nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Na Rachel Balama
RAIS Jakaya Kikwete, jana ameanza ziara ya kidola siku nne nchini Afrika Kusini ambayo ni ya kwanza kufanywa na Rais wa Tanzania nchini humo.Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, inasema ziara hiyo ya kihistoria imetokana na mwaliko wa Rais Jacob Zuma wa nchi hiyo ambaye utawala wake umekuwa na uhusiano mzuri na Tanzania tangu aliposhika madaraka ya kuongoza Taifa hilo.
Rais Kikwete ambaye ameongozana na ujumbe wake akiwemo mkewe Mama Salma, waliondoka nchini jana mchana kwenda nchini humo katika Jiji la Pretoria.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa, pamoja na marais waliotangulia nchini Tanzania, waliwahi kutembelea nchini humo kwa shughuli mbalimbali lakini hakuna Rais wa Tanzania ambaye aliwahi kualikwa kwa ziara rasmi ya kiserikali au ya kidola tangu nchi hiyo iingie katika mfumo wa demokrasia mwaka 1994.
Rais Kikwete pia atafanya mazungumzo ya kiserikali Rais Zuma, kutiliana saini mikataba ya makubaliano katika nyanja mbalimbali, kufanya mkutano na waandishi wa habari na kutembelea Uwanja wa Uhuru akiwa na mwenyeji wake.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa, viongozi hao pia watakula chakula cha mchana na wafanyabiashara wa Tanzania, Afrika Kusini na kufanya mazungumzo ya pamoja ili kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi kati ya nchi hizo.
Rais Zuma ataandaa dhima ya kitaifa kwa ajili ya Rais Kikwete na ujumbe wake kwatika nyumba ya wageni nchini humo.
Julai 20 mwaka huu, Rais Kikwete na ujumbe wake watakwenda Cape Town nchini humo ambapo watatembelea kisiwa cha wapigania uhuru wa Afrika Kusini ambao walifungwa kwa miaka mingi na Makaburu akiwemo Rais mstaafu Bw. Nelson Mandela kinachoitwa Robben.
Rais Kikwete na ujumbe wake, watarejea nchini Julai 21 mwaka huu
RAIS Jakaya Kikwete, jana ameanza ziara ya kidola siku nne nchini Afrika Kusini ambayo ni ya kwanza kufanywa na Rais wa Tanzania nchini humo.Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, inasema ziara hiyo ya kihistoria imetokana na mwaliko wa Rais Jacob Zuma wa nchi hiyo ambaye utawala wake umekuwa na uhusiano mzuri na Tanzania tangu aliposhika madaraka ya kuongoza Taifa hilo.
Rais Kikwete ambaye ameongozana na ujumbe wake akiwemo mkewe Mama Salma, waliondoka nchini jana mchana kwenda nchini humo katika Jiji la Pretoria.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa, pamoja na marais waliotangulia nchini Tanzania, waliwahi kutembelea nchini humo kwa shughuli mbalimbali lakini hakuna Rais wa Tanzania ambaye aliwahi kualikwa kwa ziara rasmi ya kiserikali au ya kidola tangu nchi hiyo iingie katika mfumo wa demokrasia mwaka 1994.
Rais Kikwete pia atafanya mazungumzo ya kiserikali Rais Zuma, kutiliana saini mikataba ya makubaliano katika nyanja mbalimbali, kufanya mkutano na waandishi wa habari na kutembelea Uwanja wa Uhuru akiwa na mwenyeji wake.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa, viongozi hao pia watakula chakula cha mchana na wafanyabiashara wa Tanzania, Afrika Kusini na kufanya mazungumzo ya pamoja ili kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi kati ya nchi hizo.
Rais Zuma ataandaa dhima ya kitaifa kwa ajili ya Rais Kikwete na ujumbe wake kwatika nyumba ya wageni nchini humo.
Julai 20 mwaka huu, Rais Kikwete na ujumbe wake watakwenda Cape Town nchini humo ambapo watatembelea kisiwa cha wapigania uhuru wa Afrika Kusini ambao walifungwa kwa miaka mingi na Makaburu akiwemo Rais mstaafu Bw. Nelson Mandela kinachoitwa Robben.
Rais Kikwete na ujumbe wake, watarejea nchini Julai 21 mwaka huu