Rais Kikwete anavunja Baraza la Mawaziri lini?

baharia Ar

JF-Expert Member
Dec 1, 2013
837
314
Wakuu nashindwa kuelewa nini mantiki ya rais wangu kuto kulivunja baraza la mawaziri, tunamaliza wiki sasa tangu kampen ianze mawaziri wanatumia nafasi za uwaziri wao kuomba ubunge na wengine wanatumia uwaziri wao kuombea u rais. Na bunge halijavunjwa mpaka sasa licha ya ahadi Kuwa litavunjwa tarehe 20/8/2015 lakin mpaka sasa wabunge wanautumia ubunge wao kuusaka ubunge hivi nchi hii ninani katurogaaa

1) Muda wa kushika madaraka ya Waziri na Naibu waziri utaanza tarehe atakapoteuliwa kushika madaraka hayo.

(2) Kiti cha waziri au Naibu Waziri kitakuwa wazi litokeapo lo lote kati ya mambo yafuatayo:-

(a) Endapo mwenye madaraka atajiuzulu au kufariki dunia;

(b) Ikiwa mwenye madaraka hayo atakoma kuwa Mbunge kwa sababu yoyote isiyohusika na kuvunjwa kwa Bunge;

(c) Ikiwa Rais atafuta uteuzi na kumuondoa kazini mwenye madaraka hayo;

(d) Iwapo atachaguliwa kuwa Spika;

(e) Iwapo Waziri Mkuu atajiuzulu au kiti chake kikiwa wazi kwa sababu nyingine yoyote;

(f) Ukiwadia wakati wa Rais mteule kushika madaraka ya rais basi mara tu kabla rais mteule hajashika madaraka hayo;

(g) Iwapo Baraza la Maadili linatoa uamuzi unaothibitisha kwamba amevunja Sheria ya maadili ya viongozi wa Umma.
 
#UKAWA imewachanganya masisiem kama wale wajenzi wa mnara wa babeli walipoanza kupishana lugha .
Ccm wajiandae kisakolojia kuwa wapinzani mwaka huu Jk amesahau hata kuvunja baraza la mawaziri chezea UKAWA.wewe
 
jamani muwe mnajaribu kusoma, bunge lilishavunjwa kwa mujibuwa tangazo la serikali katika gazeti la serikali.

Gazeti gani ?ilikuwa lini?mbona Magufuli anazunguka kama waziri wa ujenzi ?
 
baharia Ar

Nakwambia hili la baraza la mawaziri kutokuvunjwa nahisi ni kwamba kuna kitu kinachoendelea..........haikubaliki hata kidogo kodi ya Wananchi iendelee kutumiwa kuwalipa mishahara watu ambao inajulikana kabisa muda wao umeshakatika

Ila Mi naweza kusema ya kwamba kuna janja anaeleza mkwe......re lakini safari hii WATAISOMA NAMBA•••••••••••••••!
 
Last edited by a moderator:
Akiwa ana livunja sijui pinda atamuangaliaje magufuli,makamba na asha rose,mzee pinda nilimuona juzi,yani kanyong'onyea kweli,eti kinana ndo kipimo chao cha maadili,
 
hapa hoja iliopo mezani ni kuvunjwa baraza la mawaziri na sio kuvunjwa kwa bunge

bunge likivunjwa automatically kunapaswa baraza la mawaziri kuvunjwa maana kunakuwa hakuna mwenye sifa ya kuwa waziri, tunashuhudia mwendelezo wa dharau za watawala.
 
Gazeti gani ?ilikuwa lini?mbona Magufuli anazunguka kama waziri wa ujenzi ?

Ata mimi hapa sikumuelewa magufuli alitoa amri akiwa kama waziri sasa sijajua kama baraza limevunjwa uyu mtu alikengeuka au vipi? Na sheria inasemaje ktk hili
 
bunge likivunjwa automatically kunapaswa baraza la mawaziri kuvunjwa maana kunakuwa hakuna mwenye sifa ya kuwa waziri, tunashuhudia mwendelezo wa dharau za watawala.

Hii ni kwa mujibu wa katiba ama ni mawazo yako?
 
Pengine imeonekana kuwa endapo baraza lingevunjwa, basi wengi wangehamia upande wa pili. Inaweza kuwa ni sababu ya kisiasa pia. Mtazamo wangu.
 
Back
Top Bottom