Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 21 Oktoba, 2022



Mapendekezo 18 ya Ripoti yanasomwa na Prof. Rwekaza Mukandala
  1. Kikosi kazi kinapendekeza mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa iruhusiwe, pia mikutano ya ndani ya vyama hivyo
  2. Sheria ya vyama vya siasa ifanyiwe marekebisho
  3. Mfumo wa sasa wa kugawa ruzuku kwa vyama vya siasa uendelee, isipokuwa 10% ya fedha zinazotolewa sasa zitolewe kwa mgawanyo sawa kwa vyama vyote.
  4. Tume ya taifa ya Uchaguzi isilazimike kufuata amri ya yeyote, na utendaji wake uruhusiwe kuhojiwa mahakamani
  5. Wajumbe wa tume ya taifa ya uchaguzi wateuliwe na kamati inayoongozwa na jaji mkuu wa Tanzania, akisaidiwa na jaji mkuu wa Zanzibar. Pia, nafasi itangazwe, watu wafanyiwe usaili kisha majina yapelekwe kwa Rais kwa uteuzi
  6. Matokeo ya Rais jahojiwe Mahakamani
  7. Wasimamizi wa uchaguzi wazingatie sheria na maadili
  8. Tume ya taifa ya uchaguzi ipewe fedha kwa wakati
  9. Itungwe sheria kusimania shughuli za tume ya uchaguzi, pia iwepo sheria moja ya kusimamia chaguzi zote, maafisa wa uchaguzi wanaoengua wagombea bila sababu maalumu wawajibishwe
  10. Matumizi ya tehama kwenye uchaguzi yaboreshwe
  11. Sharti ya uwepo wa sera ya jinsia liwepo kwenye sheria za vyama vya siasa, pia ushiriki wa wanawake kwenye vyombo vya maamuzi isipungue 40%
  12. Sheria zinazokwamisha ushiriki wa wa watu wenye ulemavu kwenye siasa ziangaliwe upya
  13. Juhudi za ushirikishwaji wa vijana kwenye siasa ziongezwe
  14. Serikali iongeze utoaji wa elimu ya uraia, pia ifundishwe kwenye ngazi zote za elimu, pia mtaala wa elimu uzingatoe elimu ya uraia.
  15. Swala la rushwa litamkwe katika katiba ya nchi ili wananchi waelewe
  16. Kuanzishwe utaratibu wa mijadaa kila mwaka itakayohusisha viongozi wakubwa wa kitaifa na kisiasa ili kudumisha mshikamano, mahakama iwe ni mamlaka ya mwisho ya kuamua pindi maridhiano yanapokwama
  17. Wanahabari waunde chombo cha kusimamia wanahabari na vyombo vyao, vyombo vya umma vitoe muda sawa wa kutangaza habari za wagombea wa vyama vyote kwa usawa, uwepo mchakato wa wazi wa kuwajibisha vyombo vya habari badala ya kufungiwa pekee na mkurugenzi wa habari na mawasiliano
  18. Mchakato wa katiba mpya uendelee, hata hivyo mjadala wa kitaifa kuhusu katiba mpya uanze kabla ya kuanza kwa mchakato wa kuandika katiba mpya ili kujadili ajenda muhimu za muungano, mamkala ya Rais, Rushwa, tume ya uchaguzi n.k

Afadhali umeedit No18.

Ungeharibu thread.
 
Hapo ndipo tunapoona mapungufu ya waTanzania, suala hili silo la rais wala chama cha upinzani au tabaka fulani la wananchi.

Suala hili ni la waTanzania wote haitakiwi majority wakae wamewaachia ulingoni wapo rais na wapinzani.
Huu ni mchakato wa wanasiasa na sio watanzania. Sijasikia jambo litakalomsaidia mtanzania bali mawazo ya wanasiasa kutafuta namna bora ya kuendelea kula keki ya Taifa.
 
Tunakoelekea kuzuri.
rejoice.png
 
Tumpongeze sana Profesa Mkandala kwa kazi nzuri pamoja na kikosi kazi chake kwa ujumla; ila kwenye "nukuu" hiyo hapo, Profesa anapelekea na mimi nianzishe Chama changu cha Siasa, nikamate hela ya Serikali kama itakuwa imejisahau kwa kiwango hicho.

Kwani ni sababu zipi zilizopelekea hiyo 10% ikawa haigawiwi sawa kwa vyama vyote vya Siasa? Nitaanzisha chama changu muda siyo mrefu
Idadi ya wabunge kupitia chama husika hupelekea mganwanyo huo wa 10% uendeje.
 
Kuna kipi kipya kilikuwa hakijasemwa wakati wa kukusanya maoni ya Katiba mpya chini ya Jaji Warioba?

Kama kuna kipya ambacho mtu amekiona kwenye hiyo tume atuambie wenzake. Wasomi wetu wanatia aibu sana. Kama ni wasomi wa kweli si wangemwambia tu Rais maoni anayoyatafuta yako kwenye makabrasha ya Tume ya Warioba!!?

Cha ajabu hata Warioba naye alikubali kuhojiwa na hiyo Tume ya Mukandala. CCM watu wa ajabu sana.
 
  • Sheria zinazokwamisha ushiriki wa wa watu wenye ulemavu kwenye siasa ziangaliwe upya
Hawa watu wana nafasi zao special ambazo wamepewa kama kundi la watu maalumu.

Mimi ninachoweza kupendekeza kwenye kundi hili ni kwamba wanapokuwa wamepewa hizo nafasi zao (uwaziri kwa mfano), wawe wanabadilishana wao kwa wao tu na kwa kipindi cha miaka mitano. Tuseme kwa mfano, akimaliza mmoja miaka mitano, miaka mitano mingine anafuata mwingine na inapotokea kwa mfano dharula kwamba Baraza la Mawaziri limevunjwa (kwa sababu nyingine maalum tofauti na uchaguzi mkuu) au limefanyiwa marekebisho madogo, hawa watu wasiondolewe kwenye nafasi zao, na hivyo wasihusike na mabadiliko hayo; unless kama mtu mwenyewe alliyekuwa kwenye nafasi ya aina hiyo, awe amehusika kwa kiwango kikubwa sana katika kuchangia marekebisho hayo kufanyika

Zaidi ni kuwa napendekeza neno ULEMAVU lisitumike kwenye majina ya Wizara au Tasisi wanazotumika, isipokuwa litumike neno "MAHITAJI MAALUM" . Tusitume majina kama . "WIZARA YA....... NA WENYE ULEMAVU" bali tutumie "WIZARA YA....... NA WENYE MAHITAJI MAALUM"
 
Tume ya taifa ya Uchaguzi isilazimike kufuata amri ya yeyote, na utendaji wake uruhusiwe kuhojiwa mahakamani
 
nafasi itangazwe, watu wafanyiwe usaili kisha majina yapelekwe kwa Rais kwa uteuzi Hii hapana
 
Idadi ya wabunge kupitia chama husika hupelekea mganwanyo huo wa 10% uendeje.
Hapo ndipo sasa inabidi Profesa anirudishe tena kwenye Lecture Theatre za UDSM ili akanipige Lecture upya. Wewe nimekuelewa, ila yeye amenipoteza kabisa; anaanza kuni-prompt nianze kufanya investment kwenye siasa wakati sikuwa na mpango huo
 
SSH anapita mle mle katika njia za JK, Kwamba ruhusu demokrasia na wataongea sana tu na kadri wanavyoongea wanapimwa na hao wanao wasikiliza mwisho wa siku madhara ya siasa zao yanapunguzwa nguvu na ule uhuru wa wao kuongea.

Inataka moyo sana haswa kwa mwanasiasa kuwa na uwezo wa kuvumilia kile kinachosemwa na kukichukulia kama ni maneno ya kawaida na kuendelea na maisha kama vile hakuna kilichosemwa.
 
Serikali iongeze utoaji wa elimu ya uraia, pia ifundishwe kwenye ngazi zote za elimu, pia mtaala wa elimu uzingatoe elimu ya uraia.
Kwa mara ya kwanza kabisa, hii hoja nyingine ya muhimu sana imeibuliwa hapa. Mimi nitafurahi zaidi kama taasisi za elimu pamoja na wizara husika watalipatia priority zaidi swala hili kuliko lile jingine la kubadilisha lugha ya mtaala wa nchi nzima kwenda kwenye Kiswahili
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 21 Oktoba, 2022



Mapendekezo 18 ya Ripoti yanasomwa na Prof. Rwekaza Mukandala
  1. Kikosi kazi kinapendekeza mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa iruhusiwe kufanyika kwa mujibu wa katiba na sheria, mikutano ya ndani ya vyama vya siasa iendelee kufanyika bila vikwazo vyovyote, yafanyike marekebisho ya sheria ili kuhakikisha mikutano ya hadhara inafanyika kwa ufanisi.
  2. Sheria ya vyama vya siasa ifanyiwe marekebisho ili kulipatia baraza la vyama vya siasa linaloundwa na vyama vyenyewe mamkala ya kushughulikia swala la uvunjifu wa maadili ya vyama vya siasa kupitia kamati yake ya maadili, msajili wa vyama vya siasa aandae muongozo wa chaguzi za ndani za vyama vya siasa.
  3. Mfumo wa sasa wa kugawa ruzuku kwa vyama vya siasa uendelee, isipokuwa 10% ya fedha zinazotolewa sasa zitolewe kwa mgawanyo sawa kwa vyama vyote vyenye usajili kamili.
  4. Tume ya taifa ya Uchaguzi isilazimike kufuata amri au maagizo ya mtu yeyote, idara yoyote ya serikali, chama chochote cha siasa, taasisi au asasi yoyote na utendaji wake uruhusiwe kuhojiwa kwenye mahakama ya juu ili kuongeza uwajibikaji wa tume.
  5. Wajumbe wa tume ya taifa ya uchaguzi wateuliwe na kamati inayoongozwa na jaji mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (mwenyekiti) jaji mkuu wa Zanzibar (M/mwenyekiti), kamishna wa serkretarieti ya maadili ya viongozi wa umma Tanzania bara, mwenyekiti wa tume ya maadili ya viongozi wa umma ya Zbar, mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu na wajumbe 2 watakaoteuliwa na jaji mkuu wa JMT baada ya kupendekezwa na chama cha wanasheria Tanganyika na chama cha wanasheria Zbar. Pia, angalau wajumbe wawili wa uteuzi wawe wanawake, sifa za kuwa mwenyekiti, makamu au mjumbe ziainishwe, nafasi za ujumbe zitangazwe, watu wafanyiwe usaili kisha majina yapelekwe kwa Rais kwa uteuzi
  6. Matokeo ya Rais jahojiwe kwenye Mahakama ya juu
  7. Wasimamizi wa uchaguzi wazingatie sheria, maadili, weledi, uwazi na ushirikishwaji wa wadau wakati wa kufanya kazi zao. Wasimamizi watakaokiuka taratibu wawajibishwe kwa mujibu wa sheria.
  8. Tume ya taifa ya uchaguzi ipewe fedha kwa wakati ili iweze kutelekeza majukumu yake ipasavyo.
  9. Itungwe sheria kusimania shughuli za tume ya uchaguzi, pia iwepo sheria moja ya kusimamia chaguzi zote badaa ya uwepo wa sheria mbili kama sasa, maafisa wa uchaguzi watakao engua wagombea kushiriki uchaguzi bila kuzingatia sheria na weledi wawajibishwe kwa mujibu wa sheria.
  10. Matumizi ya tehama kwenye uchaguzi yaboreshwe na kuongezwa.
  11. Sharti ya uwepo wa sera ya jinsia liwepo kwenye kila chama cha siasa, na ujumuishi wa makundi maalumu, pia ushiriki wa jinsia moja kwenye vyombo vya maamuzi isipungue 40%
  12. Sheria zinazokwamisha ushiriki wa wa watu wenye ulemavu kwenye siasa ziangaliwe upya
  13. Juhudi za ushirikishwaji wa vijana kwenye siasa ziongezwe
  14. Serikali iongeze utoaji wa elimu ya uraia, pia ifundishwe kwenye ngazi zote za elimu, pia mtaala wa elimu uzingatoe elimu ya uraia.
  15. Swala la rushwa litamkwe katika katiba ya nchi ili wananchi waelewe
  16. Kuanzishwe utaratibu wa mijadaa kila mwaka itakayohusisha viongozi wakubwa wa kitaifa na kisiasa ili kudumisha mshikamano, mahakama iwe ni mamlaka ya mwisho ya kuamua pindi maridhiano yanapokwama
  17. Wanahabari waunde chombo cha kusimamia wanahabari na vyombo vyao, vyombo vya umma vitoe muda sawa wa kutangaza habari za wagombea wa vyama vyote kwa usawa, uwepo mchakato wa wazi wa kuwajibisha vyombo vya habari badala ya kufungiwa pekee na mkurugenzi wa habari na mawasiliano
  18. Mchakato wa katiba mpya uendelee, hata hivyo mjadala wa kitaifa kuhusu katiba mpya uanze kabla ya kuanza kwa mchakato wa kuandika katiba mpya ili kujadili ajenda muhimu za muungano, mamkala ya Rais, Rushwa, tume ya uchaguzi n.k
Maneno ya Rais Samia Suhuhu Hassan
Kazi hii imechukua miezi 10, haikuwa rahisi. Pengine ningewaacha ingechukua zaidi ya muda huu, lakini mimi pia navutwa shati.

Tumepokea, na kama mlivyoona ripoti yenu ina mambo kadhaa, sisi kwenye serikali inabidi tujipange vikosi kadhaa, na wengine kati yenu tutawaomba mje kwenye vikosi kazi hivyo tujadili.

Siyo kwamba leo tumepewa ripoti ya kikosi kazi, kesho tutaanza kutekeleza hapana. Tumepoke, na wananchi wasikie tumepokea na tutafanyia kazi.

Na nyie watu wa siasa mjichambue, ni kazi ya jaji mtungi na watu wake. Nakubailiana na hoja ya 40% ya wanawake kwenye vyama vya siasa.

Mgao wa ruzuku tutauangalia, hatuwezi kusema tutaongeza fedha zaidi sababu ni swala la kibajeti.

Matumizi ya teknolojia kwenye tume ya uchaguzi ni muhimu, ili teknolojia inayotumika iweze kutoa matarajio ambayo watu wanataka.

Tume ya uchaguzi tutalikalia kitako, ya serikali yatakwenda na ya ripoti nayo tutayaangalia.

Mijadala ya kisiasa kila mwaka iwepo, kaeni mjijadili, msijadili tu serikali, mjijadili na ninyi wenyewe. Mijadala heathy, hata serikali inaweza kuwezesha mijadala hii.

Wanawake mara nyingi nafasi muhimu wakigombea wanaambiwa kaa upande, au wanaambiwa njoo chukua hiyo gombea. Ukikuta wanawake kawekwa ni mwepesi mno, kapangwa kumsindikiza mtu. Kwa hili nakubaliana nao, ni pamoja na kuwasomesha wanawake, kuwatia moyo kwamba wanaweza.

Rushwa ni kidonda ndugu, hakuna hata chama kimoja kimenusurika hapa. Hakuna chama ambacho hakifanyi, nadhani ni tabia ambayo tunatakiwa kuibadilisha. Watu wajue, kuchaguliwa si mimi, ni chama. Hili la Rushwa, tujitazameni sote.

Maswala ya mikutano hakuna anayekataa, lakini lazima kuwe na jicho. Hatutaki kurudi tulikotoka, polisi wataanza tena kupiga watu. Tunaposema kwamba kanuni lazima tuzitazame siyo kwa nia mbaya, ni nia njema. Lazima tutazame kanuni na sheria ndipo turuhusu.

Naipongeza Kamati. Wamejaribu sana sana kuukaribia mstari unaoliliwa miaka yote na Watanzania. Mstari wa usawa na uwazi kwenye siasa za Tanzania.

Lajini Kamati hii imekwepa kabisa tena kwa tahadhari kubwa eneo la Mgombea Binafsi. Haki hii inaitaka serikali kuwajibika kwa kuiongezea kwenye sheria ya Uchaguzi

Pia, wangesema kabisa, sheria ya Uchaguzi iwaengue wakurugezi wa Halmashauri na Manispaa kuwa Wasimamizi wa Uchaguzi. Kila wilaya kuwepo na vetting ya kupata wasimamizi wa Uchaguzi hadi ngazi ya Kata
 
Back
Top Bottom