Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
WANAJAMVI WENZANGU:
Kuna hii stori katika Raia Mwema le ukurasa wa 3 ambayo naona vyema ni-share nayni, na hasa iwapo kama kuna mtu analifahamu tukio hili na ni nani huyo kigogo wa UVCCM.
Bastola ya kigogo UVCCM yatoiboa tumbo mwanafunzi wa CBE.
Na Mwandishi wetu.
Bastola ya kigogo wa makao makuu ya UVCCM mjini Dar es Salaam imemjeruhi tumboni mwanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE), Raia Mwwema imeelezwa.
Habari za uhakika zinaeleza kwamba mtu mmoja anayetajwa kuwa dereva wa kigogo huyo, alikwaruzana na mwanafunzi huyo Emmanuel James (30) eneo la Sinza Mugabe karibu na Hoteli ya City Style.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, wakati wa tukio hilo kigogo huyo hakuwepo kwenye gari ambalo aliacha bastola yake na dereva aliitumia kuwafyatulia risasi vijana waliomhoji sababu ya kuwamwagia maji machafu.
Baada ya vijana hao kupiga kelele za kwa nini wamemwagiwa maji machafu, dereva huyo alipaki gari na kuanza kuwafokea vijana hao na walipojibizana naye alifyatua risasi mbili hewani na baadaye moja kumlenga tumboni Emmanuel James, kinaeleza chanzo cha habari.
Tukio hilo ambali limertokea saa saba usiku wa Novemba 30 2011 limeibua maswali mengi baada ya kuwapo taarifa za kutokamatwa kwa wahusika wala silaha iliyotumika katika tukio hilo.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa (kipolisi) Kinondoni, Camillus Wambura, hakuwa katika nafasi ya kuzungumzia tukio hilo kutokana na kuwa katika majukumu mengine ya kitaifa.
Juhudi za kumpata Emmanuel kujua hali yake na kueleza kuhusiana na tukio hilo hazikuweza kufanikiwa wiki hii, huku wahusika wakielezwa kutamba kutochukuliwa hatua zozote.
Taarifa ya tukio hilo zimeripotiwa katika kituo cha polisi cha Urafiki Dar es Salaam ambako imeelezwa kwamba hadi sasa wamekuwa wazito kuwahoji wahusika na kufanya uchunguzi zaidi kuhusu silaha iliyotumika.