MANKA MUSA
JF-Expert Member
- Jul 9, 2014
- 922
- 1,093
Rais Samia Suluhu Hassan amehudhuria Mkutano wa Jukwaa la Mifumo ya Chakula Afrika (AGRF) 2023 linaloendelea Jijini Dar es Salaam. Tanzania imepata bahati nyingine tena ya kuaminiwa kwa kuwaleta pamoja wakuu wa nchi na wataalamu toka mataifa mbalimbali, kujadili moja ya jambo muhimu kabisa kwa ustawi wa bara letu na ulimwengu, upatikanaji wa chakula.
Afrika imebarikiwa kuwa na asilimia 65 ya ardhi yote inayofaa kwa kilimo duniani lakini zaidi ya Waafrika milioni 250 bado wanalala njaa kila siku. Jukumu letu kuleta mabadiliko ya hali hii ni kubwa na linalohitaji hatua za haraka.
Mikutano ya namna hii ya viongozi, wataalamu na wabobezi ni muhimu katika kubuni mikakati ya kuongeza kasi ya kubadili mifumo ya chakula, kuanzia uzalishaji kwenye kilimo na mnyororo mzima wa thamani, kupitia utekelezaji wa sera bora na uwekezaji sahihi.
Afrika imebarikiwa kuwa na asilimia 65 ya ardhi yote inayofaa kwa kilimo duniani lakini zaidi ya Waafrika milioni 250 bado wanalala njaa kila siku. Jukumu letu kuleta mabadiliko ya hali hii ni kubwa na linalohitaji hatua za haraka.
Mikutano ya namna hii ya viongozi, wataalamu na wabobezi ni muhimu katika kubuni mikakati ya kuongeza kasi ya kubadili mifumo ya chakula, kuanzia uzalishaji kwenye kilimo na mnyororo mzima wa thamani, kupitia utekelezaji wa sera bora na uwekezaji sahihi.