PRof. Mutakyahwa

Mzee wa Usafi

JF-Expert Member
Apr 16, 2008
644
292
Leo wanataaluma na wataalamu wa sayansi ya dunia (Earth Scientists-Geologists et al) tumemzika mwanataaluma mahiri Prof.Mutakyahwa. Prof.Muta ni mmoja wa wataalamu waliotoa mageo karibia wote walioko migodini na nje ya nchi ambayo ndo wanaaingizia mifuko ya hifadhi ya jamii mabilioni ya shilingi. Amesaidia kuongeza namba ya wahitimu wa shahada mbalimbali. Cha ajabu serikali nzima imeishia kwa Kanumba, TBC1 wameacha kutangaza mambo mengine isipokuwa maziko ya Kanumba....Je wazalishagi hawaonekani isipokuwa wasanii wa luninga tu, au kwakuwa Prof.Muta sio maarufu kwa wanasiasa.


Sisi wasome wachache tulioko Tanzania tunasema RIP Prof.Muta kazi yako na mchango kwa Taifa ni kubwa kuliko wasanii wa tasnia ya filamu. Tutakukumbuka daima kwa jinsi ulivyo saidia taifa hili....mara ya mwisho kukuona nilikupakiza kwa gari na tuliongea mengi mmojawapo ulisema ulipewa nafasi ya kufundisha nje ila ukaweka uzalendo mbele ukaamua kurudi nyumabani ili kuanzisha Geology department pale Mlimani.. Watawala hawaoni hilo isipokuwa umaarufu wao kwa kwenda kwa marehemu Kanumba.......daima tutakukumbuka
 
Wakongwe wa Geology wanazidi kwish tu
Dr Mnali, Dr Kapilima, Dr Msindai na Sasa Prof. Muta,

RIP Prof. Muta
 
Mungu ailaze mahala pema roho ya Prof Muta... nawasikitia waliobaki chuo watakosa mafundisho yake na furaha yake ya kufundisha
 
So sad, R.I.P Prof, kweli nilifurahia sana course zako, kwa wale wote waliosoma CoET uhandisi wa madini kamwe hawatamsahau.
 
Leo wanataaluma na wataalamu wa sayansi ya dunia (Earth Scientists-Geologists et al) tumemzika mwanataaluma mahiri Prof.Mutakyahwa. Prof.Muta ni mmoja wa wataalamu waliotoa mageo karibia wote walioko migodini na nje ya nchi ambayo ndo wanaaingizia mifuko ya hifadhi ya jamii mabilioni ya shilingi. Amesaidia kuongeza namba ya wahitimu wa shahada mbalimbali. Cha ajabu serikali nzima imeishia kwa Kanumba, TBC1 wameacha kutangaza mambo mengine isipokuwa maziko ya Kanumba....Je wazalishagi hawaonekani isipokuwa wasanii wa luninga tu, au kwakuwa Prof.Muta sio maarufu kwa wanasiasa.


Sisi wasome wachache tulioko Tanzania tunasema RIP Prof.Muta kazi yako na mchango kwa Taifa ni kubwa kuliko wasanii wa tasnia ya filamu. Tutakukumbuka daima kwa jinsi ulivyo saidia taifa hili....mara ya mwisho kukuona nilikupakiza kwa gari na tuliongea mengi mmojawapo ulisema ulipewa nafasi ya kufundisha nje ila ukaweka uzalendo mbele ukaamua kurudi nyumabani ili kuanzisha Geology department pale Mlimani.. Watawala hawaoni hilo isipokuwa umaarufu wao kwa kwenda kwa marehemu Kanumba.......daima tutakukumbuka

vipi kikwete alikuwepo?
 
Back
Top Bottom