Rais Kikwete ateua wakuu wapya wa mikoa

Leo Mh. Raisi wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania ameteua waku wa mikoa na kuwapandisha hadhi baadhi ya wakuu wa wilaya kuwa wakuu wa Mikoa. Mmoja wa wateule hao ni Mh. Eng. Stela Manyanya (MB). Mimi hapa ndipo ninapo hitaji ufafanuzi, hivi ni kwa nini Mbunge ateuliwe tena kuwa Mkuu wa Mkoa?? Najua huyu si wa kwanza kuna wengi walisha wahi kuwa wabunge na wakuu wa mikoa. Hapa tatizo ni nini? Je hatuna watendaji wakutosha serikalini au popote pale wasio kuwa wabunge au tatizo ni nini?? Tafadhali naomba kusaidiwa.

Nawasilisha,
Ni moja ya mbinu za CCM kuwapumbaza wabunge wao wenye misimamo mikali ingawa kwetu sisi wanainchi haina maana na ni kubana nafasi kwa watanzania wengine wenye uwezo.
 
Hakuna jipya hapo.Naona ameamua kudhirishia uma na wasomi kuwa ushkaji kwake ni kipaumbele kwa kumpeleka Sadiki kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam
 
big up mr prezident uteuzi wako umetukuka atakaye kukosoa ashindwe na alegee na baada ya hapo wote wapeleke semina elekezi ili wasije kuchemka big uop!!!!
 
sidhani ka atarudi tena bungeni 2015,aangalie yaliyomkuta Abluazizi na mwenzie mama mbega
 
Tatizo lenu bwana mnakomalia ishu hata hazina msingi wowowte sasa kuna ubaya gani mbunge kuwa mkuu wa mkoaacheni wivu wa kike au kwakuwa ni mwanamke mwenzenu kapewa shavu!!!
 
suluhu ya huu upuuzi unaondelea ni kuandika katiba mpya tuu itakayomwondolea rais hayo mamlaka ya teuzi..
 
Hakuna jipya kwakweli, ni wale wale maswahiba. Tena waliokataliwa na wananchi, just imagne Joel Bendera, Mwantumu mahza. Haya na huyo manyanyaaa. Kweli rais wa magamba ni sikio la kufa.
 
Vipi Lau Masha na Batilda Buriani ndo kawatosa jumla?au atawapa ubunge viti maalumu kuna nafasi 7 zimebaki za ubunge wa kuteuliwa
 
Mmoja wa wateule hao ni Mh. Eng. Stela Manyanya (MB). Mimi hapa ndipo ninapo hitaji ufafanuzi, hivi ni kwa nini Mbunge ateuliwe tena kuwa Mkuu wa Mkoa??

hofu ya ma-RC na ma-DC kutumika na kundi/mtu fulani kuelekea uchaguzi 2015 ndiko kulikopelekea kuchelewa kutangazwa na hata ya Mbunge kuwa RC, CCM hawaaminiani tena
 
Tafsiri ya haya yote ni UZUSHI tu!!!
Mbunge ni mwakilishi wa Wananchi dhidi ya Serikali,
Na mkuu wa mkoa ni mwakilishi wa Raisi (May be dhidi ya Wananchi)
Sasa mtu mmoja kushika hivi vyeo viwili ni kuchanganyana tu,
Nashindwa kuelewa huyo mchaguaji alifikiria nini.
Tukisema tunaambiwa tuna gubu,
Au ni wafuasi wa chama flani,
but huyu jamaa anatuzingua kwa kweli!!
 
Mkuu wa wilaya kinondoni vp? Au kwa vile wilaya hiyo imetoa wabunge wa upinzani wawili?

Hata mie nashangaa huyu kijana wa Kinondoni Rugimbana ni mchapa kazi mzuri aliyestahili kupanda cheo badala yake wanapandishwa wakina Gallawa!! Jakaya acha mambo ya kuwapa vyeo masharobaro bila kuangalia vigezo vya uwezo, haya ndiomambo yanayokupunguzia hadhi machoni pa wananchi hata kama unajifanya hujali.!!Watu wa Mbeya watafanya sherehe kwa kuondolewa mzigo huo wa Mwakipesile, sasa hata muungwana akienda hawatampopoa na mawe!!
 
Back
Top Bottom