Rais Kikwete amteua Bibi Mwanahamisi Omari Kitogo kuwa msaidizi wa Rais katika Huduma za Jamii

CV yake ni muhimu iwekwe humu ili tunue kama kastahili maana anaweza kuwa kuwe kwenye kukadiria ujenzi pengine alipotea njia tu.
 
Hivi hiyo kazi aliyokuwa anaifanya (ukadiriaji majengo) na hiyo mpya ya huduma za jamii mbona naona kama hazifanani? Au ndo kusema atajifunzia huko huko ofisini? Labda mimi ndo nitakuwa sielewi hapo!

unajua hiyo kazi aliyopewa ni jamii...huelewi nini hapo au una miaka 12
 
Tusubiri tuone Hollande wa Ufaransa atateua mawaziri wangapi.
Tanzania tumelogwa.
 
hiyo ni govt/private partnership.hivi naibu waziri katiba na sheria jina lake nani?kitu kimetulia balaa
 
dah!....

classmate hongera sana....!

ingawa napata shida kidogo kwamba ametumia base ipi kukupa hiyo kazi....!

hongera sana qs!
 
JK bana, haishi vihoja, Ukadiriaji majengo na huduma za jamii wapi na wapi? COWI (a private company) na mambo ya huduma za jamii (Government business) wapi na wapi? Au ndio anamsogeza karibu, isiwe anawasumbua usalama wa taifa-ccm, kumuescoti anapokuwa anatoka ikulu kwenda kupasha misuli....
 
mitanganyika ina wivu wa kike

nilivyomwelewa power ni kuwa nafasi aliyopewa haina uhusiano wa moja kwa moja na qualifications zake-quantity surveyor. Nilitegemea mteule awe mtu aliyesoma mambo ya ustawi wa jamii. Hata hivyo nahisi anaweza kutimiza malengo yake katika nafasi hiyo mpya ikiwa ni pamoja na kuinua kipato chake!!
 
hali ya uchumi ni mbaya, waziri mkuu alikiri serikali haina fedha sasa hawa manaibu waziri wawili kwenye baadhi ya wizara, bado tena ameteua wabunge wapya,leo tena ameteua msaidizi wake kwenye maswara ya jamii hawa wote watapewa ma vx mapya.
 
Kweli ujinga ni sawa na ukimwi, ukiupata ujue maisha yako kwishney! House girl katoka wapi kwenye mada hii?

Unaujua Ukimwi wewe..................mbona watu wagonjwa na wanadunda tu mjinga wewe mnyanyapaaaaji mkubwa kwa wenye Ukimwi watu tunawapa moyo waishi muda mrefu we unasema maisha yao kwishney.
 
Jukumu lake ni kuwajibika kwa Watanzania wenye matatizo mbalimbali wenye shida ya kumuona Rais kwa utatuzi wa matatizo yao na kwa pale Ikulu wana siku zao maalumu za kuwasikiliza wananchi wenye matatizo mbalimbali; mimi niliwahi enda pale nikiwa na tatizo langu ambalo nilihangaika ngazi zote hata nikaamua kumpandia Mukulu; reception nkaunganishwa na Msaidizi wa masuala ya Kijamii ambaye alikua Mtawa akanisikiliza naye akaniunganisha kwa msaidizi wa mambo ya kisheria kwa hakika alinisaidia na likatatuliwa
 
Hivi huo nao uteuzi wa ngazi ya Rais? Kwa nini portifolio hizo zisiwe zimeainishwa bayana kisha Utumishi na Hazina wakafanya kazi yao? Hivi huyu jamaa vipi, mi huwa simuelewi kabisa
 
Naona akina mwanahamisi, mwanahawa, mwajuma, mwadawa, siajabu, sikujua......ndo wakati wao huu.

Kidawa, somoe, mwanshamba, sikitu, mwanamkasi, mwashani, mwazanije, havijawa, mwanakilanga, mwafumbo, havijawa, mwapombe, mwamvua, mwagesti, mwauwani, mwaija, biti haji, biti mrisho, nk nk nk nk
 
Kikwete ana karama (na uwezo) wa kuudhi mno. By the time of his miserable departure atakuwa ametufikisha kwenye extreme-ends.
 
sijui na mimi huku petrinamwana huku niliko ataniteua au mpaka niwe mwanapetrina akiniteuawa sijui itakuwaje segere yake kijiji kizima kitajua nimeteuliwa baada ya dakika ya kwanza naona wenye ngekewa zao wanajimwanga
 
Back
Top Bottom