Polisi wamwaachia huru mzee aliyekutwa gesti na mtoto wa miaka 14

Rosena

Member
Sep 11, 2012
51
4
Usiku wa kuamkia leo, huko Iringa sehemu za Kihesa katika gesti fulani kuna mzee amekutwa na mtoto wa miaka 14. Wateja waliokuwa ndani ya gesti hiyo hawakupendezwa na kitendo hicho cha kinyama kwani mzee huyo pia alionekana kuwa na afya mbaya. Ndipo walipoamua kuwashirikisha wahudumu wa gesti hiyo kwamba kitendo hicho ni kinyume cha sheria hivyo ikapigwa simu polisi kituo cha kihesa, na polisi walifika na kumchukua mtuhumiwa pamoja na mtoto huyo. Leo asubuhi mzee amerudi na maelezo kuwa ameachiwa baada ya kuwapa polisi shilingi laki tatu.Yule mtoto amechukuliwa Mikumi kwa mama yake na mama pamoja na mtoto wamedanganywa na mzee yule kwamba amemchukua ili amsomeshe.
 
kisheria ni kosa. mtoto ambaye yuko chini ya miaka 18 hata kama atakubali, hiyo ni statutory rape, labda awe mkewe...hapo ndo kwenye matatizo sasa kwasababu dini ya kiislam inaruhusu mwanamke kuolewa hata akiwa na miaka 12 alimradi tu awe amevunja ungo...yaani akivunja ungo tu hata kama ana miaka gani ruksa kwao kumwoa. ndio maana wamekuwa wakishinikiza sana kwamba sheria ya ndoa ya mwaka 1971 inakiuka misingi ya dini ya kiislam..ukiona jamaa wameng'ang'ana sana kushambulia sheria ya ndoa, ujue wanataka kubemenda watoto walio chini ya miaka hata ya 18. ajabu gani hii jamani?
 
Back
Top Bottom