Usiku wa kuamkia leo, huko Iringa sehemu za Kihesa katika gesti fulani kuna mzee amekutwa na mtoto wa miaka 14. Wateja waliokuwa ndani ya gesti hiyo hawakupendezwa na kitendo hicho cha kinyama kwani mzee huyo pia alionekana kuwa na afya mbaya. Ndipo walipoamua kuwashirikisha wahudumu wa gesti hiyo kwamba kitendo hicho ni kinyume cha sheria hivyo ikapigwa simu polisi kituo cha kihesa, na polisi walifika na kumchukua mtuhumiwa pamoja na mtoto huyo. Leo asubuhi mzee amerudi na maelezo kuwa ameachiwa baada ya kuwapa polisi shilingi laki tatu.Yule mtoto amechukuliwa Mikumi kwa mama yake na mama pamoja na mtoto wamedanganywa na mzee yule kwamba amemchukua ili amsomeshe.