Posho za Wabunge na Maisha ya Dodoma

William umeleta pointi ya msingi suala la kujiuliza kinachofanya Dodoma hoteli ziwe ni nini? Ukweli wabunge wenyewe wanapaswa kulaumiwa wameweka ubinafsi mbele hawajali maslahi ya Taifa, hata leo serikali ikeleta muswaada wa kujenga Hosteli utapingwa; wao wanachotaka ni pesa; nina uhakika kama wabunge wangeweka maslahi ya Taifa mbele hosteli ingekuwapo, au bunge liwepo wakati vyuo vimefungwa Dodoma pana vyuo vingi tu tatizo wabunge wetu wanataka kuwa kama wafalme, hata posho zikiongezwa hiyo halitakuwa suluhisho kumbuka ongezeko la posho litasababisha wafanyibiashara kuongeza bei ya bidhaa zao. Unamkumbuka congressman wa Texas aliyeamua kuwa atalala ofisini kwake wakati wa vikao vya congress hawa wetu wataweza?

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
-
- Sasa yes, inapotaka kutatua tatizo la posho za wabunge lazima uliangalie hilo cause ni reality, Wabunge wetu pesa tunazo walipa atleast nusu zinaishia kwenye mikono ya wananchi wa majimbo yao, hiyo ni FACT, lakini mimi naongelea niliyoyaona Dodoma as a reality, sio hadithi za mtaani!

William.

Kuwalipa wananchi wa majimbo Yao ni sehemu ya kazi Yao Kama ilivyoainishwa kwenye Katiba? Sidhani Kama Hiyo ni sehemu ya kazi Yao. Wabunge wanafanya hivyo kwa sababu wanataka favor kutoka kwa wapiga kura wao. Kwa Nini watake favor hiyo????? What are they buying????
 
Hakuna hoja hapa..wewe kula,lala na ishi vizuri baba yako alishatengeneza mazingira..nchi hii wabunge ni 357 tu,watanzania ni milioni 45..huwezi kuuangalia ugumu wa maisha kwa watu 357 tu..huko ni kutaka kukwepa majukumu ya msingi ya serekali..kuondoa umasikini kwa wananchi wake
 
Unahitaji kuwa na ngozi ngumu kama kiboko kutetea posho ya 200,00 kwa wabunge kwenye nchi ya kipato cha chini ya dola!!
 
Mzee W. J. Malecela vipi kuhusu wanaosimamia na kutumia sheria hizo? Hapa naongelea mahakimu,majaji na mapolisi. Hawa unawazungumziaje? Je,hawahitaji hiyo miposho? Je,hawapo katika mazingira ya kupokea rushwa ili wapindishe usimamizi na utekelezaji wa sheria?

Mzee hapa labda kama una ajenda nyingine,lakini kama ni suala la ugumu wa maisha,hili ni janga la kitaifa. Hakuna cadre iliyo exceptional.

hawa hawahitaji posho....kwanza wao kazi yao 'sio hatari kwa taifa' kwa hiyo ni sahihi kuishi maeneo 'dangerous'kwani si viongozi wa taifa loh......
 
Nyingi ya hotel hizo ni za kwao wenyewe hivyo kama maisha ni magumu si wapunguze bei ili waweke usawa, kuna kipi cha kuufanya usingizi wa usiku mmoja kuulipia 70+? na ukichunguza mji huo ndo mana hauendelei maji na umeme ni hapo mjini tu nenda kilomita kadhaa nje ya mji hakuna haduma muhimu wananchi wanadhiki mpaka miguuni.
 
kaka, willium,

hivi maisha unayoyajua ni ya wabunge tu? hebu siku moja jaribu kuongelea maisha ya watumishi wengine wa umma, wakulima, wafugaji, wavuvi nk ambao naamini hata hapo dodoma wapo, kisha tuone kama hiyo posho ya laki 1+ kwa siku bado ni ndogo kwa wabunge

ubarikiwe mpendwa
 
nimetoa hoja kutokana na niliyoyaona na ni kawaida yetu sisi waafrika kwa wananchi kuwafuata wabunge Dodoma kwenye kikao kuwaomba misaada!

William.

Mzee sasa hapa nawe unaingia mkenge wa kufikiria kwa "wanasiasa wa kawaida". Wabunge ndiyo wanataka mzunguko wa wao kuombwa na wapiga kura husikatike kamwe.
Mzee kwanini wabunge hao wasitafute suluhisho la wapiga kura wao kuwa ombaomba?
Huoni kama hiyo ni janja ya wabunge hao kuwafanya wapiga kura wao kuwa tegemezi daima?!
 
- Wabunge ni tofauti sana na hao wengine, WAO NI WATUNGA SHERIA! sasa mwenye kutaka sheria mbovu kwa wananchi akiwapa rushwa na kutupitishia sheria mbovu kwa taifa utasema ni sawa na wengine serikalini?


William.

mpendwa,

hii kauli ni ya hatari sana. nadhani ingekuwa enzi za mwalimu, hata kuitoa hadharani hapa kwenye mtandao usingethubutu. hebu yarudie maadili ya watanzania. au rejea katiba ya JMT, au hata imani ya kwanza ya chama chako cha CCM: "BINADAMU WOTE NI SAWA"

tafadhari, usichochee matabaka katika jamii yetu

ubarikiwe sana
 
- Wabunge ni tofauti sana na hao wengine, WAO NI WATUNGA SHERIA! sasa mwenye kutaka sheria mbovu kwa wananchi akiwapa rushwa na kutupitishia sheria mbovu kwa taifa utasema ni sawa na wengine serikalini?


William.

Nimekushangaaa sana malecela , kwani kila siku ni kutunga sheria ? Je mahandisi afanye nini ambaye kila siku ni kusaini mikataba .Posho ni kidogo ndiyo lakini ni kwa wote maana tunagawana sungura
 
Hakuna hoja hapa..wewe kula,lala na ishi vizuri baba yako alishatengeneza mazingira..nchi hii wabunge ni 357 tu,watanzania ni milioni 45..huwezi kuuangalia ugumu wa maisha kwa watu 357 tu..huko ni kutaka kukwepa majukumu ya msingi ya serekali..kuondoa umasikini kwa wananchi wake

- Wabunge 357 wanatunga sheria za wananchi Millioni 40, so wako tofauti!

William.
 
Ugumu wa maisha ni kwa kila mtanzania, Mbunge, mhandisi, mwalimu, shehe, padri, mwanafunzi, mkulima, mfugaji, mwizi, kahaba, mfungwa na kadhalika.

Hakuna sababu ya kuwachukulia wabunge Kama watu ambao wake affected zaidi ya wengine, wananchi wote wanapigika sana mtaani, wanapigika mpaka wanaichukia CCM, kwa sera zake ambazo zinadhana kwamba Mtu anayepata posho ya 200,000/= kwa siku ana maisha magumu hivyo inabidi aangaliwe kipekee na Yule mkulima anayeshindia alfu kwa siku anasahaulika.

Maisha ni magumu huku mtaani, ondokeni Dodoma Hotel, tokeni bungeni kwa masaa, tokeni ofisini na kwenye magari yenu muone watu wanavyopigika huku mtaani.

kweli mkuu huu ugumu haupo dodoma tu bali ni tz nzima!
 
kweli mkuu huu ugumu haupo dodoma tu bali ni tz nzima!

- Watunga sheria ni muhimu sana kuliko wengine wote kwenye taifa, ndio maana China inasonga mbele kwa sababu wanalijua hilo na wanlijali sana kuliko yote, wanahakikisha wabunge wao hawapo kwenye mazingara ya kwua wazi kwa rushwa ndio maan wakiwashika kunakuwa hakuna excuse, maana walishawatengenezea mazingara bora dawa ni Risasi tu!

- Na sisi tujifunze, hii hoja ijadilike sasa, sio lazima posho iwe laki mbili, lakini something must be done now!

William.
 
- Ni watunga sheria hawa, so ni tofauti sana na watu wengine kwenye serikali!

William.

ni kweli tofauti.....maana hawa wanapiga makofi kila siku ilhali....

Mwalimu huko tandahimba kijijini anaishi kwa hofu ya simba mshahara 430,000 gross
mtumishi wa serikali anayehakikisha shughuli zinaenda ipasavyo sh 410,000
polisi anayehatarisha maisha mshahara wake aibu hata kuutaja...
Mahakimu
madaktari


halafu unasema hawahitaji posho? Mazingira magumu wanayofanya kazi unayajua wewe? Ama kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaaa

ila ni kweli kazi yao ni tofauti .......maana hata wanavyohatarisha maisha wacha wahatarishe.....hawana 'umuhimu' kwa taifa


Kwa style hii haistaajabishi ccm inapoteza mvuto kila siku... Mmejaa matabaka vichwani mwenu.... Kuna watu muhimu na wasio muhimu...kuna ambao pamoja na kufanya kazi hatarishi au kuishi mazingira hatarishi hamuwazi kuwapz posho ya mazingira magumu, mnawaza kujiongezea posho....ubinafsi ndio utawaangamiza......

Na sitashangaa hali hii kwenda mpaka majimboni....... Hawawawazii wananchi na shida zao, bali waona matumbo yao..........

Wabunge wa ccm wasipobadlili tabia 2015 wataingia 100 tu bungeni...

Hawaoni hali halisi.....
Hawaoni wananchi walivyowachoka.....
 
- Wabunge ni tofauti sana na hao wengine, WAO NI WATUNGA SHERIA! sasa mwenye kutaka sheria mbovu kwa wananchi akiwapa rushwa na kutupitishia sheria mbovu kwa taifa utasema ni sawa na wengine serikalini?


William.

Nyamaza wewe Lemutuz wanatunga sheria gani? kazi kugonga meza tuu na kubishana na wabunge hodari wa CDM labda waongeze posho kwa wabunge wa CDM ambao utendaji wao tunauona. Unataka Ukope hela kwa mama yako nini? ha ha ha ha! ha
 
- Watunga sheria ni muhimu sana kuliko wengine wote kwenye taifa, ndio maana China inasonga mbele kwa sababu wanalijua hilo na wanlijali sana kuliko yote, wanahakikisha wabunge wao hawapo kwenye mazingara ya kwua wazi kwa rushwa ndio maan wakiwashika kunakuwa hakuna excuse, maana walishawatengenezea mazingara bora dawa ni Risasi tu!

- Na sisi tujifunze, hii hoja ijadilike sasa, sio lazima posho iwe laki mbili, lakini something must be done now!

William.

watunga sheria ni muhimu kuliko wanaotekeleza sheria?

Kuna umuhimu gani wa kutunga sheria ambazo hazitekelezwi kama sasa hivi? Kila mtu anajiamulia anavyotaka? Sheria zimebakia vitabuni...

Hujajiuliza hilo? Hebu litafakari uje na uzi wake........

Watunga sheria hawana maana kama sheria zenyewe hazifuatwi, kama sheria zenyewe hazitekelezwi, na hazitekelezwi kutokana na 'kutowajali' kimaslahi watekeleza sheria......na kwa mtindo huo watunga sheria wataishia kuwa wapiga makofi........
 
kweli halishiba hamkumbuki mwenye njaa. wewe unaopata wapi ujasiri wa kusema "kwamba wengi wa Wabunge waliokuwa wanapinga posho ni wale wenye uwezo mkubwa sana kipesa kwamba hata hawahitaji hiyo posho ya sh. 70,000 kwa siku maana kwao ni peanuts na ni wachache sana, ninasema hii hoja ijadiliwe tena, tunawaweka wabunge wengi pagumu sana kimaishana hata kutuongoza".wezo wako wa kufikiria ni mdogo sana, na si mwenzetu hujui maisha wanaishi watanzania kwa sasa. umeshafanya ubunge ni ajira.

- Heshima mbele JF, hivi karibuni nilikuwa Dodoma hili la Wabunge na posho limenishitua sana ukizingatia kwamba nilikuwa mmoja wa wananchi waliopinga sana Wabunge kuongezewa posho, there I was in Dodoma, hotel ya hadhi ya wabunge ni Dodoma hotel, bei ya chini sana kwa chumba ni Sh. 65,000 kwa siku; ukienda mtaani ni sh. 50,000 kwa siku, I mean bado wabunge hawajala na ku-deal na wananchi kutoka majimbo yao ambao humiminika kila siku Wabunge wanapokuwa Dodoma, kuwalilia shida za binafsi.

- Serikali itafute suluhisho la hili tatizo kwa sababu ni tatizo, tunaawaacha wabunge in an open field ya kupokea rushwa, nimeona Wabunge wengine wakiishi sehemu ambazo ni very dangerous kwa kiongozi wa taifa tunayemtegemea kuishi, halafu unakuta magazeti yakifurahia mbunge apigwa mapanga, mbunge aibiwa, I mean as taifa we have to do something, nchi nyingi Duniani, infact hata Zambia tu Serikali imewajengea Special Hostel wabunge wake kwenye maeneo ya viwanja vya bunge kupunguza hili tatizo la posho, I mean kwa hali niliyoiona hili tatizo halikwepeki ni lazima lizungumzike.

- Nilichojifunza kule Dodoma ni kwamba wengi wa Wabunge waliokuwa wanapinga posho ni wale wenye uwezo mkubwa sana kipesa kwamba hata hawahitaji hiyo posho ya sh. 70,000 kwa siku maana kwao ni peanuts na ni wachache sana, ninasema hii hoja ijadiliwe tena, tunawaweka wabunge wengi pagumu sana kimaishana hata kutuongoza.



William John Samwel Malecela @DSM City!
 
- Wabunge ni tofauti sana na hao wengine, WAO NI WATUNGA SHERIA! sasa mwenye kutaka sheria mbovu kwa wananchi akiwapa rushwa na kutupitishia sheria mbovu kwa taifa utasema ni sawa na wengine serikalini?


William.

Kwa hoja yako ya leo umenikumbusha ule usemi wa Mzee Malechela aliousema kwamba wanaolaumu utendaji uongozi wa Reli ya kati..."they can go to hell"

Watanzania wamechoka mbaya hawana pesa mifukoni, Walimu ndio kabisa hawapati mafao yao na hata mshahara ni kiduchu, Madaktari mpaka wa leo wamedanganywa kama watoto, Wanajeshi hawalipwi haki zao za msingi kama nauli ya likizo, Mapolisi hali taabani, angalia vurugu za Ikwiriri zimesababishwa na ukata wa hao mapolisi uliopelekea wao kuwa na urafiki na wafugaji wa kupeana rushwa, Ukweli William sasa nakuona kuwa unaanza kuonyesha wewe umeathiriwa na umatabaka kwani umefikia kutaka kutuaminisha kuwa Mbunge/Mtunga sheria ni mtu asiyestahili kupata machungu ya hali mbaya ya uchumi tulionao watanzania, Unajaribu kutuaminisha kuwa wabunge wawapo Dodoma hufuatwa na watu wengi kwa ajili ya kusaidia matatizo yao,..yes huo ni wajibu wao na si lazima awakirimu kwa pesa kwani kama hakuingia kwa rushwa naamini atawaambia kuwa sina posho kwa ajili yenu,

William jaribu siku mmoja pale Dodoma umfuate Kudadadeeeki umuombe nauli ya kurudia USA , nafikiri pamoja na akili yake ilivyo lakini atakupa jibu linalostahili
 
Back
Top Bottom