Pichani, mawaziri hao lazima wapumzishwe na kushtakiwa

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,896
SAM_1114.JPG
SAM_1125.JPG
 
tena peleka mahakamani kabsaaa. Hiyo list angeongezwa Zee toka gombe hapo Wassira na Lukuvi dah ingekuwa poa kinoma
 
tena peleka mahakamani kabsaaa. Hiyo list angeongezwa Zee toka gombe hapo Wassira na Lukuvi dah ingekuwa poa kinoma

Hahaha, wanalindana hawa, utakuta hawa kwenye list baadhi wanabaki hasa walio maswahiba na Mkulu
 
Ni fedheha kuongozwa na viongozi wezi na vibaka kama hawa waliosheheni ndaaniya chama cha CCM. Hospitalini hakuna dawa,watoto wetu wanasomea sehemu hatarishi na dhalilishi, mishahara inalipwa kwa mbinde, wazee wetu wanakufa kwa kukosa matunzo ya pensheni ambayo licha ya kuwa ndogo, dhalilishi lakini inashindikana kuilipa au inalipwa ki magumashi, sarafu yetu inazidi kuwa karatasi kwa kupoteza thamani kila kukicha.
Kwa upande mwingine majambazi haya ndaniya sare za CCM yanatanua watoto wao wakisoma nje ya nchi au katika "Academys" wanaendesha magari yenye thamani ya kuendesha hospitali kadhaakwa mwaka bila tatizo, vibaka hawa hawatumii fedha waliyoiroga na kuimaliza thamani, kila anayepatwa na masahibu tunaambiwa alikutwa na dola! Ngedere hawa lazima wang'oke, tena si wao tu ingefaa wang'olewe wote kuanzia Rais haditarishi ili nchi ianze upya kwa maana hata Rais mwenyewe ametajwa mara kibao kuhusika na vikashfa kashfa hadi vya kununuliwa suti na kugawana ngawira za uuzaji wa nyumba kimagumashi.
Yote haya yamefanyika Polisi wakiwepo, idara zao za upelelezi zikiendelea kunyonya kodi zetu, dude linaloitwa TAKUKURU likiwepo tena likifanya kazi ya kuwachamba uharo wao hawa jamaa, Usalama wataifa wakiwepo, tena bila aibu wakiendelea kuzibanjua "Imprest" za kazi walizofanya za kuwalinda vibaka hawa kwa gharama ya sisi waathirika! Vibaka hawa wameiba kila mahali; kuanzia kwenye Halmashauri, mbuga za wanyama hadi kwenye kihenge chetu walala hoi - Benki Kuu!!!! Cha kushangaza Bado tunawaita waheshimiwa na wanapigiwa saluti na askari tunaowalipa kwa kodi zetu! Iko wapi fahari ya kuwa mtanzania tuliyojengewa miaka ya nyuma na Hayati Babu yetu Nyerere? Iko wapi jeuri ya kuwaita majirani waliokuwa kama sisi wakatihuo "manyang'au"? Uko wapi utu wa Binadamu wote ni sawa?
Tanzania, Ooh Tanzania, tunakuombea kwa Mungu usife kabla ya 2015 maana unavuja damu nyingi mno na yaelekea kuna wachache tu wa kukusaidia. Naomba unihesabu mimikuwa mmoja wapo, naomba wahesabu wana CHADEMA kuwa wamoja wapo.
Watanzania mnangoja nini sasa msijiunge na harakati mpya za ukombozi wa mama yetu Tanzania???
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI NA UWALINDE WANAHARAKATI WA UKOMBOZI. A LUTA CONTINUA.
 
Ni fedheha kuongozwa na viongozi wezi na vibaka kama hawa waliosheheni ndani ya chama cha CCM. Hospitalini hakuna dawa,watoto wetu wanasomea sehemu hatarishi na dhalilishi, mishahara inalipwa kwa mbinde, wazee wetu wanakufa kwa kukosa matunzo ya pensheni ambayo licha ya kuwa ndogo, dhalilishi lakini inashindikana kuilipa au inalipwa ki magumashi, sarafu yetu inazidi kuwa karatasi kwa kupoteza thamani kila kukicha.
Kwa upande mwingine majambazi haya ndaniya sare za CCM yanatanua watoto wao wakisoma nje ya nchi au katika "Academys" wanaendesha magari yenye thamani ya kuendesha hospitali kadhaakwa mwaka bila tatizo, vibaka hawa hawatumii fedha waliyoiroga na kuimaliza thamani, kila anayepatwa na masahibu tunaambiwa alikutwa na dola! Ngedere hawa lazima wang'oke, tena si wao tu ingefaa wang'olewe wote kuanzia Rais haditarishi ili nchi ianze upya kwa maana hata Rais mwenyewe ametajwa mara kibao kuhusika na vikashfa kashfa hadi vya kununuliwa suti na kugawana ngawira za uuzaji wa nyumba kimagumashi.
Yote haya yamefanyika Polisi wakiwepo, idara zao za upelelezi zikiendelea kunyonya kodi zetu, dude linaloitwa TAKUKURU likiwepo tena likifanya kazi ya kuwachamba uharo wao hawa jamaa, Usalama wataifa wakiwepo, tena bila aibu wakiendelea kuzibanjua "Imprest" za kazi walizofanya za kuwalinda vibaka hawa kwa gharama ya sisi waathirika! Vibaka hawa wameiba kila mahali; kuanzia kwenye Halmashauri, mbuga za wanyama hadi kwenye kihenge chetu walala hoi - Benki Kuu!!!! Cha kushangaza Bado tunawaita waheshimiwa na wanapigiwa saluti na askari tunaowalipa kwa kodi zetu! Iko wapi fahari ya kuwa mtanzania tuliyojengewa miaka ya nyuma na Hayati Babu yetu Nyerere? Iko wapi jeuri ya kuwaita majirani waliokuwa kama sisi wakatihuo "manyang'au"? Uko wapi utu wa Binadamu wote ni sawa?
Tanzania, Ooh Tanzania, tunakuombea kwa Mungu usife kabla ya 2015 maana unavuja damu nyingi mno na yaelekea kuna wachache tu wa kukusaidia. Naomba unihesabu mimikuwa mmoja wapo, naomba wahesabu wana CHADEMA kuwa wamoja wapo.
Watanzania mnangoja nini sasa msijiunge na harakati mpya za ukombozi wa mama yetu Tanzania???
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI NA UWALINDE WANAHARAKATI WA UKOMBOZI. A LUTA CONTINUA.
 
Ni vizuri tumchambuwe kila mmoja na tuhuma dhidi yake kupata ukweli. Nundu anapigwa vita kwa kuzuwia ulaji si vinginevyo. Yeye ameeleza, na tunaotaka kuelewa tumeelewa,kuwa hana investor anayempigia debe bali anataka wote waliojitokeza kuwekeza au kukopesha nchi ili Gati 13 na 14 zijengwe kwa manufaa ya nchi WASHINDANISHWE ili apatikane anayetufaa. Anataka wapelekewe Request for Proposal ili waeleze conditions zao zipambanishwe.

Shinikizo la mafisadi wa TPA, Wizarani na Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge na kwengineko ni kuwa apewe kazi hiyo mjenzi China Communications Construction Company (CCCC) na Tanzania ikope US$540,000,000 kutoka China Exim Bank na pesa hizo alipwe huyu mjenzi zote bila kupunguzwa. Gharama hii ya US$540,000,000 ameikasimu CCCC yeye mwenyewe. Papo hapo hao wawekezaji na wakopeshaji wanasema magati hayo hayagharimu pesa hizo na makadirio yao ni US$300,000,000

CCCC wanawapambe chungu nzima wakusinikiza hilo hata wamemchukuwa Naibu Waziri Uchukuzi kumlipia gharama zote na kumtembeza kuona walikojenga bandari Uchina na baadaye Mauretania na Equatorial Guinea. Alienda Uchina kwa kibali cha Waziri Mkuu baada ya kumdanganya kuwa Waziri hakuwepo kupendekeza apatiwe kibali, jambo ambao si kweli. Alipoomba Kibali hicho tarehe 17 Novemba 2011 Waziri Mkuu alikuwa Mpanda kwenye Investors Forum ya mikoa mitatu na Waziri alikuwa Dar es Salam. Alipopeleka kibali cha kwenda Mauretania na Equatorial Guinea Waziri Mkuu alimshtukia na kukirudisha kwa Waziri aridhie. Waziri hakuridhia kwani alipopata melekezo hayo jamaa alikuwa amekwishaondoka bila ya idhini ya mtu yeyote. Hivyo alienda kukutana na CCCC Mauretania na Equatorial Guinea BILA KIBALI CHOCHOTE. Na aliporejea akapeleka ripoti yake kwa Waziri Mkuu akipendekeza CCCC wapewe ujenzi huo. Waziri Mkuu alishtuka tena na kumtaka apeleke ripoti hiyo kwa Waziri sio kwake.

Kilichofanyika dhidi ya Waziri Nundu ni kumgeuzia kibao baada ya mbinu zote za kumtaka awaachie mafisadi na CCCC yao kulitesa taifa kushindikana. Hapo ikazushwa kuwa kuna MOU kati yake na mmoja wa wawekezaji aitwaye China Merchants Holdings (CMH) na ikasemwa kuwa MOU inampa CMH kuendesha gati hizo kwa miaka 45 baada ya ujenzi. Nundu alisema bungeni, nami nimetafiti kuwa hakuna MOU kama hiyo na yote yanayosemwa dhidi yake ni uongo na uzushi. Nundu aliwasilisha kwa Spika MOU kati ya Wizara na CMH ambayo kimsingi inampa CMH fursa ya kufanya utafiti ili ajiridhishe kama ni busara kuwekeza kwenye mradi huo. MOU za namna hii Wizara na taAsisi zake zimesaini na wawekezaji na mabenki wengi waliyojitokeza na zina muda ili kama hakuna kinachoendelea mwekezaji au benki hiyo inatemwa.

Nundu ni mkombozi si fisadi. Mafisadi wanageuza kibao ili CCCC ambaye ni mjenzi aliyekasimu gharama yeye mwenyewe apewe maradi huo kwa gharama hizo na taifa lilipe. Yeye kama mjenzi inabidi ashindanishwe na wajenzi wengine, jambo ambalo mafisadi hawalitaki kabisa. CCCC wakipewa mradi huu sisi tunaojuwa undani wa kushinikizwa Nundu aondoke ili mafisadi wafanye mambo yao kama kawaida, tutautowa ukweli wote bila kuficha chochote. Tunayajuwa yote! Mungu ibariki Tanzania, Mungu walinde wakombozi kama Waziri Nundu
 
Ni vizuri tumchambuwe kila mmoja na tuhuma dhidi yake kupata ukweli. Nundu anapigwa vita kwa kuzuwia ulaji si vinginevyo. Yeye ameeleza, na tunaotaka kuelewa tumeelewa,kuwa hana investor anayempigia debe bali anataka wote waliojitokeza kuwekeza au kukopesha nchi ili Gati 13 na 14 zijengwe kwa manufaa ya nchi WASHINDANISHWE ili apatikane anayetufaa. Anataka wapelekewe Request for Proposal ili waeleze conditions zao zipambanishwe.

Shinikizo la mafisadi wa TPA, Wizarani na Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge na kwengineko ni kuwa apewe kazi hiyo mjenzi China Communications Construction Company (CCCC) na Tanzania ikope US$540,000,000 kutoka China Exim Bank na pesa hizo alipwe huyu mjenzi zote bila kupunguzwa. Gharama hii ya US$540,000,000 ameikasimu CCCC yeye mwenyewe. Papo hapo hao wawekezaji na wakopeshaji wanasema magati hayo hayagharimu pesa hizo na makadirio yao ni US$300,000,000

CCCC wanawapambe chungu nzima wakusinikiza hilo hata wamemchukuwa Naibu Waziri Uchukuzi kumlipia gharama zote na kumtembeza kuona walikojenga bandari Uchina na baadaye Mauretania na Equatorial Guinea. Alienda Uchina kwa kibali cha Waziri Mkuu baada ya kumdanganya kuwa Waziri hakuwepo kupendekeza apatiwe kibali, jambo ambao si kweli. Alipoomba Kibali hicho tarehe 17 Novemba 2011 Waziri Mkuu alikuwa Mpanda kwenye Investors Forum ya mikoa mitatu na Waziri alikuwa Dar es Salam. Alipopeleka kibali cha kwenda Mauretania na Equatorial Guinea Waziri Mkuu alimshtukia na kukirudisha kwa Waziri aridhie. Waziri hakuridhia kwani alipopata melekezo hayo jamaa alikuwa amekwishaondoka bila ya idhini ya mtu yeyote. Hivyo alienda kukutana na CCCC Mauretania na Equatorial Guinea BILA KIBALI CHOCHOTE. Na aliporejea akapeleka ripoti yake kwa Waziri Mkuu akipendekeza CCCC wapewe ujenzi huo. Waziri Mkuu alishtuka tena na kumtaka apeleke ripoti hiyo kwa Waziri sio kwake.

Kilichofanyika dhidi ya Waziri Nundu ni kumgeuzia kibao baada ya mbinu zote za kumtaka awaachie mafisadi na CCCC yao kulitesa taifa kushindikana. Hapo ikazushwa kuwa kuna MOU kati yake na mmoja wa wawekezaji aitwaye China Merchants Holdings (CMH) na ikasemwa kuwa MOU inampa CMH kuendesha gati hizo kwa miaka 45 baada ya ujenzi. Nundu alisema bungeni, nami nimetafiti kuwa hakuna MOU kama hiyo na yote yanayosemwa dhidi yake ni uongo na uzushi. Nundu aliwasilisha kwa Spika MOU kati ya Wizara na CMH ambayo kimsingi inampa CMH fursa ya kufanya utafiti ili ajiridhishe kama ni busara kuwekeza kwenye mradi huo. MOU za namna hii Wizara na taAsisi zake zimesaini na wawekezaji na mabenki wengi waliyojitokeza na zina muda ili kama hakuna kinachoendelea mwekezaji au benki hiyo inatemwa.

Nundu ni mkombozi si fisadi. Mafisadi wanageuza kibao ili CCCC ambaye ni mjenzi aliyekasimu gharama yeye mwenyewe apewe maradi huo kwa gharama hizo na taifa lilipe. Yeye kama mjenzi inabidi ashindanishwe na wajenzi wengine, jambo ambalo mafisadi hawalitaki kabisa. CCCC wakipewa mradi huu sisi tunaojuwa undani wa kushinikizwa Nundu aondoke ili mafisadi wafanye mambo yao kama kawaida, tutautowa ukweli wote bila kuficha chochote. Tunayajuwa yote! Mungu ibariki Tanzania, Mungu walinde wakombozi kama Waziri Nundu
 
Hii nchi inaubabaishaji sijawahi kuona sio kama ccm hamna watu wazur kiutendaji but mkuu amezidiwa na ushkaji na atakuwa anapata 50% ya wizi wa hao masela wake haiwezekani awalinde hvyo
 
Binafsi sijawa na hali ya kumpigia debe waziri fulani, ila tu vyombo husika katika kutathmini utendaji wao likiwemo bunge na mdhibiti wa hesabu za serikali wameona hawafai tuheshimu vyombo hivyo. Huku kuanza kuwapigia debe watuhumiwa ni kuingilia jambo tusilokuwa na uhakika kwa kujenga utetezi tokana na utetezi wa mtuhumiwa.
 
Ni vizuri tumchambuwe kila mmoja na tuhuma dhidi yake kupata ukweli. Nundu anapigwa vita kwa kuzuwia ulaji si vinginevyo. Yeye ameeleza, na tunaotaka kuelewa tumeelewa,kuwa hana investor anayempigia debe bali anataka wote waliojitokeza kuwekeza au kukopesha nchi ili Gati 13 na 14 zijengwe kwa manufaa ya nchi WASHINDANISHWE ili apatikane anayetufaa. Anataka wapelekewe Request for Proposal ili waeleze conditions zao zipambanishwe.

Shinikizo la mafisadi wa TPA, Wizarani na Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge na kwengineko ni kuwa apewe kazi hiyo mjenzi China Communications Construction Company (CCCC) na Tanzania ikope US$540,000,000 kutoka China Exim Bank na pesa hizo alipwe huyu mjenzi zote bila kupunguzwa. Gharama hii ya US$540,000,000 ameikasimu CCCC yeye mwenyewe. Papo hapo hao wawekezaji na wakopeshaji wanasema magati hayo hayagharimu pesa hizo na makadirio yao ni US$300,000,000

CCCC wanawapambe chungu nzima wakusinikiza hilo hata wamemchukuwa Naibu Waziri Uchukuzi kumlipia gharama zote na kumtembeza kuona walikojenga bandari Uchina na baadaye Mauretania na Equatorial Guinea. Alienda Uchina kwa kibali cha Waziri Mkuu baada ya kumdanganya kuwa Waziri hakuwepo kupendekeza apatiwe kibali, jambo ambao si kweli. Alipoomba Kibali hicho tarehe 17 Novemba 2011 Waziri Mkuu alikuwa Mpanda kwenye Investors Forum ya mikoa mitatu na Waziri alikuwa Dar es Salam. Alipopeleka kibali cha kwenda Mauretania na Equatorial Guinea Waziri Mkuu alimshtukia na kukirudisha kwa Waziri aridhie. Waziri hakuridhia kwani alipopata melekezo hayo jamaa alikuwa amekwishaondoka bila ya idhini ya mtu yeyote. Hivyo alienda kukutana na CCCC Mauretania na Equatorial Guinea BILA KIBALI CHOCHOTE. Na aliporejea akapeleka ripoti yake kwa Waziri Mkuu akipendekeza CCCC wapewe ujenzi huo. Waziri Mkuu alishtuka tena na kumtaka apeleke ripoti hiyo kwa Waziri sio kwake.

Kilichofanyika dhidi ya Waziri Nundu ni kumgeuzia kibao baada ya mbinu zote za kumtaka awaachie mafisadi na CCCC yao kulitesa taifa kushindikana. Hapo ikazushwa kuwa kuna MOU kati yake na mmoja wa wawekezaji aitwaye China Merchants Holdings (CMH) na ikasemwa kuwa MOU inampa CMH kuendesha gati hizo kwa miaka 45 baada ya ujenzi. Nundu alisema bungeni, nami nimetafiti kuwa hakuna MOU kama hiyo na yote yanayosemwa dhidi yake ni uongo na uzushi. Nundu aliwasilisha kwa Spika MOU kati ya Wizara na CMH ambayo kimsingi inampa CMH fursa ya kufanya utafiti ili ajiridhishe kama ni busara kuwekeza kwenye mradi huo. MOU za namna hii Wizara na taAsisi zake zimesaini na wawekezaji na mabenki wengi waliyojitokeza na zina muda ili kama hakuna kinachoendelea mwekezaji au benki hiyo inatemwa.

Nundu ni mkombozi si fisadi. Mafisadi wanageuza kibao ili CCCC ambaye ni mjenzi aliyekasimu gharama yeye mwenyewe apewe maradi huo kwa gharama hizo na taifa lilipe. Yeye kama mjenzi inabidi ashindanishwe na wajenzi wengine, jambo ambalo mafisadi hawalitaki kabisa. CCCC wakipewa mradi huu sisi tunaojuwa undani wa kushinikizwa Nundu aondoke ili mafisadi wafanye mambo yao kama kawaida, tutautowa ukweli wote bila kuficha chochote. Tunayajuwa yote! Mungu ibariki Tanzania, Mungu walinde wakombozi kama Waziri Nundu


Nahisi wewe ni Nundu mwenyewe. Unachopigania si integrity yako bali ni hofu ya kuenguliwa uwaziri maana ndiyo tu umeonja "utamu" wake. Ndiyo maana kuna mahala humu ndani kuna thread inazungumzia dhana(concept) ya "AMEULA" ambayo mchangiaji moja kasema ilianzishwa na huyo huyo aliyekuteua kuwa waziri.
 
tatizo chama cha vilaza wezi tupu. mkuu ndo usiseme katoa muda wa kuchakachua km wa madeni yA EPA eti wajiondoe. Unapewa kura na maskini uwe prezdaa unashindwa fukuza vimeo. Chama kinakufia hk.
 
Ni fedheha kuongozwa na viongozi wezi na vibaka kama hawa waliosheheni ndani ya chama cha CCM. Hospitalini hakuna dawa,watoto wetu wanasomea sehemu hatarishi na dhalilishi, mishahara inalipwa kwa mbinde, wazee wetu wanakufa kwa kukosa matunzo ya pensheni ambayo licha ya kuwa ndogo, dhalilishi lakini inashindikana kuilipa au inalipwa ki magumashi, sarafu yetu inazidi kuwa karatasi kwa kupoteza thamani kila kukicha.
Kwa upande mwingine majambazi haya ndaniya sare za CCM yanatanua watoto wao wakisoma nje ya nchi au katika "Academys" wanaendesha magari yenye thamani ya kuendesha hospitali kadhaakwa mwaka bila tatizo, vibaka hawa hawatumii fedha waliyoiroga na kuimaliza thamani, kila anayepatwa na masahibu tunaambiwa alikutwa na dola! Ngedere hawa lazima wang'oke, tena si wao tu ingefaa wang'olewe wote kuanzia Rais haditarishi ili nchi ianze upya kwa maana hata Rais mwenyewe ametajwa mara kibao kuhusika na vikashfa kashfa hadi vya kununuliwa suti na kugawana ngawira za uuzaji wa nyumba kimagumashi.
Yote haya yamefanyika Polisi wakiwepo, idara zao za upelelezi zikiendelea kunyonya kodi zetu, dude linaloitwa TAKUKURU likiwepo tena likifanya kazi ya kuwachamba uharo wao hawa jamaa, Usalama wataifa wakiwepo, tena bila aibu wakiendelea kuzibanjua "Imprest" za kazi walizofanya za kuwalinda vibaka hawa kwa gharama ya sisi waathirika! Vibaka hawa wameiba kila mahali; kuanzia kwenye Halmashauri, mbuga za wanyama hadi kwenye kihenge chetu walala hoi - Benki Kuu!!!! Cha kushangaza Bado tunawaita waheshimiwa na wanapigiwa saluti na askari tunaowalipa kwa kodi zetu! Iko wapi fahari ya kuwa mtanzania tuliyojengewa miaka ya nyuma na Hayati Babu yetu Nyerere? Iko wapi jeuri ya kuwaita majirani waliokuwa kama sisi wakatihuo "manyang'au"? Uko wapi utu wa Binadamu wote ni sawa?
Tanzania, Ooh Tanzania, tunakuombea kwa Mungu usife kabla ya 2015 maana unavuja damu nyingi mno na yaelekea kuna wachache tu wa kukusaidia. Naomba unihesabu mimikuwa mmoja wapo, naomba wahesabu wana CHADEMA kuwa wamoja wapo.
Watanzania mnangoja nini sasa msijiunge na harakati mpya za ukombozi wa mama yetu Tanzania???
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI NA UWALINDE WANAHARAKATI WA UKOMBOZI. A LUTA CONTINUA.
Nakuunga mkono 100%
 
Back
Top Bottom