Rais Kikwete kwa hili sikusamehi

Ringo Edmund

JF-Expert Member
May 10, 2010
4,879
1,125
Rais umekuwa mwepesi kuliko marais wote niliowahi kuwasikia hapa duniani. Kwanza nijuavyo Rais ni kiongozi na kiongozi ni lazima akae mbele ili aliongoze kundi mahali pa kuelekea.

Na kauli ya Rais najua ni ya mwisho, hatakiwi kukurupuka kuzungumza kwani ana washauri wa kutosha.

Kauli za Kikwete zenye utata.

1. Mimi ni mmoja wa wasiotaka DOWANS isilipwe, wewe kama rais unaungana na wananchi kulia nani wa kutusaidia?
Je unataka tufunge na kuomba ili Mungu atuondolee DOWANS?

Kwani ulikaa kimya muda mrefu tukawa tunakusubiri labda utatuokoa na hiki kikombe kichungu lakini kumbe na wewe huna msaada.

2. Uzio uliojengwa jangwani ubomolewe, ulipotoa hilo agizo nikawa nasubiri utekelezaji, lakini wapi, halmashauri nimesikia imegoma.

Sasa najiuliza je unajua uzito wa kauli yako kwa sasa kama rais na si kama Jakaya? Ni bora usiwe unazungumza rais wangu kwani sauti yako walio chini yako wameizoea mpaka sidhani kama wanakusikiliza tena.

3.Sijui kwa nini Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali zote zilizopo, hapo ndipo ulinichosha sana rais wangu. Uliomba kuwa rais wa Tanzania ili kiwe nini?

Nakuombea umalize miaka yako minne iliyobaki kwa amani ili tujipange upya ila kwa hayo sikusamehi.
 
Mkuu Ringo nilidhani kuna mengine...kumbe haya tu! Binafsi huyu bwana kuingia madarakani 2005 nilipiga moyo konde...kwamba nchi itakaa likizo kwa miaka 10 na probably ndicho tunachokiona sasa!
 
Sikutegemea jipya kwa jk tangu awali kwa kuwa namfahamu ni mtu wa mizaha, kujionesha, umaarufu, na hana mtazamo anao upigania katika uongozi popote alipowahi shika.
 
Huu urais wake ni wa Hisani...ni km mchezo wa bahati nasibu ambao mshindi hakutaraji afanyie nini ushindi huo
 
rais umekuwa mwepesi kuliko marais wote niliowahi kuwasikia hapa duniani.kwanza nijuavyo rais ni kiongozi na kiongozi ni lazima akae mbele ili aliongoze kundi mahali pa kuelekea.na kauli ya rais najua ni ya mwisho,hatakiwi kukurupuka kuzungumza kwani ana washauri wa kutosha.
kauli za kikwete zenye utata.
1.mimi ni mmojawapo wasiotaka dowans ilipwe.
..wewe kama rais unaungana na wananchi kulia nani wa kutusaidia?je unataka tufunge na kuomba ili mungu atuondolee dowans?kwani ulikaa kimya muda mrefu tukawa tunakusubiri labda utatuokoa na hiki kikombe kichungu lakini kumbe na wewe huna msaada.
2.uzio uliojengwa jangwani ubomolewe.
..ulipotoa hilo agizo nikawa nasubiri utekelezaji.lakini wapi halmashauri nimesikia imegoma.sasa najiuliza je unajua uzito wa kauli yako kwa sasa kama rais na si kama jakaya?ni bora usiwe unazungumze rais wangu kwani sauti yako walio chini yako wameizoea mpaka sidhani kama wanakusikiliza tena.
3.sijui kwanini tanzania ni masikini pamoja na rasilimali zote zilizopo.
..hapo ndipo ulinichosha sana rais wangu,uliomba kuwa rais wa tanzania ili kiwqe nini?nakuombea umalize miaka yako minne iliyobaki kwa amani ili tujipange upya ila kwa hayo sikusamehi.
Duh! Ndg yangu umenizidishia machungu. Kila kukicha ninaposoma mada za namna hi nazidi kuchoka. Halafu kuna watu wanadhubutu kumtetetea. Eti kafanya mazuri. Unafiki mtupu na cfaham ni nani wa kutusaidia hili ikiwa kama kiongozi wetu hawezi. Sasa anafanya nini madaratjani? Anyway, tuzidi kuvumilia, ila mpaka lini. Ni nchi pee Afr Mash ambayo kila kitu kimepanda bei. Angalieni bei ya mafuta ilivyo juu. Watanzania wote tujipe pole kwa yote haya, hasa kwa kushindwa kusimamia kile anachosema. Na kushindwa kukemea mafisadi anaowalinda na kuwapigania!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom