Prof. Tibaijuka amjibu Jussa; adai Jussa amepotosha Wazanzibari

Btw ingawa kuna masuali yangu mengi umekwepa kuyajibu mtu mzima wewe na msomi wetu wa "kitanzania bara" nkugusie hili la mafuta na gesi ili ndo ujue kama SMT ni wezi na dhulma na wamekalia kula Mali za wazenji, kama watu wanavojidai suala la mafuta na gesi yameingizwa katika muungano, tangu ipatikane gesi ya songosongo mbona hakuna mgao wa mapato yakeee?!!! Yakhe waweza tupa jibu au znz ikilima bangi itakuw ya znz lkn mafuta ni ya SMT? Mifano yako chengu halafu inakurudia mwenyeo, Bobuk hujanipatia jibu la Almasi inapatikana wapi na je BIG BROTHER hatakiwi kuitumia iyo?

Hivi wewe Chilubi unaposoma majibu yangu akili zako unakuwa umeweka wapi? tatizo lako unafikiri Ki-Makunduchi ni sawa na Kiswahili!

Ngoja nianze na suala la Almasi ambalo nilishakujibu. Almasi inapatikana Tanganyika specifically Shinyanga. Big brother anaitumia kwa maendeleo ya Tanganyika, kwasababu madini sio suala muungano. Kama mnataka (Wa-ZNZ) madini liwe suala la Muungano basi leteni hoja kwenye Bunge la JMT. Hiyo itakuwa right direction kuelekea SERIKALI MOJA maana polepole kila jambo litakuwa la Muungano.

Kuhusu gas ya songosongo, hivi unafikiri hiyo 4% mnayopewa kila mwezi na SMT mapato yake yanatoka wapi? Au unataka mfungiwe pipe la gas kutoka Songosongo hadi Unguja na Pemba ndiyo ujue kwamba mnapata mapato yanayo tokana na gas ya Songosongo? Tumia akili kidogo basi hata kama ni za Madrassa.
 
Ata kinyamwezi si kiswahili :D
Enhe nkuulize, umesema kama almasi tunataka iwe ya Muungano tuipeleke hoja bungeni, je masuala ya mafuta yalipelekwa baraza la wakilishi Zanzibar? Na kama hayakupelekwa je huoni kama yameingizwa kinyemela nyuma ya pazia? Hizo article of union zilizoongezwa zote hujui kama ni haram? Hujui kama mambo ya muungano kila upande una haki yake ya kuyajadili? Vile vile ukae utambue kuwa Tanganyika imekufa totally, hakuna hata serikali, na nfio maana wenye akili wameshtuka, wakaamua pawe na serikali 3 ili kila upande uwe na serikali yake!

Sijasikiapo Zanzibar ikipewa 4% inayotokana na songosongo!! Hebu nipe hesabu hasa, mana mi naona SMT inajukumu la kuipa Zanzibar mapato yake kila mwezi kutoka kila nyanja, gesi, mgao wa fedha kikawaida, misaada ya nje, budget ya Tanzania etc! Nipe exact source nipate details za mgao wa songosongo,,,,, kwani kuunganishiwa pipe ya gesi ndo kuonesha mgao ama kuonesha kuwa mnatuuzia?
 
Btw,,, Bobuk wewe kumbuka ile mfano ulontolea kuhusu kukutwa bangi na mafuta, lau kama ungesema kuwa , mafuta yameekwa katika muungano badala ya vile ulivosema wewe ningekuelewa, kwaiyo Zanzibar tukichimba tukapata dhahabu itabaki kuwa ya Zanzibar, au itakuwa ya Muungano?
 
Mimi bado nitaka kufahamu hivi wewe Chilubi una umri gani? na umesoma hadi chuo (read darasa la ngapi?). Unaishangaza uaposema 1+1 = 11 (LoL!).

Wakati mafuta na gas asilia yanaingizwa kwenye mambo ya Muungano yalijadiliwa na kupitoshwa na Bunge la JMT ambamo kuna wabunge kutoka ZNZ. Na hilo jambo kupata baraka wajumbe > 2/3 kutoka Tanganyika na > 2/3 kutoka ZNZ walikubali. Kama Wa-ZNZ wasingetaka liingie kwene muungano lisiingiengia kwani wabunge wa Tanganyika hata kama wote wangetaka halafu wa ZNZ wakakataaa basi lisingeingia. Unataka Wazanzibari mshirikishwe vipi?

Ndiyo almasi ikipatikana sasa hivi ZNZ ni ya Wazanzibari TU because madini sio suala la muungano. Mbona huelewi?!

4% mnayopewa kila mwezi na SMT ni jumla ya mapato yote inayopata SMT including, misaada, gas ya Songosongo etc. Kama unataka kufahamu gasi ya Songosongo inachangia kiasi gani kwenye 4% tembelewa website ya Bunge na tafuta book la budget ya SMT.

Hivi ni lini Shamuhuna na Prof Tibaijika wanatajiuzulu? Pia ni lini SMZ itatuma pingamiza UN dhidi ya JMT kuongezea EEZ?
 
Nataka kuweka hili wazi, nakerekwa sana na tabia ya baadhi ya watanzania wenzetu kutoka visiwani ambao wamepata bahati ya kusoma na kuishi nje ya nchi kuchochea maneno ya chokochoko ya kuchokoa Muungano. Sitaki kuhoji agenda yao lakini kiukweli wamenichosha mno. Wamesababisha hata baadhi ya watanzania kutoka bara kuwa na wakati mgumu wanapojaribu kuanzisha makazi visiwani (hasa Kisiwa cha Pemba). Tunaonekana kama maadui, na unaangaliwa kwa jicho la hasama kweli ikitokea umelazimisha kufanya maisha.

Hivi karibu Mhe. Jusa aliibua tuhuma nzito ndani ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar na kuungwa mkono na wajumbe wengi kwa kile alichokiita, Wabara kukwapua ardhi ya Zanzibar. Na tuhuma hizi ni mfululizo wa maneno ya chini chini yanakuzwa na wazanzibar wachache hasa walio nje ya nchi wakijiita wanaharakati wa kuikomboa zanzibar dhidi ya wabara. Watu hawa wachache wameadhimia muungano uvunjike hata kesho ili Zanzibar iwe huru. Ndo maana sitashangaa Mtu kama Mhe. Justa kutoa tuhuma za aina ile ndani ya nchi yake. Imefika hatua watanzania tuwape wazanzibar wanachokihitaji....Uhuru wao maana tunaelekea kuchoka matusi na masimango.

Hili si sahihi, Tanzania ni moja na wengi wetu tumeikuta na kuzaliwa kwenye Tanzania hii. Inawezekana kuna mapungufu ya kimakubaliano lakini sidhani kama mapungufu hayo yanaenda hadi kwenye kubaguana na kunyimana hata maji. Mbona wapo wazanzibar wengi tunaishi nao vizuri huku bara na hatuwasikii wakilalamikia Muungano? Mi nadhani ipo haja nyie mnaoona mapungufu mrudi nchini na ikiwezekana mkafungue kesi ya kikatiba ili tujue moja kuwa wapo watu wameamua kupigania ukombozi wa nchi inayoitwa "Zanzibar".
 
Nataka kuweka hili wazi, nakerekwa sana na tabia ya baadhi ya watanzania wenzetu kutoka visiwani ambao wamepata bahati ya kusoma na kuishi nje ya nchi kuchochea maneno ya chokochoko ya kuchokoa Muungano. Sitaki kuhoji agenda yao lakini kiukweli wamenichosha mno. Wamesababisha hata baadhi ya watanzania kutoka bara kuwa na wakati mgumu wanapojaribu kuanzisha makazi visiwani (hasa Kisiwa cha Pemba). Tunaonekana kama maadui, na unaangaliwa kwa jicho la hasama kweli ikitokea umelazimisha kufanya maisha.

Hivi karibu Mhe. Jusa aliibua tuhuma nzito ndani ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar na kuungwa mkono na wajumbe wengi kwa kile alichokiita, Wabara kukwapua ardhi ya Zanzibar. Na tuhuma hizi ni mfululizo wa maneno ya chini chini yanakuzwa na wazanzibar wachache hasa walio nje ya nchi wakijiita wanaharakati wa kuikomboa zanzibar dhidi ya wabara. Watu hawa wachache wameadhimia muungano uvunjike hata kesho ili Zanzibar iwe huru. Ndo maana sitashangaa Mtu kama Mhe. Justa kutoa tuhuma za aina ile ndani ya nchi yake. Imefika hatua watanzania tuwape wazanzibar wanachokihitaji....Uhuru wao maana tunaelekea kuchoka matusi na masimango.

Hili si sahihi, Tanzania ni moja na wengi wetu tumeikuta na kuzaliwa kwenye Tanzania hii. Inawezekana kuna mapungufu ya kimakubaliano lakini sidhani kama mapungufu hayo yanaenda hadi kwenye kubaguana na kunyimana hata maji. Mbona wapo wazanzibar wengi tunaishi nao vizuri huku bara na hatuwasikii wakilalamikia Muungano? Mi nadhani ipo haja nyie mnaoona mapungufu mrudi nchini na ikiwezekana mkafungue kesi ya kikatiba ili tujue moja kuwa wapo watu wameamua kupigania ukombozi wa nchi inayoitwa "Zanzibar".
Mkuu wasikutiushe sana hawa watu ambao leo wamepoteza kabisa mwelekeo. Kuvunja muungano haiwezekani japo inawezekana kuwepo kwa serikali tatu.. Kuna Wazanzibara wengi kulikko Zanzibar yenyewe na ndio maana wanaogopa kuitisha kura za maoni (referundum) wakifahamu kwamba hawawezi kushinda maana kura nyingi za bara zitawamaliza. Na hakuna Mzanzibara hata mmoja anayekubali kuondolewa Utanzania wake arudi Zanzbiar, hata huyo Jussa maneno mengi tu ya kisiasa lakini mwoga wa kauli zake mwenyewe ikiwa kweli tutaamua kuuvunja Muungano.

Madai ya kutafuta kuchora ramani upya, sijui makubaliano ya mamlaka ya kiserikali na kadhalika wamepewa vya kutosha hawaridhiki kinyegemshindo, na wataendelea kudai hadi watuache uchi maana sijaona bunge lenye wawakilishi wengi kutoka sehemu mbili tofauti pasipo kufuata idadi ya wananchi wanaowawakilisha. Sijaona serikali mbili zilizoungana zikigawa madaraka na mamlaka ati kuleta uuwiano haya nayaona Tanzania kutokana na madai yasiyokwisha ya Wazanzibar. Waulize wanachangia kiasi gani ktk serikali ya muungano na wao huchukua kiasi gani hawataki kusema japokuwa wanapewa mara mbili ya mchango..Hivyo kinacholiliwa hapa ni MTUKULA, umaskini sio lazima uwe wa mali bali huanza na akili na maskini wa akili ni mbaya na hatari kuliko fukara. Jussa ni mmoja wao!
 
Bobuk mi sijasoma nna miaka 14 ndo maana nashindwa kufahamu unavoandika, kwanza sifahamu unapoandika neno "read" katika mabano sifahamu unamaanisha nini!

Pitia maelezo yako ya post za nyuma ndo utajua km we mwenyeo hufahamiki, huelezi kitu straight!

Hilo suala la mapato ya songo na mazagazaga mengine linatakiwa liwe 40% znz ilobaki tanganyika!

FYI suala la mafuta na gesi ya zanzibar limepitishwa kwa 2/3 ya bunge zima na sio 2/3 ya znz na 2/3 ya bara. Kwa hivyo wazenji wangeinua mikono na miguu yao wasingeweza kuwazidi wabunge wa bara! Hivyo basi jambo hilo limepitishwa kiharamu halina uhalali

Dotto umenena, tupeni Uhuru wetu kwani kuna tabu gani? Tukiubunja huu muungano ambao hata mkataba wake ume expire kutakua na hasara gani wakati serikali 2 ni kukaa na kujadili mambo kiungwana? Kwa mfano wazanzibara na watanganyika visiwani waruhusiwe kuendeleza shuhuli zao kama kawaida, kuna EAC, free movement tena patakua na kasoro gani? Kwanini wengine wameshikilia muungano ubaki kama bara haifaidiki na zenji? Mi nashangaa kweli kweli!!!
 
Mkandara, kwani Zanzibar walitaka idadi ya wabunge wawe sawa? Au walitaja kura ya jambo iwe kwa 2/3 from zenji alone na 2/3 from bongo alone?
Idadi ya wabunge tu basi watakuwa wamechemsha mana bongo kuna mikoa mingi na sehemu nyingi inayotaka kuwakilishwa!!
 
Back
Top Bottom