apolycaripto
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 644
- 225
Katika kipindi cha maswali na majibu ya papo kwa papo,baada ya kuulizwa na Mh. Mbowe juu ya mgogoro wa Jimbo la Arusha.Pinda alianza kwa kuelezea ni jinsi gani Mh.Godbless Lema kuwa chanzo cha vurugu.Nanukuu mgogoro huu umesababishwa na Mbunge wa Arusha(Lema) ambaye ni mtu wa vurugu vurugu hivi.Hiki ndicho kilichomuuzi Lema na kudai yote kuwa Waziri Mkuu kadanganya Bunge na Wananchi.
Kauli ya Waziri Mkuu ilinitia mashaka kwa kuwa nilikuwa simjui vizuri Mh. Lema kama kweli ni mtu wa vurugu vurugu kama alivyosema.Jana nimeingiwa na hofu juu ya uwezo wa Mh. Godbless Lema hasa katika medani za kisiasa.Lema anaongozwa na siasa za enzi za kina Isike na Mirambo kuwa kiongozi bora sharti uwe mfano kwa kila kitu hata kama ni upuuzi kwa sasa.Angalia jana,umetoka mahakamani na wenzio kila mmoja kapanda gari yake na kuelekea anakojua.Wewe (Lema) mbali na kusalimiana unazua agenda nyingine kwa midadi eti peoples power safari ya mguu kama zuzu mtaani.Hii si akili ya kawaida kwa kiongozi anayefikiri.Sasa nimeamini kuwa Lema ni tofauti na Viongozi wengine wa CHADEMA.Hizi ni siasa za kufukuza ndege porini ili kupata kitoweo.
Vijana wengi Arusha hawana kazi,hivyo tusitumie fursa hii kuwaangamiza na polisi.Ikiwa anadhamira ya kweli,ajaribu kuwaunganisha na mfuko wake wa jimbo baadhi yao ili kupunguza makali ya kimaisha badala ya kuwatundika kwemye milipuko ya wapiganaji (polisi) nayeye kubakia salama.sifa za kijinga eti mbunge wetu haogopi polisi! mbona jana alikimbia na kutoweka kusikojulikana.
Kauli ya Waziri Mkuu ilinitia mashaka kwa kuwa nilikuwa simjui vizuri Mh. Lema kama kweli ni mtu wa vurugu vurugu kama alivyosema.Jana nimeingiwa na hofu juu ya uwezo wa Mh. Godbless Lema hasa katika medani za kisiasa.Lema anaongozwa na siasa za enzi za kina Isike na Mirambo kuwa kiongozi bora sharti uwe mfano kwa kila kitu hata kama ni upuuzi kwa sasa.Angalia jana,umetoka mahakamani na wenzio kila mmoja kapanda gari yake na kuelekea anakojua.Wewe (Lema) mbali na kusalimiana unazua agenda nyingine kwa midadi eti peoples power safari ya mguu kama zuzu mtaani.Hii si akili ya kawaida kwa kiongozi anayefikiri.Sasa nimeamini kuwa Lema ni tofauti na Viongozi wengine wa CHADEMA.Hizi ni siasa za kufukuza ndege porini ili kupata kitoweo.
Vijana wengi Arusha hawana kazi,hivyo tusitumie fursa hii kuwaangamiza na polisi.Ikiwa anadhamira ya kweli,ajaribu kuwaunganisha na mfuko wake wa jimbo baadhi yao ili kupunguza makali ya kimaisha badala ya kuwatundika kwemye milipuko ya wapiganaji (polisi) nayeye kubakia salama.sifa za kijinga eti mbunge wetu haogopi polisi! mbona jana alikimbia na kutoweka kusikojulikana.