozi wao mbalimbali ivyo kupata uhakika wa mawazo yao kufanyiwa kazi.

Baadhi ya maoni ya wanachama wa Jamiiforums.com
Ameyaweka wazi hayo katika mkutano wa Bawacha katika siku ya mwanamke duniani.

Rais Samia akihutubia taifa kupitia mkutano huo amewaambia kuwa huwa anasoma maoni ya katiba mpya, wabunge wa Covid19 na mengineyo kuhusu Serikali yake kupitia mtandao maarufu wa JamiiForums.

My take:
Leo ndio nimejua kuwa kumbe Rais Samia nae ni mdau wa JamiiForums.

Hii imetuinua sana wana jukwaa hili.
Sasa Maxence Melo umemsikia mwenyewe mama anapitia JF kusoma mijadala.

Rai yangu kwako jukwaa la siasa limejaa uchafu ningependekeza thread zote zisiruke hewani bila approval ya moderator ili kupunguza uchafu jukwaani.

Na ikiwezekana uongeze nguvu jukwaa la siasa ili mijadala yenye afya irudi kama zamani, watu hawachangii jukwaa la siasa Sasa hivi limejaa matakataka mengi.

Please litendee haki JF ambayo leo mama ameipaisha kama platform anayoitegemea kupata maoni.

Na ndio sababu tuliokataa unafki tumejipambanuwa wazi kwamba Magufuli alikuwa ni shetani na muuwaji, mama ameyasoma yote haya na leo ameahidi kwa kusema never, never again.

Cc: Pascal Mayalla
Jf ni kubwa sana kuliko wengine wanavyoiona

Jf ina heshima zaidi na inasomeka na kila aina ya watu na matabaka ya kila aina
Muwe mnachangia hoja kwa heshima bila kutukanana na pia kuheshimu mawazo ya wengine

Huwa anacheka kwa mengi humu unaweza kuta anamsoma kiduku pia
Mods, JF imepewa heshima kubwa sana. Kama Rais huwa anapitia humu kupata maoni yetu kama sehemu ya umma wa Watanzania, hakika nawaambieni, hakuna kiongozi ambaye hatapita JF.

Lakini ili maoni yetu yapewe uzito wa kupewa tafakuri ni lazima Mods walinde hadhi ya jukwaa kwa kuwapa adhabu kale wale wote wanaoligeuza jukwaa lionekane ni la wahuni.

Mtu akitukana au kukejeli, apigwe ban hata ya miezi 6 au mwaka mzima. Kuna watu humu, wanashangaza, wanafikia kumtukana kiongozi, unatafakari na kujiuliza JF siku hizi imebeba watu wa namna gani?

Mods, lirudisheni jukwaa kwenye heshima yake ili kiwe ni chanzo muhimu cha habari kwa wasio na habari, liwe ni jukwaa la ushauri kwa viongozi wa Serikali, vyama na taasisi mbalimbali.
Kama kweli Mh. Rais unapitiaga maoni yetu yakiwemo ya kupunguza mfumuko wa bei na kupanda kwa gharama za maisha, tunaomba usiishie tu kucheka, jitahidi kupitia kwa wasaidizi wako kutupunguzia ukali wa maisha ili 2025, usitumie nguvu kubwa kutuomba kura. Achana na usemi wa Waswahili kwamba; "Mwenye shibe hamkumbuki mwenye njaa". Please mama, jitahidi kutulegezea gharama za maisha ili na sisi tukupende toka moyoni na siyo tukupende kwa unafiki au kwa sababu ya kukuogopa kutokana na nafasi uliyo nayo.
Binafsi ninaamini, ukiamua unaweza kupunguza gharama za maisha kwa wananchi wako.

Pia soma: Moshi: Yanayojiri katika Kongamano la BAWACHA Siku ya Wanawake Duniani Machi 3, 2023; Rais Samia mgeni rasmi
 
Ameyaweka wazi hayo katika mkutano wa Bawacha katika siku ya mwanamke duniani.

Rais Samia akihutubia taifa kupitia mkutano huo amewaambia kuwa huwa anasoma maoni ya katiba mpya, wabunge wa Covid19 na mengineyo kuhusu Serikali yake kupitia mtandao maarufu wa JamiiForums.

My take:
Leo ndio nimejua kuwa kumbe Rais Samia nae ni mdau wa JamiiForums.

Hii imetuinua sana wana jukwaa hili.
 
Back
Top Bottom