MWANAWAVITTO
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 258
- 220
Katika tathmini ya takribani miaka mitatu,kituo kikuu cha polisi ARUSHA MJINI kimekuwa kikiiba mali za Raia,kumekuwa na matukio ya fedha kuibiwa ndani ya kituo kwa mfano Fedha za KIBO PALACE.Siyo hizo pekee, wanaiba simu za mkononi, pochi za fedha nk.Nimefuatilia kwa ukaribu madai ya watu ambao mali zao zinafikishwa kituoni hapo yakiwemo MAGARI na PIKIPIKI na kugundua WIZI MKUBWA wa VIPURI unaofanywa ndani kituo.Betri za magari na pikipiki, radio na vifaa vinginevyo vimekuwa vikipotea kituoni hapo.Ukiongeza vitendo vya rushwa na unyanyasaji kituo hiki kinapoteza hadhi ya kuitwa "ARUSHA POLICE CENTRE"natoa wito kwa IGP SAID MWEMA kuunda kikosi kazi cha kuchunguza tuhuma hizi na kisha kuwachukulia hatua wahusika, vinginevyo itanilazimu kubadili maana halisi ya JESHI LA POLISI ARUSHA.Naomba kuwasilisha