Bundewe
JF-Expert Member
- Jun 14, 2011
- 400
- 141
Takwimu zinaonesha kwamba Rais wetu ameshafanya safari 322 katika kipindi cha miaka 6 ya utawala wake. Hii ni wastani wa Safari 53.6 kwa mwaka. endapo tutachukulia wastani wa kuspend siku 3 tu kwa kila safari moja, kiongozi wetu atakua ameishi nje ya nchi yake kwa kipindi cha jumla ya siku 966 tangu aingie madarakani. Huu ni wastani tu ingawa natambua kwamba zipo safari ambayo amespend zaidi ya wiki nzima hasa zile za Marekani na Ulaya. Kipindi cha siku 966 ni sawa na miaka 2 na kama miezi nane hivi kipindi ambacho kinakaribia nusu ya kipindi chake alichokwishakaa madarakani.
Endapo kila safari moja ambayo huambatana na ujumbe mzito, itagharimu Tshs. 300,000,000/- Mpaka sasa tayari kiasi cha Tshs. 98.8 Bilioni zimekwishatumika kugharamia safari hizo.
Endapo gharama za ujenzi wa barabara kiwango cha lami ni wastani wa Tshs. 700,000,000/- kwa kilomita, fedha hizo zingejenga kilomita 141 za lami, Hivyo kwa mfano barabara ya Nzega - Tabora (Km 116) ingekamilika kiwango cha lami na chenji ingebaki, nk. Endapo gharama za kujenga chumba kimoja cha darasa ni Tshs. 12,000,000/-, fedha hizi zingetosha kujenga vyumba 8233 vya madarasa, nakadhalika.
Sina maana kwamba Rais asisafiri, isipokuwa angeweza kupunguza safari hizo, hali ya kifedha ya serikali ingeboreka bila shaka. Hatuoni wimbi la viongozi wenzie wakitutembelea kwa kasi ambayo yeye anawatembelea. Vilevile ujumbe anaoambatana nao ni mzigo mkubwa kwa Taifa. Jambo hili limepigiwa kelele mara nyingi lakini tunaambiwa kwamba Rais anakwenda kuhemea, mpaka sasa hatujaambiwa ni kiasi gani kimepatikana kutokana na kuhemea kwake badala yake tunaona Serikali ikizidi kudhoofika kifedha kiasi cha kushindwa hata kulipa mishahara kwa watumishi wake.
Nawasilisha.
Endapo kila safari moja ambayo huambatana na ujumbe mzito, itagharimu Tshs. 300,000,000/- Mpaka sasa tayari kiasi cha Tshs. 98.8 Bilioni zimekwishatumika kugharamia safari hizo.
Endapo gharama za ujenzi wa barabara kiwango cha lami ni wastani wa Tshs. 700,000,000/- kwa kilomita, fedha hizo zingejenga kilomita 141 za lami, Hivyo kwa mfano barabara ya Nzega - Tabora (Km 116) ingekamilika kiwango cha lami na chenji ingebaki, nk. Endapo gharama za kujenga chumba kimoja cha darasa ni Tshs. 12,000,000/-, fedha hizi zingetosha kujenga vyumba 8233 vya madarasa, nakadhalika.
Sina maana kwamba Rais asisafiri, isipokuwa angeweza kupunguza safari hizo, hali ya kifedha ya serikali ingeboreka bila shaka. Hatuoni wimbi la viongozi wenzie wakitutembelea kwa kasi ambayo yeye anawatembelea. Vilevile ujumbe anaoambatana nao ni mzigo mkubwa kwa Taifa. Jambo hili limepigiwa kelele mara nyingi lakini tunaambiwa kwamba Rais anakwenda kuhemea, mpaka sasa hatujaambiwa ni kiasi gani kimepatikana kutokana na kuhemea kwake badala yake tunaona Serikali ikizidi kudhoofika kifedha kiasi cha kushindwa hata kulipa mishahara kwa watumishi wake.
Nawasilisha.