Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
Aliyejifungua mapacha watano atoboa siri
na Ali Lityawi, Kahama
SHIJA Maige, mkazi wa Kata ya Bulungwa, wilayani Kahama ambaye hivi karibu alijifungua mapacha watano, amesema alikimbia katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando Mjini Mwanza kwa kuwa tangu watoto wake waanze kufa hajawahi kuona maiti zao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Shija alisema yeye alikuwa amelazwa wodi namba nne huku watoto wake wakiwa wodi namba mbili na kwamba alikuwa akienda wakati wa kuwanyonyesha tu, lakini kila alipokuwa akienda alikuta kuna upungufu wa watoto wake bila wauguzi kumuonyesha maiti zao.
Mwanamke huyo ambaye alishawahi kuzaa watoto mapacha wawili katika mimba zake sita alisema pia alilazimika kukimbia kwa kuwa wanawake wenzake waliokuwa wamelazwa naye walikuwa wakimwambia kuendelea kuwepo katika maeneo hayo hata yeye angepelekwa machinjioni walikokuwa wakipelekwa watoto wake.
Alidai kuwa hata mumewe aliyekuwa amefika siku moja kumuangalia alikuwa ameshauawa, hali ambayo ilimfanya atoroke na kumuacha mtoto wake mmoja aliyebaki.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Meja mstaafu Bahati Matala, Ofisa Tawala wa Wilaya ya Kahama, Paulo Cheyo, alisema kutokana na madai ya mama huyo aliuagiza uongozi wa hospitali ya wilaya kuhakikisha suala hilo linafanyiwa kazi na mama huyo anarudishwa hospitali ya Bugango chini ya uangalizi wa muuguzi kutoka hospitali hiyo.
Cheyo alisema mbali ya hilo, ofisi yake inahitaji kupata ufafanuzi wa kina kuhusu mama huyo tangu alipokuja katika Hospitali ya Wilaya hadi kupelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando na pia mama huyo aende katika hospitali ya Bugando kujiridhisha juu ya kufariki kwa wanawe.
Kwa upande wake, Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama Heleni Membe alisema kuwa maneno anayoongea mama huyo yanatokana na kuchanganyikiwa baada ya kupata kifafa cha uzazi na kufariki kwa watoto wake hao wanne.
na Ali Lityawi, Kahama
SHIJA Maige, mkazi wa Kata ya Bulungwa, wilayani Kahama ambaye hivi karibu alijifungua mapacha watano, amesema alikimbia katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando Mjini Mwanza kwa kuwa tangu watoto wake waanze kufa hajawahi kuona maiti zao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Shija alisema yeye alikuwa amelazwa wodi namba nne huku watoto wake wakiwa wodi namba mbili na kwamba alikuwa akienda wakati wa kuwanyonyesha tu, lakini kila alipokuwa akienda alikuta kuna upungufu wa watoto wake bila wauguzi kumuonyesha maiti zao.
Mwanamke huyo ambaye alishawahi kuzaa watoto mapacha wawili katika mimba zake sita alisema pia alilazimika kukimbia kwa kuwa wanawake wenzake waliokuwa wamelazwa naye walikuwa wakimwambia kuendelea kuwepo katika maeneo hayo hata yeye angepelekwa machinjioni walikokuwa wakipelekwa watoto wake.
Alidai kuwa hata mumewe aliyekuwa amefika siku moja kumuangalia alikuwa ameshauawa, hali ambayo ilimfanya atoroke na kumuacha mtoto wake mmoja aliyebaki.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Meja mstaafu Bahati Matala, Ofisa Tawala wa Wilaya ya Kahama, Paulo Cheyo, alisema kutokana na madai ya mama huyo aliuagiza uongozi wa hospitali ya wilaya kuhakikisha suala hilo linafanyiwa kazi na mama huyo anarudishwa hospitali ya Bugango chini ya uangalizi wa muuguzi kutoka hospitali hiyo.
Cheyo alisema mbali ya hilo, ofisi yake inahitaji kupata ufafanuzi wa kina kuhusu mama huyo tangu alipokuja katika Hospitali ya Wilaya hadi kupelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando na pia mama huyo aende katika hospitali ya Bugando kujiridhisha juu ya kufariki kwa wanawe.
Kwa upande wake, Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama Heleni Membe alisema kuwa maneno anayoongea mama huyo yanatokana na kuchanganyikiwa baada ya kupata kifafa cha uzazi na kufariki kwa watoto wake hao wanne.