Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete ashiriki mdahalo, mkutano wa World Economic Forum for Africa

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
50ac8e7bf1ed1cb14d17e643df4b8c45.jpg
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameshiriki katika mdahalo wakati wa mkutano wa World Economic Forum for Africa unaofanyika Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo muhimu unaokutanisha wafanyabiashara, wanasiasa na viongozi wa kiserikali una lengo la kutoa fursa kwa wadau wa maendeleo barani Africa, kukutana na kujadili mustakabali wa maendeleo na uwekezaji barani Afrika.

Katika mkutano huo, Mheshimiwa Rais Mstaafu aliwakilisha Kamisheni ya Kimataifa ya Elimu (The Education Commission) ambapo alikutana na wadau wa elimu na vyombo vya habari kuelezea Mpango wa Kizazi cha Elimu barani Afrika.

Chanzo: HabariLeo
 
Kikwete presidency was a failure! Leo wengine wanamuona anafaa kwa sababu wanamlinganisha na JPM. But this man was a failure. No wonder hata Yale mamilioni ya MO Ibrahim Foundation yalimpita pembeni. And this is what I hate about African leaders. Wanafanya madudu wakiwa madarakani wakitoka wanaanza kuhubiri yaliyowashinda wao. Pathetic!
 
Kikwete presidency was a failure! Leo wengine wanamuona anafaa kwa sababu wanamlinganisha na JPM. But this man was a failure. No wonder hata Yale mamilioni ya MO Ibrahim Foundation yalimpita pembeni. And this is what I hate about African leaders. Wanafanya madudu wakiwa madarakani wakitoka wanaanza kuhubiri yaliyowashinda wao. Pathetic!
Wakati wenu huu kina Masanja
 
Back
Top Bottom