nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
March 11th, 2011
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete mchana wa leo, Ijumaa, Machi 11, 2011, amerejea nyumbani kutoka kwenye ziara ya kikazi mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Kikwete aliondoka Jumatano wiki hii kwenda Ethiopia ili kujiunga na marais wenzake wa Afrika ambao wamepewa jukumu ya kutafuta suluhu katika mgogoro wa kisiasa wa nchi ya Afrika Magharibi ya Ivory Coast.
Mjini Addis Ababa, Rais Kikwete alijiunga na marais kutoka Afrika Kusini, Chad, Mauritania na Burkina Faso kuendelea na jitihada za kutafuta jinsi ya kurejesha amani na demokrasia katika Ivory Coast.
Kundi hilo la marais wa Afrika lilipewa jukumu hilo na Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika (AU) katika kikao chake cha Januari, mwaka huu, mjini hapo hapo Addis Ababa.
Mzozo wa Ivory Coast ulilipuka kufuatia matokeo ya raundi ya pili ya Uchaguzi Mkuu wa Rais nchini humo Novemba 28, mwaka jana, 2010.
Katika matokeo hayo, Tume ya Uchaguzi ya Ivory Coast ilimtangaza aliyepata kuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Alassane Quattara kuwa mshindi.
Lakini siku nne baadaye, Baraza la Katiba ya nchi hiyo lilibatilisha matokeo hayo kwa kufuata matokeo ya kura 600,000 katika majimbo saba ya kaskazini mwa nchi ambako ndiko ngome ya Mheshimiwa Quattara. Badala yake, Baraza hilo lilimtangaza aliyekuwa anatetea kiti chake, Mheshimiwa Laurent Gbagbo kuwa mshindi.
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
11Machi, 2011
Rais Kikwete aliondoka Jumatano wiki hii kwenda Ethiopia ili kujiunga na marais wenzake wa Afrika ambao wamepewa jukumu ya kutafuta suluhu katika mgogoro wa kisiasa wa nchi ya Afrika Magharibi ya Ivory Coast.
Mjini Addis Ababa, Rais Kikwete alijiunga na marais kutoka Afrika Kusini, Chad, Mauritania na Burkina Faso kuendelea na jitihada za kutafuta jinsi ya kurejesha amani na demokrasia katika Ivory Coast.
Kundi hilo la marais wa Afrika lilipewa jukumu hilo na Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika (AU) katika kikao chake cha Januari, mwaka huu, mjini hapo hapo Addis Ababa.
Mzozo wa Ivory Coast ulilipuka kufuatia matokeo ya raundi ya pili ya Uchaguzi Mkuu wa Rais nchini humo Novemba 28, mwaka jana, 2010.
Katika matokeo hayo, Tume ya Uchaguzi ya Ivory Coast ilimtangaza aliyepata kuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Alassane Quattara kuwa mshindi.
Lakini siku nne baadaye, Baraza la Katiba ya nchi hiyo lilibatilisha matokeo hayo kwa kufuata matokeo ya kura 600,000 katika majimbo saba ya kaskazini mwa nchi ambako ndiko ngome ya Mheshimiwa Quattara. Badala yake, Baraza hilo lilimtangaza aliyekuwa anatetea kiti chake, Mheshimiwa Laurent Gbagbo kuwa mshindi.
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
11Machi, 2011