Rais Magufuli, tunataka Katiba mpya

HORSE POWER

JF-Expert Member
Feb 22, 2015
2,099
1,415
Habari wanaJF,

Kama mjuavyo, kasi ya 'utumbuaji majibu' imeshamiri. Imepamba moto kiasi kwamba wapo waliobeba kaulimbiu hii 'kikasuku' bila ya kuangalia mipaka ya mamlaka zao.

Niharakishe kutamka hapa kwamba naunga mkono harakati za Rais JPM za kudhibiti wizi 'uliohalalishwa' Serikalini na Taasisi za Umma,kujenga nidhamu kwenye utumishi wa Umma,kudhibiti ukwepaji kodi n.k. Nchi ilikua kwenye 'auto pilot'. Imegeuzwa shamba la bibi,imekua maficho ya wadudu kama mchwa na kupe. Lakini pia kuna 'cannibals'.

Pamoja na juhudi hizi,ni hatari kutegemea mtu au kikundi cha watu kunyoosha mambo.Hili ni suala la nyakati.Hatuwezi kupata Magufuli na Nyerere kila siku.Jambo bora na lenye afya kwa mustakabali wa nchi ni KUSUKA MFUMO MADHUBUTI wa kuongoza nchi yetu.

Hapo ndipo penye ULAZIMA wa Katiba mpya.Katiba ya wananchi (wenye nchi),sio Katiba ya wanasiasa au genge la watu fulani.Tunataka Katiba yetu.Na pa kuanzia kupo.Tuanzie pale kwenye Rasimu ya pili ya Tume ya Katiba.Katiba inayopendekezwa ni ya wanasiasa na washirika wao.

Sisi wananchi HATUITAKI.

Rais Magufuli,tunakuomba sana,kama kweli unawatetea wanyonge,tupatie Katiba yetu.Najua mahafidhina kwenye chama chako hawataki kuiona rasimu ya Warioba,lakini jua kwamba wanyonge wana matumaini makubwa kwako.Tupatie Katiba,hakutokua na tabu tena ya kutumbua majipu kwa mikono kwani Rasimu ile imebeba 'zana' za kutumbulia.

Rais Magufuli,tunataka Katiba mpya.Naanza mimi 'kupiga mayowe'.Chonde chonde Rais wetu,usiondoke bila ya kutuachia alama yako.
 
Jipu Kuu ni Katiba lakini inamnufaisha unadhani atajitumbua bila ya sisi wananchi kuungana na kumlazimisha?
 
Yakamuliwe kwanza majipu maana yalikuepo mpaka kwenye hiyo katiba tarajiwa yakinyauka ndo mchakato uanze
 
Kilio chako kimesikika.Utapewa Katiba pendekezwa iliyosukwa na mwanasheria msomi Mtemi Chenge aka joka lenye makengeza
 
Jipu Kuu ni Katiba lakini inamnufaisha unadhani atajitumbua bila ya sisi wananchi kuungana na kumlazimisha?
Kabla ya kudai katiba mpya jiulize kwanza ,kwenye katiba tuliyo nayo ni ibara gani inayoruhusu watu wale rushwa, wawe wazembe ofisini, wasaini mikataba ya hovyo, ni ibara gani ???

Hata ikija katiba mpya ,watu hawawezi kueshimu makaratasi ,ni lazima awepo kiongozi wa kuwachukulia hatua wanaokosea.


Hata tukiwa na katiba mpya kama kiongozi wa juu ni mla rushwa hamna kitakachotokea...

Ni bora watanzania wakajikita kutafuta MTU makini( kama ccm walivyofanya uchaguzi huu) kila unapofika uchaguzi mpya. Na siyo kukalia maigizo, ukurupukaji, upuuzi, unafiki, na ushabiki wa kuchukua watu waliokatwa kwenye vyama vyao kama chadema walivyofanya uchaguzi mkuu uliopita...
 
Kabla ya kudai katiba mpya jiulize kwanza ,kwenye katiba tuliyo nayo ni ibara gani inayoruhusu watu wale rushwa, wawe wazembe ofisini, wasaini mikataba ya hovyo, ni ibara gani ???

Hata ikija katiba mpya ,watu hawawezi kueshimu makaratasi ,ni lazima awepo kiongozi wa kuwachukulia hatua wanaokosea.


Hata tukiwa na katiba mpya kama kiongozi wa juu ni mla rushwa hamna kitakachotokea...

Ni bora watanzania wakajikita kutafuta MTU makini( kama ccm walivyofanya uchaguzi huu) kila unapofika uchaguzi mpya. Na siyo kukalia maigizo, ukurupukaji, upuuzi, unafiki, na ushabiki wa kuchukua watu waliokatwa kwenye vyama vyao kama chadema walivyofanya uchaguzi mkuu uliopita...

Mzee lazima uwekwe mfumo na sheria madhubuti (katiba). Hatuwezi kutegemea mtu. Pata picha mfano alivyoondoka mwalimu kama angeacha katiba nzuri leo tungekuwa tunahangaika na nambo ya maana na sio majipu.
 
Mzee lazima uwekwe mfumo na sheria madhubuti (katiba). Hatuwezi kutegemea mtu. Pata picha mfano alivyoondoka mwalimu kama angeacha katiba nzuri leo tungekuwa tunahangaika na nambo ya maana na sio majipu.
Taja sehemu kwenye katiba hii inayowaruhusu watu wafanye ya hovyo ikiwemo kuiba
 
Kabla ya kudai katiba mpya jiulize kwanza ,kwenye katiba tuliyo nayo ni ibara gani inayoruhusu watu wale rushwa, wawe wazembe ofisini, wasaini mikataba ya hovyo, ni ibara gani ???

Hata ikija katiba mpya ,watu hawawezi kueshimu makaratasi ,ni lazima awepo kiongozi wa kuwachukulia hatua wanaokosea.


Hata tukiwa na katiba mpya kama kiongozi wa juu ni mla rushwa hamna kitakachotokea...

Ni bora watanzania wakajikita kutafuta MTU makini( kama ccm walivyofanya uchaguzi huu) kila unapofika uchaguzi mpya. Na siyo kukalia maigizo, ukurupukaji, upuuzi, unafiki, na ushabiki wa kuchukua watu waliokatwa kwenye vyama vyao kama chadema walivyofanya uchaguzi mkuu uliopita...


Tunataka katiba kama ile ya Brazil raisi ukiboronga tunakukamata tunapeleka mahakamani, itamfanya raisi aliye madarakani aongoze kwa uadilifu ili asije akafungwa
 
Mzee lazima uwekwe mfumo na sheria madhubuti (katiba). Hatuwezi kutegemea mtu. Pata picha mfano alivyoondoka mwalimu kama angeacha katiba nzuri leo tungekuwa tunahangaika na nambo ya maana na sio majipu.

Umeongea point sana Mkuu. Salute yako nakupa.
 
Kabla ya kudai katiba mpya jiulize kwanza ,kwenye katiba tuliyo nayo ni ibara gani inayoruhusu watu wale rushwa, wawe wazembe ofisini, wasaini mikataba ya hovyo, ni ibara gani ???

Hata ikija katiba mpya ,watu hawawezi kueshimu makaratasi ,ni lazima awepo kiongozi wa kuwachukulia hatua wanaokosea.


Hata tukiwa na katiba mpya kama kiongozi wa juu ni mla rushwa hamna kitakachotokea...

Ni bora watanzania wakajikita kutafuta MTU makini( kama ccm walivyofanya uchaguzi huu) kila unapofika uchaguzi mpya. Na siyo kukalia maigizo, ukurupukaji, upuuzi, unafiki, na ushabiki wa kuchukua watu waliokatwa kwenye vyama vyao kama chadema walivyofanya uchaguzi mkuu uliopita...

Yaani mtu ndiye awe badala ya Katiba? akifa je?? ha ha ha.
 
tusipopata katiba mpya mchwa waliondani ya ccm watatafuna tena viwanda vipya ili Magu aonekane hakufanya kitu, Mzee Magu ni mtu safi mtetea wanyonge lakini li-chama lake sasa ndiko kunako CCM, angalia leo hii NMC, TRL hakuna kwa sababu wametafuna
 
Back
Top Bottom