benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alirejea nchini jana kutoka nchini Namibia.
Akiwa nchini humo baada ya kuhitimisha Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Troika Jijini Windhoek nchini Namibia, alipata wasaa wa kuzungumza na sehemu ya Watanzania waishio nchini humo, baadhi wakiwa na familia zao tarehe 08 Mei, 2023.
Katika baadhi ya picha zilizotolewa na kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Samia alionekana akiwa mwenye furaha na watato wa Watanzania wananoishi nchini humo huku nyingine akionekana anapiga nao "soga" kidogo baada ya kuzungumza na Watanzania (Diaspora) katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Jijini Windhoek
Katika picha nyingi ambazo wapiga picha wa Rais huwa wanapiga sehemu kubwa huwa "hazizungumzi" na zikiwa zinakosa "context" lakini kwa picha hizi za watoto nchini Namibia pengine sasa wameanza kugundua kuwa kumpiga picha Rais sio tu kubonyeza Camera na kutoa picha.
Kila picha ya Kiongozi wa nchi inapaswa kuzungumza, inapaswa kubeba ujumbe unaojitosheleza bila hata kuandikiwa maelezo "caption",. Vitengo hivyo kwa nchi za wenzetu hapa jirani tu kama Rwanda wameliweza sana hilo kwa picha wanazozitoa za Rais PK. (Angalizo neno picha wanazozitoa halijatumia bahati mbaya hapa"
Siku za karibuni tumekuwa na picha zenye mwelekeo wa matakwa niliyoyataja hapo juu lakini binafsi niwapongeze kwa picha za Rais Samia akiwa na watoto nchini Namibia, waendelee kushikilia hapohapo.
Vipi kwako mdau, ipi ni picha bora ya Rais Samia tangu aingie Ikulu.
Akiwa nchini humo baada ya kuhitimisha Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Troika Jijini Windhoek nchini Namibia, alipata wasaa wa kuzungumza na sehemu ya Watanzania waishio nchini humo, baadhi wakiwa na familia zao tarehe 08 Mei, 2023.
Katika baadhi ya picha zilizotolewa na kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Samia alionekana akiwa mwenye furaha na watato wa Watanzania wananoishi nchini humo huku nyingine akionekana anapiga nao "soga" kidogo baada ya kuzungumza na Watanzania (Diaspora) katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Jijini Windhoek
Katika picha nyingi ambazo wapiga picha wa Rais huwa wanapiga sehemu kubwa huwa "hazizungumzi" na zikiwa zinakosa "context" lakini kwa picha hizi za watoto nchini Namibia pengine sasa wameanza kugundua kuwa kumpiga picha Rais sio tu kubonyeza Camera na kutoa picha.
Kila picha ya Kiongozi wa nchi inapaswa kuzungumza, inapaswa kubeba ujumbe unaojitosheleza bila hata kuandikiwa maelezo "caption",. Vitengo hivyo kwa nchi za wenzetu hapa jirani tu kama Rwanda wameliweza sana hilo kwa picha wanazozitoa za Rais PK. (Angalizo neno picha wanazozitoa halijatumia bahati mbaya hapa"
Siku za karibuni tumekuwa na picha zenye mwelekeo wa matakwa niliyoyataja hapo juu lakini binafsi niwapongeze kwa picha za Rais Samia akiwa na watoto nchini Namibia, waendelee kushikilia hapohapo.
Vipi kwako mdau, ipi ni picha bora ya Rais Samia tangu aingie Ikulu.